Jumatano, 14 Muharram 1447 | 2025/07/09
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Utambuzi wa Urusi wa Serikali ya Afghanistan: Hatua Zaidi ya Kuzuia Kuibuka kwa Mfumo wa Kiislamu katika Kanda hii

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Afghanistan inauona utambuzi huu kama sehemu ya mchakato mpana ambao kwao utawala wa sasa utayeyushwa hatua kwa hatua ndani ya mfumo wa kimataifa wa kisekula wa dola ya kitaifa. Mfumo huu, baada ya muda, utaiweka mbali serikali hii na lengo kuu la Kiislamu la kusimamisha na kubeba Dini ya Mwenyezi Mungu (swt). Zaidi ya hayo, utambuzi huo unaweza kuigeuza Afghanistan kuwa uwanja wa vita vya kiushindani kati ya dola za kikanda na kimataifa.

Soma zaidi...

Hatua Mpya za UN na za Kanda za Kuoanisha Serikali Tawala ya Afghanistan ndani ya Mfumo wa Kisekula wa Dunia

Katika siku za hivi karibuni, Umoja wa Mataifa umekuwa ukifuatilia shughuli zake nchini Afghanistan kwa kasi zaidi kuliko hapo awali. Ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Masuala ya Kibinadamu jijini Kabul na Kandahar, pamoja na mwaliko wa Amir Khan Muttaqi-Waziri wa Mambo ya Nje wa serikali tawala nchini Qatar, inaashiria juhudi mpya za kuendeleza mipango ya kimataifa na kushawishi serikali ya Afghanistan.

Soma zaidi...

“Al-Wala wa-l-Bara” ni Hukmu Madhubuti ya Kiislamu na Kanuni Imara ya Kidini, na Haipaswi Kutolewa Kafara kwa ajili ya Maslahi ya Kitaifa

Adam Boehler, mwakilishi wa Kizayuni wa Trump katika masuala ya wafungwa, na Zalmay Khalilzad, mjumbe wa zamani wa Marekani katika masuala ya amani nchini Afghanistan, walikutana na Amir Khan Muttaqi, waziri wa mambo ya nje wa serikali inayotawala jijini Kabul. Kufuatia mkutano huu, serikali ilimwachilia huru mfungwa wa Kimarekani kama ishara ya nia njema. Amir Khan Muttaqi alitoa wito wa "mahusiano chanya ya kisiasa na kiuchumi na Marekani." Boehler alielezea hatua hii kama hatua kuelekea "kujenga uaminifu," na Khalilzad alisema kwamba "kuachiliwa huru kwa George Glezmann ni ishara ya nia njema ya Taliban."

Soma zaidi...

Makala ya Hivi Punde ya New York Times ni Mfano Mwingine wa Mkakati wa Kugawanya wa Marekani Miongoni mwa Mujahidina wa Afghanistan

Mnamo Oktoba 24, The New York Times ilichapisha makala kutokana na mahojiano na Waziri wa Mambo ya Ndani wa sasa wa Afghanistan, ikiwa ni pamoja na moja yenye kichwa, “Je, Mwanamgambo Aliyetafutwa Zaidi Afghanistan Sasa Ni Tumaini Lake Bora la Mabadiliko?” Makala hizi zinalenga kuleta mgawanyiko na kuwaelekeza baadhi ya Mujahidina katika maslahi ya Marekani.

Soma zaidi...

Sera ya Kinafiki ya Iran: Kuwasaliti Mashia ili Kuitumikia Marekani

Katika siku chache zilizopita, zaidi ya Waislamu 500 nchini Lebanon wameuawa shahidi kutokana na mashambulizi ya umbile la Kiyahudi, huku maelfu ya wengine wakijeruhiwa. Mashambulizi haya yamechukua aina mbalimbali, ikiwa ni pamoja na mlipuko wa vifaa vya mawasiliano kama vile pager na mifumo ya walkie talkie, pamoja na mashambulizi ya angani yanayolenga wanawake, wanaume na watoto.

Soma zaidi...

Mtazamo wa Serikali Tawala katika Uchimbaji Migodi Unaziimarisha Dola Adui (Muharib) na Kuwadhoofisha Waislamu wa Afghanistan

Wizara ya Madini na Petroli ya Afghanistan imetangaza kuwa katika kipindi cha miaka miwili na nusu iliyopita, zaidi ya dolari bilioni saba zimewekezwa katika sekta ya madini nchini Afghanistan. Katika mchakato huu, kando na makampuni ya ndani, makampuni kutoka Qatar, Uturuki, Urusi, Iran, China na Uingereza pia yamechukua dori kubwa. Huu unachukuliwa kuwa uwekezaji mkubwa zaidi katika uchimbaji madini katika historia ya Afghanistan.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Afghanistan Yawapongeza Waislamu Wote kwa Mnasaba wa Idd al-Adha na Inasisitiza Umoja wa Sherehe za Kidini kama Kanuni ya Sharia!

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Afghanistan inatoa pongezi na salamu za dhati kwa Waislamu wote duniani kote kwa mnasaba wa Idd ul-Adha. Vile vile tunamuomba Mwenyezi Mungu (swt) azikubali swala, ibada, mapambano na mihanga ya Waislamu wote kwa Rehema zake na aikubalie Hijja yao.

Soma zaidi...

Kufichua Uhalifu wa Wazayuni na Kupaza sauti ya Waislamu wanaodhulumiwa wa Palestina si ‘Uhalifu’ bali ni Wajibu wa Kiislamu wa Kila Muislamu!

Mnamo Novemba 2023, wabebaji Dawah wawili wa Hizb ut Tahrir walizuiliwa na maafisa wa ujasusi wa mkoa wa Nangarhar walipokuwa wakizungumza katika maandamano yaliyolenga kulaani mashambulizi ya kikatili ya umbile la Kizayuni huko Gaza.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu