Jumanne, 07 Shawwal 1445 | 2024/04/16
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Sudan

H.  13 Muharram 1442 Na: HTS 1442 / 05
M.  Jumanne, 01 Septemba 2020

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Serikali ya Mpito na Kundi la Mapinduzi (Jabhat al-Thawrah) Wanaiweka Nchi Kwenye Mashini ya Upasuaji kwa Mara ya Pili

Mnano siku ya Jumatatu 31/08/2020 M; serikali ya mpito ilitia saini huko Juba, mji mkuu wa Sudan Kusini, makubaliano yaliyoitwa makubaliano ya amani na Chama cha Mapinduzi, na jambo maarufu zaidi katika makubaliano haya ni kuyapa uhuru maeneo mawili ya Blue Nile na Kordofan Kusini uhuru, pamoja na kugawanya mamlaka na rasilimali kati yao; Juu ya njia ya serikali ya zamani yenyewe katika kujadiliana na harakati za waasi.

Jambo baya zaidi ambalo limeikumba Sudan kwa miongo kadhaa ni kuinuliwa kwa harakati kadhaa za silaha dhidi ya serikali. Kwa madai ya kutengwa; Jambo ambalo ni la asili ambalo liliathiri maeneo yote ya Sudan, lakini madai ya kutengwa yanapatikana hata katika mji mkuu wa nchi hiyo, kwa sababu tawala hizi zimeuweka mbali Uislamu; Nidhamu ya uchungaji, na kufanya kazi kwa mfumo wa Kirasilimali, na kuutabikisha kwa sura yake mbaya zaidi, kisha baadhi ya harakati hizi kurusha mikononi mwa kafiri Magharibi, kisha kuiagiza kile anachotaka; na kile Magharibi inachotaka, iwe ni Amerika au Ulaya, ni kuipasua Sudan katika vijidola dhaifu na duni ambavyo ni rahisi kumeza na kumeng'enya, na upasuaji huu ulianzia na Sudan Kusini, ambayo ilitenganishwa kwa mandhari ile ile inayoendelea sasa; Ambapo watu wengine wa kusini waliasi na kuchukua silaha dhidi ya serikali, kisha wakawapa uhuru, katika enzi ya Rais Nimeiri, na kisha ilikuwa Naivasha iliyowapa haki ya kujitawala iliyosababisha kujitenga kwa kusini.

Na sisi hawa hapa tunaona serikali ya mpito ikiwasilisha usaliti na kukubali kuyapa maeneo haya mawili ya Kusini mwa Kordofan na Blue Nile uhuru; hivyo basi inaiweka nchi kwa mara ya pili kwenye mashini ya kupasua kwa jina la madai ya amani!!

Sisi katika Hizb ut-Tahrir / Wilayah ya Sudan kama tulivyoonya na kutanabahisha juu ya hatari ya mazungumzo hayo ya khiyana, tunaionya serikali ya mpito juu ya hatma ya kile inachofanya kwa kuyaweka maeneo ya Sudan kwenye mashini za kurarua kwa jina la amani ambayo haiwezi kuja kwa mithili ya makubaliano kama haya, na muumini haumi mara mbili kutoka shimo moja, lakini sisi hawa hapa tunauma tena na tena, wala hatuzingatii matokeo ya makubaliano mabaya kama haya!

Enyi Watu wa Sudan: wekeni mikoni yenu katika mikono ya mashababu wa Hizb ut Tahrir, na Enyi Watu wenye nguvu: ipeni Nusra Hizb ut Tahrir, Dola ya Haki na Uadilifu isimamishwe; Khilafah Rashida kwa Njia ya Utume ambayo itakomesha umwagikaji huu wa damu, ili ihifadhi umoja wa nchi hii, Badala yake, itaunganisha nchi zote za Kiislamu na kuwakata makafiri wote.

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ

"Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuitieni jambo la kukupeni uzima wa milele." [Al-Anfal: 24]

 Ibrahim Uthman (Abu Khalil)

Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir

Katika Wilayah Sudan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Sudan
Address & Website
Tel: 

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu