Himaya Yashambulia Gaza - Sami Hamdi na Kifo cha Upinzani
- Imepeperushwa katika Amerika
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Baada ya umbile la Kizayuni kuifahamisha Marekani kuhusu uamuzi wake wa kuanza tena operesheni zake za uhalifu mjini Gaza, zaidi ya wakaazi 109 wa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina - wakiwemo watoto 46 - waliuawa shahidi, na wengine wengi walijeruhiwa tangu Jumanne jioni, 28 Oktoba 2025, katika mashambulizi ya anga yaliyofanywa kote Ukanda wa Gaza. Mabomu hayo yalilenga nyumba za raia na shule inayowahifadhi watu waliokimbia makaazi yao huko Beit Lahia, kaskazini mwa Gaza.



