Kama Sehemu ya Kampeni ya “Waislamu Dhidi ya Uhalalishaji Mahusiano” Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon Yafanya Msururu wa Ziara
- Imepeperushwa katika Lebanon
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kwa kuzingatia mamlaka ya Lebanon kushiriki katika mazungumzo ya moja kwa moja ambayo hakika yatapelekea katika amani na uhalalishaji mahusiano na umbile nyakuzi na halifu la Kiyahudi, na kama sehemu ya kampeni ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon kuwatembelea wanasiasa, mamufti, wasomi, nyanja ya kisiasa, na watu mashuhuri, wajumbe kutoka Kamati Kuu ya Mawasiliano na kamati za shughuli za kikanda walifanya ziara. Hizi zilianza katika mji wa Sidon kusini mwa Lebanon kwa ziara ya Mbunge Dkt. Osama Saad, Katibu Mkuu wa Shirika Maarufu la Wananasseristi, na ziara ya Mufti wa Sidon na wilaya zake, Sheikh Salim Sousan. Hii ilifuatiwa na ziara katika mji mkuu, Beirut, kwa Naibu Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Kiislamu la Shia, msomi Sheikh Ali Al-Khatib.



