Jumamosi, 26 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/18
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kongamano la Sharm El-Sheikh Ni Kutangaza Ushindi Juu ya Ummah, Kumakinisha Utiifu, na Kuimarisha Ukaliaji wa Kimabavu

Baada ya Trump kutangaza ushindi yeye na mfuasi wake, umbile la Kiyahudi, walioupata katika hotuba yake mbele ya Knesset. Ushindi huu ulipatikana dhidi ya raia wasio na silaha, wakiwemo wanawake, watoto, na wazee, pamoja na miti na mawe, Muuaji wa Gaza alielekea kwenye kongamano hilo liliopangwa na kibaraka wake nchini Misri, Sisi, ambapo aliwaalika wale wote waliokula njama dhidi ya ardhi iliyobarikiwa.

Soma zaidi...

Maadhimisho ya Mwaka wa Pili wa Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa Matunda Yaliyonyunyiziwa kwa Damu Safi

Tarehe 7 Oktoba iliadhimisha mwaka wa pili wa operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa. Miaka miwili kamili imepita tangu umbile nyakuzi kulenga watu wetu mjini Gaza, likiwafungulia mpangilio wa kuua, kuhamisha, na njaa, na kutumia viwango vya juu vya ushenzi na ukatili dhidi yao. Kwa hivyo ni nini kimebadilika kwa vita hivi vya dhulma?!

Soma zaidi...

Kuongezeka kwa Umwagaji damu kwenye Mpaka wa Pakistan na Afghanistan na Kushindwa kwa Pande zote mbili Kushikamana na Hukmu ya Mwenyezi Mungu

Mbali na sera ya “kujizuia” iliyotabanniwa na serikali za sasa za Pakistan na Afghanistan kwa maadui wa Umma – Mayahudi, Mabaniani, na Waamerika – Pakistan pamoja na Afghanistan zilitangaza kwamba makumi ya wanajeshi kutoka kila upande walikuwa wameuawa katika mapigano ambayo yalizuka kwenye mpaka wao wa pamoja. Makabiliano hayo yalianza mnamo Jumamosi jioni kwa operesheni iliyoanzishwa na vikosi vya Taliban, na kusababisha Islamabad kuapa kutoa jibu kali. Kabul, kwa upande wake, ilitangaza kuwa vikosi vyake vilifanya operesheni dhidi ya vikosi vya usalama vya Pakistan ili kulipiza kisasi kwa ukiukaji wa mara kwa mara na uvamizi wa anga unaofanywa na jeshi la Pakistan katika eneo la Afghanistan.

Soma zaidi...

Mapigano ya Hivi Karibuni Kati ya Afghanistan na Pakistan Yanatumikia Maslahi ya Sera za Kieneo za Marekani na India

Mnamo Jumamosi usiku, vikosi vya jeshi la Afghanistan na Pakistan vilishiriki katika mapigano ya mpakani, wakishambuliana nafasi za kila mmoja kwenye Mstari wa Durand; matokeo yake, pande zote mbili za Waislamu zilipata hasara. Siku mbili kabla ya hapo, jeshi la Pakistan lilikuwa limeshambulia kwa mabomu maeneo fulani katika miji ya Kabul na Paktika, na kusababisha hasara zake zenyewe.

Soma zaidi...

Janga la Gabes, Mhasiriwa wa Machaguo ya Dola ya Kisasa

Maandamano ya watu wa Gabes kusini mwa Tunisia yanaendelea kwa sababu ya sumu inayotolewa kutoka kwa tata ya kemikali, ambayo imegeuza jiji hilo kuwa eneo lililoathirika kimazingira na kiafya, na kuathiri moja kwa moja afya ya wakaazi wa Gabes na mali asili yake. Saratani na magonjwa ya kupumua yameenea, na suala hilo limefikia hata visa vya kukosa hewa miongoni mwa wanafunzi. Miongo kadhaa ya ahadi za uongo na kupuuzwa kwa makusudi kumeifanya Gabes kuwa ishara ya kutengwa na uchafuzi wa mazingira, kwani utajiri wa phosphate umegeuka kutoka kuwa baraka hadi laana kwa sababu ya sera za serikali ya kisasa, ambayo ilichagua faida ya haraka na maslahi ya makampuni makubwa kwa gharama ya afya ya watu na haki yao ya maisha bora.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi Mirza Ahmadov Miraziz

Kwa huzuni na majonzi makubwa, tunaomboleza kuondokewa na mwana wetu mwengine madhubuti na mchamungu, na hatumtakasi yeyote mbele ya Mwenyezi Mungu. Ndugu yetu Mirza Ahmad Mir Aziz alifariki dunia siku ya Ijumaa, 10 Oktoba 2025, na swala ya janaza iliswaliwa kwa ajili yake jana, Jumamosi. Mir Aziz alizaliwa Tashkent mwaka wa 1970. Alikuwa mmoja wa maelfu ya Waislamu wenye ikhlasi na ujasiri ambao waliitikia wito wa Hizb ut Tahrir kwa watu wa Uzbekistan kufanya kazi ya kuregesha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu.

Soma zaidi...

Mauaji na Njaa ya Watoto wa Gaza Havitakwisha Kupitia Mipango ya Wale Waliohusika na Mauaji ya Halaiki Bali Kupitia Uhamasishaji wa Majeshi ya Waislamu Pekee

Katika kipindi cha miaka 2 iliyopita, watu wa Gaza wamekuwa wakikabiliwa na mashambulizi ya mabomu, mzingiro wa kikatili na jinai za kutisha zaidi za umbile la mauaji la Kiyahudi, ambapo wanawake na watoto wamekuwa wahanga wakuu. 65,000 wameuwawa, wakiwemo zaidi ya watoto 20,000 – sawa na watoto 30 wanaouawa kila siku. Watoto wamepigwa risasi kimakusudi na wavamizi wa Kiyahudi au mashambulizi ya droni barabarani, au hata wanapotafuta chakula kwenye vituo vya misaada ambavyo vimekuwa ‘mitego ya kifo’ kwa wanaokabiliwa na njaa. Kulingana na ‘Save the Children’, watoto waliuawa au kujeruhiwa katika zaidi ya nusu ya mashambulizi mabaya katika maeneo ya usambazaji wa chakula mjini Gaza ndani ya wiki nne baada ya Wakfu wa Kibinadamu wa Gaza kuanza shughuli zake.

Soma zaidi...

Ni lini Tutakomesha Uingiliaji wa Kafiri Magharibi na Mashirika yake ya Kikoloni katika Maisha Yetu, na Kuelekeza Nyuso Zetu Kwa Al-Waahid, Al-Haakim?

Chini ya ufadhili wa shirika la Ufaransa la Promediation, vyama vya kisiasa vya Sudan vilifanya warsha jijini Port Sudan, kama ilivyoripotiwa kwenye tovuti ya Sudan Tribune mnamo tarehe 5 Oktoba 2025: “Warsha inalenga kufafanua vigezo vya mazungumzo ya mustakbali yatakayoongozwa na Sudan, ikiwemo washiriki wake, eneo, na dori ya upatanishi wa kimataifa, kulingana na msemaji wa kambi hiyo Mohammed Zakaria. Viongozi wa muungano huo walisisitiza haja ya muungano wa ndani ulioshikamana. Minni Arko Minnawi, mkuu wa kamati ya kisiasa ya umoja huo, alisema hatua ya pamoja kati ya viongozi wa kiraia na kijeshi ni muhimu kwa ajili ya utulivu.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Chukueni Hatua na Msiache Masuala Yenu Yawe Mikononi mwa Maadui Zenu

Mazungumzo ya awamu ya kwanza ya mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump kusimamisha vita dhidi ya Gaza yalianza mjini Sharm El-Sheikh nchini Misri, kwa kuhudhuriwa na wajumbe wa Marekani Steve Witkoff na Jared Kushner, Waziri Mkuu wa Qatar, na wakuu wa kijasusi wa Uturuki na Misri.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu