Mauaji ya Kikatili ya Sohag katika eneo la Midford la Mji Mkuu Dhaka, ni Matokeo Yasiyoepukika ya Siasa za Kisekula na za Kiwendawazimu zisizomtambua Mungu
- Imepeperushwa katika Bangladesh
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Katika eneo la Mitford la mji mkongwe wa Dhaka, baadhi ya viongozi wa eneo la Jubo Dal, wakiongozwa na chama kikuu cha kisekula cha kisiasa nchini humu BNP, walimuua kikatili mfanyibiashara wa vyuma vichakavu aitwaye Sohag (39) kwa kumdunga kisu na kumpiga na jiwe kubwa mfululizo kwa kukataa kulipa pesa za ulaghai. Walioshuhudia walisema kwamba wahalifu hao hawakuishia kumuua tu, bali waliendelea kuonyesha unyama kwenye mwili mfu wa Sohag hata baada ya kifo chake kuthibitishwa. Mwili uliojaa damu, ulioganda uliachwa katikati ya barabara na wauaji wakasimama juu ya mwili huo huku wakisherehekea kiwendawazimu.