Logo
Chapisha ukurasa huu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Hizb ut Tahrir/ Wilayah Tunisia: Kisimamo cha Hali ya Juu Mbele ya Ubalozi wa Pakistan

Jumatatu asubuhi, Juni 21, 2021 ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilaya Tunisia ulizuru ubalozi wa Pakistan jijini Tunis ambapo ulimkabidhi kaimu wa shughuli za ubalozi huo nakala mbili za taarifa kwa vyombo vya habari ya Kiarabu na Kiurdu iliyotolewa na Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir inayoihutubia serikali ya Pakistan chini ya anwani, "Wito wa Kutaka Kumalizwa kwa Kupotezwa kwa Nguvu kwa Naveed Butt Nchini Pakistan" Ujumbe huo uliongozwa na Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano, Ustadh Yassin bin Yahya, Mwanachama wa Kamati Kuu ya Mawasiliano Ustadh Habib Al-Hajjaji, pamoja na Mkuu wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika wilaya ya Tunisia Dkt. Al Assad Al-Ajili.

Taarifa hiyo kwa vyombo vya habari ilitaja jinsi Ndugu Naveed alivyokuwa miongoni mwa Mashababu maarufu kutokana na kujitolea kwake katika Uislamu, tabia njema, mwanafikra mkweli, na aliye weza kutoa ruwaza ya "Ramani ya Barabara" ya kufikia Khilafah Rashida.

Mjumbe wa Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Tunisia

Template Design © Joomla Templates | GavickPro. All rights reserved.