Logo
Chapisha ukurasa huu

بسم الله الرحمن الرحيم

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan: Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wamzuru Ammi Sadiq (Mwenyezi Mungu Amrehemu) miongoni mwa Kizazi cha Kwanza

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/ Wilayah Sudan ulimzuru Ammi Sadiq, (Mwenyezi Mungu Amrehemu) ambaye ni miongoni mwa kizazi cha kwanza nyumbani kwake mnamo Jumanne, 16 Juni 2020 M. Ujumbe huo ulimjumuisha: Ustadh Hatem Jaafar, Ustadh Hassan Ismail, Mwanachama wa Baraza la Wilayah ya Sudan, Ustadh Naser Ridha Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Mawasiliano, Ustadh Muhammad Jama (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, na Ustadh Abdullah Hussein, Mratibu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano, na Ustadh Khalid Abdullah na Hadi Hamed, Wanachama wa Hizb ut Tahrir walio andamana na Ustadh Fakhurdeen Mallah.

Kwa wale wasiomjua Ammi Sadiq, yeye ni miongoni mwa kizazi cha kwanza cha Wabebaji Ulinganizi nchini Sudan aliye lingania Khilafah Rashidah kwa Njia ya Utume katika miaka ya sitini wakati wa enzi ya Raisi Nimeiry. Yeye na baadhi ya Mashabab walihukumiwa kifo lakini ni kwa qadhaa ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kwamba walitumikia kifungo pekee cha miaka kadhaa gerezani.

Ziara hii ilihitimishwa kwa Mashabab kuomba dua.

Mjumbe wa Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan

Imebadilishwa mara ya mwisho mnamoAlhamisi, 25 Juni 2020 13:15
Template Design © Joomla Templates | GavickPro. All rights reserved.