Logo
Chapisha ukurasa huu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Maafisa wa Jeshi WachaMungu Hupenda Jihad, Wakitafuta Shahada au Ushindi kwa Ajili ya Radhi za Mwenyezi Mungu (swt)

Uislamu sio tu umefaradhisha Jihad pekee, umejenga hamu nzito ya Jihad ambayo imeutofautisha Ummah huu na mataifa mengine kwa karne kumi na tatu. Umeuwezesha Ummah huu kubeba hasara kubwa kwa hiari, ili kuwashinda maadui wa Uislamu na Waislamu. Kwa kumtegemea Mwenyezi Mungu pekee, majeshi ya Waislamu yaliyashinda majeshi makubwa zaidi yaliyopigana kwa msingi wa imani fisidifu, ulinzi wa eneo au ubwana wa rangi ya ngozi. Kutimiza dori yao ya kuhakikisha Uislamu unatawala, majeshi ya Waislamu yaliondoa vizingiti vya kimada katika utabikishaji wa kivitendo wa Uislamu. Hivyo basi watu waliingia katika Uislamu makundi kwa makundi, na kuasisi misingi mipana ya Ummah wa leo, unaojumuisha matabaka ya rangi tofauti tofauti.

Hata baada ya kuvunjwa Khilafah mnamo 1924 M, mapenzi ya Jihad ndani ya Ummah huwahofisha maadui wa Waislamu. Miaka 25 ya kumbukumbu ya mauwaji ya Srebrenica yana mfano ndani yake. Huku takriban wanaume na wavulana wa Kiislamu 8,000 wa Bosnia wakiwa wameuwawa na Waserbia kwa kipindi cha siku kumi na moja, baada ya vikosi vya Kiholanzi vya Umoja wa Mataifa kuutelekeza mji wa Srebrenica mnamo 11 Julai 1995, Uingereza ilikuwa na wasiwasi kwamba vikosi vya Waislamu vilivyokuweko chini ya amri ya Umoja wa Mataifa vingevunja safu kupigana na Waserbia. Mapenzi ya Jihad yaliyoiporomosha Urusi ya Kisovieti hadi chini nchini Afghanistan, sasa yameilazimisha Amerika kuomba mpango wa kuokoa uso wake. Mapenzi ya Jihad katika Waislamu wa Kashmir Iliyokaliwa huihofisha Dola ya Kibaniani, ambayo imeiunganisha kwa nguvu Kashmir Iliyokaliwa mnamo 5 Agosti 2019, ilhali bado ingali inakumbana na upinzani mkali hadi leo.

Badala ya kukuuza mapenzi ya Jihad miongoni mwa majeshi, watawala wa Waislamu walioko sasa wanapigana kampeni kwa niaba ya dola za Kimagharibi na washirika wao, umbile la Kiyahudi na Dola ya Kibaniani, dhidi ya Kupingana katika njia ya Mwenyezi Mungu (swt). Ama watawala wa Pakistan, ni wachangamfu katika kudhoofisha hamu yenye harara ya Waislamu ndani ya jeshi la Pakistan ya kutangaza vita vya ukombozi wa Kashmir Iliyokaliwa. Badala ya kuwahamasisha maafisa wa Kiislamu na wanajeshi kupigana na kuikomboa Kashmir, wanawavunja moyo kutopigana na adui. Wanapigia debe fikra kwamba vita sio chaguo, ima kwa sababu ya adui kumiliki silaha za kinuklia au udhaifu wa uchumi wetu. Ama Waislamu watukufu wanaopigana dhidi ya uvamizi popote walipo, watawala wa kiimla wa Waislamu huwashutumu kuwa "magaidi". Lakini, kama ilivyo miradi yote ya mkoloni, jaribio hili la kuangamiza Jihad litafeli kwa sababu Ummah daima umeshikamana na Mwenyezi Mungu (swt) na Mtume Wake (saw) na kheri iliyoko ndani yake imeenea sehemu zote za mwili wake, ikiwemo majeshi yake.

Afisa wa jeshi aliye mtiifu kwa Mwenyezi Mungu (swt) na Mtume Wake (saw) ni lazima aweke moyoni na akilini mwake kuwa Uislamu umeweka Jihad kama faradhi, ambayo kupuuzwa kwake kunakaribisha hasira za Mwenyezi Mungu (swt), huku kutekelezwa kwake huleta thawabu kubwa. Na azingatie yale yaliyotajwa kuhusu Jihad ndani ya Quran. Mwenyezi Mungu (swt) anasema,

[كُتِبَ عَلَيْكُمُ الْقِتَالُ وَهُوَ كُرْهٌ لَّكُمْ ۖ وَعَسَىٰ أَن تَكْرَهُوا شَيْئًا وَهُوَ خَيْرٌ لَّكُمْ ۖ وَعَسَىٰ أَن تُحِبُّوا شَيْئًا وَهُوَ شَرٌّ لَّكُمْ ۗ وَاللَّهُ يَعْلَمُ وَأَنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ]

“Mmeandikiwa kupigana vita, navyo vinachusha kwenu. Lakini huenda mkachukia kitu nacho ni kheri kwenu. Na huenda mkapenda kitu nacho ni shari kwenu. Na Mwenyezi Mungu anajua na nyinyi hamjui.” [Surah al-Baqarah: 216].

Katika Ayah hii tukufu, Mwenyezi Mungu (swt) amewafaradhisha Waislamu walio na uwezo wa kupigana kutekeleza Jihad dhidi ya uovu wa adui anayefanya ufasiki dhidi ya Uislamu. Wakati huo huo Uislamu unatambua kwamba kupigana ni kitu ambacho kinasababisha upinzani ndani ya nafsi na kuutibu vilivyo upinzani huo. Mwenyezi Mungu (swt) anasema,

 [وَهُوَ كُرْهٌ لَّكُمْ] “navyo vinachusha kwenu” ikimaanisha kuwa kupigana ni kugumu na kuzito nyoyoni. Hakika, kupigana ni kama Ayah ilivyo kusifia. Kunahusisha kuuliwa kama shahidi, kujeruhiwa, kupambana na maadui na kuvumilia uzito wa safari, ima katika baridi kali ya Siachen au joto kali la majangwa ya Thar. Mwenyezi Mungu (swt) kisha akasema, [وَعَسَى أَن تَكْرَهُواْ شَيْئًا وَهُوَ خَيْرٌ لَّكُم] “Lakini huenda mkachukia kitu nacho ni kheri kwenu” ikimaanisha, kupigana hufuatiwa na ushindi na tamkini juu ya adui.

Afisa wa jeshi Muislamu na azingatie yale yaliyotajwa kuhusu Jihad katika Sunnah. Utukufu wa Jihad ni maarufu ndani ya Sunnah ya RasulAllah (saw). Imepokewa katika Sahih,

«مَنْ مَاتَ وَلَمْ يَغْزُ وَلَمْ يُحَدِّثْ نَفْسَهُ بِالْغَزْوِ، مَاتَ مِيتَةً جَاهِلِيَّــة»

“Yeyote anayekufa na hakupigana (yaani katika njia ya Mwenyezi Mungu), na wala hakutamani nafsi yake kupigana, amekufa kifo cha kijahiliya (zama kabla ya Uislamu). ” Katika siku ya ufunguzi (Al-Fath) (alipoifungua Makkah), Mtume (saw) alisema,

«لَا هِجْرَةَ بَعْدَ الْفَتْحِ وَلكِنْ جِهَادٌ وَنِيَّةٌ، وَإِذَا اسْتُنْفِرْتُمْ فَانْفِرُوا»

“Hakuna Hijrah (kuhama kutoka Makkah hadi Al-Madinah) baada ya ufunguzi, lakini Jihad na nia njema pekee. Mkitakikana mtoke, basi tokeni.” [Bukhari] Mpokezi mkubwa wa Hadith, Az-Zuhri, anafafanua, “Jihad inahitajika kwa kila mtu, ima ajiunge kivitendo katika kupigana au abakie nyuma. Yeyote anaye bakia nyuma anahitajika kutoa usaidizi, endapo usaidizi utahitajika; kutoa msaada, endapo msaada utahitajika; na kusonga mbele, endapo ataamrishwa kufanya hivyo. Ikiwa hahitajiwi, basi atabakia nyuma.” Hakika, Sunnah inawalingania Waislamu katika majeshi kwa lile ambalo ni lazima lipendwe, kupigana katika Njia Yake (swt), kutafuta ushindi au shahada ya juu kabisa. RasulAllah (saw) amesema,

«مَا أَحَدٌ يَدْخُلُ الْجَنَّةَ يُحِبُّ أَنْ يَرْجِعَ إِلَى الدُّنْيَا وَلَهُ مَا عَلَى الأَرْضِ مِنْ شَىْءٍ، إِلاَّ الشَّهِيدُ، يَتَمَنَّى أَنْ يَرْجِعَ إِلَى الدُّنْيَا فَيُقْتَلَ عَشْرَ مَرَّاتٍ، لِمَا يَرَى مِنَ الْكَرَامَةِ»

“Hakuna yeyote atakaye ingia Peponi apende kurudi duniani hata alikuwa na kila kitu katika ardhi, isipokuwa Mujahid, atatamani arudi duniani auliwe mara kumi, kutokana na ile hadhi anayoiona (kutoka kwa Mwenyezi Mungu).” [Bukhari]

Afisa wa jeshi mwenye imani na azingatie kwamba kizazi cha kwanza na bora cha Uislamu kilitangaza Jihad ili kuwakomboa watu kutokana na watawala madhalimu, ili wauhisi Uislamu kivitendo. Mwenyezi Mungu (swt) anasema,

[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ قَاتِلُواْ الَّذِينَ يَلُونَكُم مِّنَ الْكُفَّارِ وَلْيَجِدُوا فِيكُمْ غِلْظَةً وَاعْلَمُواْ أَنَّ اللّهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ]

“Enyi mlio amini! Piganeni na wale makafiri walio karibu yenu, na wakute ugumu kwenu. Na jueni ya kwamba Mwenyezi Mungu yu pamoja na wacha- Mungu.” [Surah at-Tawbah 9: 123]. Mwenyezi Mungu (swt) anawaamrisha waumini, walio karibu zaidi na dola ya Kiislamu, kisha wale walio mbali zaidi. Hivyo, Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) alianza kuwapiga vita washirikina katika Bara Arabu. Pindi Mwenyezi Mungu (swt) alipompa udhibiti juu ya Makkah,

Al-Madinah, At-Ta'if, Yemen, Yamamah, Hajr, Khaybar, Hadhramawt na mikoa mingine ya Kiarabu, na makabila mbali mbali ya Kiarabu kuingia katika Uislamu makundi kwa makundi, yeye (saw) alianzisha Jihad dhidi ya Watu wa Kitabu. Yeye (saw) alianza maandalizi ya kupigana na Warumi ambao eneo lao lilikuwa karibu zaidi na Bara Arabu, na kwa hivyo, walikuwa na haki kubwa zaidi ya kulinganiwa Uislamu. Hivyo, Mtume (saw) alikwenda hadi akafika Tabuk katika mwaka wa tisa baada ya Hijrah yake, akiuongoza Ummah katika kuzikabili dola zilizokuwa zikiongoza zama hizo. 

Je, afisa mchaMungu wa jeshi atazingatia vitendo vya Makhalifah Waongofu (Khulafaa Rashideen) (ra), katika kuitekeleza kwao Jihad? Baada ya Mwenyezi Mungu (swt) kumchagulia Mtume (saw) Pepo Yake (swt), Khilafah kwa Njia ya Utume iliipa Jihad haki yake kamili. Khalifah wa Kwanza Muongofu, Abu Bakr As-Siddiq (ra), alianza kuyaandaa majeshi ya Kiislamu kupigana na Makruseda wa Kirumi na Majusi wa Kifursi. Kwa baraka ya misheni hii, Mwenyezi Mungu (swt) akamfungulia ardhi na kuleta udhalilifu kwa Kaisari na Kisra. Mikononi mwa Khalifah wa Pili Muongofu, 'Umar bin Al-Khattab (ra), Mwenyezi Mungu aliwadhalilisha makafiri, akafungua sehemu za mashariki na magharibi ya dunia kwa nuru ya utawala wa Kiislamu. Kisha, katika zama za Khalifah wa Tatu Muongofu 'Uthman (ra), ukweli usio na mithili wa Uislamu uliingia katika sehemu nyingi za dunia, ikiwemo bara dogo la India. Na Khalifah wa Nne Muongofu, Ali (ra), alimakinisha udhibiti juu ya eneo linalojumuisha mabara matatu. Hivyo basi, Makhalifah Waongofu (Khulafaa Rashideen) (ra) waliuendeleza Uislamu, wakitoa ushuhuda katika maneno ya Mwenyezi Mungu (swt)  [وَاعْلَمُواْ أَنَّ اللَّهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ]“Na jueni kwamba Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wachaMungu.”

Afisa mtambuzi wa jeshi na azingatie kwamba pindi Jihad inapopuuzwa, maadui huwa na hamu ya kuzishambulia kambi za Uislamu, na kupata udhibiti juu ya ardhi nyingi za Kiislamu. Ilhali, kila mtawala mwadilifu wa Kiislamu au kamanda wa jeshi anapotimiza amri ya Jihad, Mwenyezi Mungu (swt) humpa nusra na kumfanya mshindi juu ya adui. Hakika, utekelezaji wa Jihad huleta utukufu, huku upuuzaji wake huleta udhalilifu. RasulAllah (saw) alitangaza, «مَا تَرَكَ قَوْمٌ الْجِهَادَ إلاّ ذُلّوا»  “Hakuna watu wowote wanaoiacha Jihad isipokuwa hudhalilika.” [Ahmad]. Hivyo Waislamu walishindwa na Mongoli walipoipuuza Jihad na hatimaye wakawashinda kwa Jihad katika Ein Jaloot. Waislamu walioipuuza jihad walishindwa na Makruseda, hadi Salahudin alipowaongoza katika ushindi baada ya ushindi. Ama Khilafah Uthmani, iliendeleza Jihad kiasi ya kuwa miji mikuu ya Ulaya ikaanza kuanguka na ile ambayo ilikuwa bado haijachukuliwa ilitetemeka na kutetemeka.

Afisa wa jeshi anaye tafuta Jannah na azingatie hali ya Ummah hivi sasa. Kutoka katika yale yote yaliyoteremshwa na Mola wa Viumbe na historia ya watu wema na wale waliokuwa na mapungufu katika jukumu lao la Jihad, analazimika kusimama wapi? Hakika tangu Ummah upoteze ngao yake, Khilafah, mnamo 1924, ulipoteza pamoja nayo Jihad ya kufungua ardhi mpya kwa Uislamu. Zaidi ya hayo, maadui walizikalia ardhi zake, ima iwe ni umbile la Kiyahudi linaloikalia Palestina upande wa magharibi au Dola ya Kibaniani inayoikalia Kashmir upande wa mashariki. Lakini, kunapokosekana Khilafah, kupigana na makafiri wanaozikalia ardhi zetu, hakusimami. RasuAllah (saw) amesema,

«وَالْجِهَادُ مَاضٍ مُنْذُ بَعَثَنِيَ اللَّهُ إِلَى أَنْ يُقَاتِلَ آخِرُ أُمَّتِي الدَّجَّالَ لاَ يُبْطِلُهُ جَوْرُ جَائِرٍ وَلاَ عَدْلُ عَادِلٍ، وَالإِيمَانُ بِالأَقْدَارِ»

“Na Jihad imekuwepo tangu Mwenyezi Mungu aliponitumiliza hadi siku wa mwisho katika Ummah watakapopigana na Dajjal. Haibatilishwi na udhalimu wa dhalimu wala uadilifu wa mwadilifu, na imani juu ya Qadar.” [Abu Daud] Hivyo basi, kupigana na makafiri ni Faradhi, ima mtawala wa Waislamu awe ni Khalifah, au mtawala wa Waislamu awe hatawali kwa Uislamu. Kwa hayo, ni Faradhi juu ya majeshi ya Waislamu kuhamasika katika kupigana na majeshi vamizi.

Endapo mtawala atakubali kupeleka jeshi, basi atakuwa amefanya sahihi. Endapo atajaribu kulizuia jeshi kutokana na kupigana, akawa kizingiti njiani mwake, basi na kuwepo Salahuddin miongoni mwa jeshi hilo, atakayemkanyaga mtawala huyo chini ya miguu yake, na kuhamasisha jeshi kuzitakasa ardhi tukufu kutokana na uvamizi.

Ni wazi kwamba watawala wa Waislamu walioko sasa ni kizingiti njiani mwa afisa wa jeshi huyu na utiifu wake kwa Mwenyezi Mungu (swt). Watawala wa Waislamu walioko sasa wanatangaza kuwa vita sio chaguo na kumtangaza yule anayepigana kama adui wa Ummah. Watawala hawa huwatesa wale wanaobeba silaha wenyewe ima dhidi ya Waamerika nchini Afghanistan au Dola ya Kibaniani katika eneo lilikokaliwa la Kashmir. Baya zaidi, wamesawazisha mahusiano na wavamizi, ambapo inamakinisha zaidi uvamizi wao. Hili ni hata ingawa Mwenyezi Mungu (swt) ameamrisha,

 [وَاقْتُلُوهُمْ حَيْثُ ثَقِفْتُمُوهُمْ وَأَخْرِجُوهُمْ مِنْ حَيْثُ أَخْرَجُوكُمْ] “Na wauweni popote mwakutapo, na muwatoe popote walipo kutoeni” [Surah al-Baqarah 2: 191]. Ayah hii tukufu inatumika kwa wale wote wanaopigana na maadui wanaojishughulisha na kupigana na Uislamu na watu wake. Inamaanisha kwamba nishati yetu ni lazima itumiwe katika kupigana nao, kama ambavyo nishati yao inatumiwa katika kupigana na sisi, na katika kuwafurusha kutoka katika maeneo waliotufurusha.

Hivyo, ni wazi kwa afisa huyu wa jeshi kwamba watawala walioko sasa kamwe hawatayafurusha majeshi vamizi kutoka katika Ardhi za Waislamu, wala kurudisha Khilafah ili ufaradhi wa kufungua ardhi mpya kwa Uislamu uregee. Inamuangukia kila afisa wa jeshi kutibu hali hii mbaya. Kila afisa ni lazima asimame na Ummah na faradhi kubwa ya Jihad juu yao. Ni jukumu la maafisa wa jeshi kuwang'oa watawala walioko sasa, kunyosha Nusra yao kwa ajili ya kusimamisha tena Khilafah kwa Njia ya Utume (saw). Hapo na hapo pekee, ndipo watakapopigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu (swt), na kumaliza udhalimu kote ulimwenguni. Hivyo, maafisa wa jeshi wa Kiislamu wa leo na wawe mithili ya Maanswari waliomnusuru Mwenyezi Mungu (swt) na Mtume Wake (saw), kiasi ya kuwa Mwenyezi Mungu (swt) aliwasifu katika ayah Zake na malaika wakakimbilia katika mazishi ya bwana wao, Sa’ad bin Muadh (ra). Imepokewa na Tirmidh kutoka kwa Anas bin Malik (ra) kwamba RasulAllah (saw) alisema kuhusu mazishi ya Sa’ad bin Muadh (ra), «إِنَّ الْمَلَائِكَةَ كَانَتْ تَحْمِلُهُ» “Hakika, Malaika walikuwa wanambeba.” Waliobarikiwa hakika ni wale maafisa wa jeshi wa leo wanaofuata njia ya Maanswari.

Imeandikwa kwa Ajili ya Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir na
Musab Umair – Pakistan

Imebadilishwa mara ya mwisho mnamoJumatatu, 27 Julai 2020 12:49
Template Design © Joomla Templates | GavickPro. All rights reserved.