Jumatatu, 09 Rajab 1447 | 2025/12/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Wakati Dola ya Kibaniani Inapozivua Niqab Kwenye Nyuso za Mabinti wa Kiislamu, Warithi wa Muhammad Bin Qasim Wako Wapi Ndani ya Jeshi la Pakistan?

Mnamo Jumatatu, 15 Disemba 2025, katika sherehe moja, Waziri Mkuu wa jimbo la India la Bihar, Nitish Kumar, aliichana niqab kutoka kwa daktari mmoja Muislamu, Nusrat Parveen. Baada ya kufanya hivyo, alicheka kana kwamba kuichana niqab hiyo kutoka kwa uso wa mwanamke wa Kiislamu ilikuwa ni mzaha. Ilhali, Mayahudi walipomfunua mwanamke mmoja wa Kiislamu na kumdhihaki hali yake, Swahaba aliyekuwepo alimuua Myahudi huyo; na Mayahudi walipomuua shahidi Swahaba huyo baadaye, Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) alizingira kabila lote, akawakamata na kuwafunga wote, na alikuwa akitoa hukumu juu yao, lakini hatimaye, baada ya maombezi, adhabu ndogo ilitolewa: kabila lote lilifukuzwa Madina. Lakini leo hakuna dola ya kulinda heshima ya Dkt. Nusrat Parveen na kumpa Baniani huyu muovu, Nitish Kumar, funzo.

Soma zaidi...

Kuvunjwa Moyo Kupya: Watu wa Gaza Wanakufa kwa Baridi Baada ya Kuachwa Kuteswa na Mauaji ya Halaiki kwa Miaka Miwili!

Maafa yanayoikumba Palestina inayokaliwa kwa mabavu yanaendelea bila kukoma. Tangu kuanguka kwa Khilafah, ambayo mtawala wake aliwahi kutamka, “Palestina ni ardhi iliyonyweshwa kwa damu ya mababu zangu, na iwapo Khilafah itaanguka, mtaichukua bila malipo,” uvamizi wa Waingereza (ulioitwa Mamlaka) uliibadilisha. Na hadi leo, umbile la Kiyahudi linaloikalia kwa mabavu, lililoundwa na Uingereza na kuungwa mkono na nchi za Magharibi kwa mali yake yote, vifaa, ujuzi na uwezo wake wote, linaendelea kuwaua watu wa ardhi iliyobarikiwa, likiwafanyia ukatili vijana na wazee, na kuwatishia wafungwa kuwaua na kuwanyonga, huku ulimwengu ukitazama. Limeizingira Gaza kwa miaka mingi, likiishambulia bila kuchoka kwa ukatili usiofikirika, na kusababisha mauaji ya zaidi ya watu elfu sabiini. Na ulimwengu wa Kiislamu, pamoja na majeshi yake na wanazuoni, hutazama na kuona kama vipofu wanavyofanya, na husikia vilio vya wanawake waliofiwa kama viziwi wanavyosikia!

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi wa Habari

Tunafurahi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, kuwaalika wataalamu wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria mkutano na waandishi wa habari ambapo Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan atazungumza chini ya kichwa: “Usimamizi wa Amerika wa Mgogoro wa Sudan: Kuongeza Majeraha na Kugawanya Nchi”

Soma zaidi...

Unyanyasaji wa Kimpangilio wa Kijinsia Dhidi ya Wanawake wa Sudan Hautoi Jibu lolote kwa Kukosekana kwa Dola Inayojali Heshima ya Mwanamke Mwislamu

Mnamo Alhamisi tarehe 11 Disemba, shirika, ‘The Strategic Initiative for Women in the Horn of  Africa’, liliripoti kuwa limerekodi karibu matukio 1300 ya unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake katika majimbo 14 nchini Sudan tangu vita vianze nchini humo mnamo Aprili 2023, huku Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vikilaumiwa kwa 87% ya visa hivi. Lilielezea unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake ukitumika kama silaha ya kimfumo katika mzozo huo, likisema “umeenea, unarudiwa rudiwa, unakusudiwa na mara nyingi unalenga”. Ubakaji ulichangia robo tatu ya matukio yaliyorekodiwa, huku visa 225 vikihusisha watoto, baadhi wakiwa na umri wa miaka 4. Matukio yalitokea majumbani, maeneo ya umma na pia yalijumuisha kizuizini cha muda mrefu cha wanawake ambao waliteswa, kubakwa na genge na ndoa za kulazimishwa. Mnamo Jumapili tarehe 7 Disemba, vikundi vya matibabu vya Sudan viliripoti kwamba watoto na wanawake kadhaa walinyanyaswa kingono na kubakwa walipokuwa wakikimbia kukamatwa kwa El Fasher huko Darfur na RSF Oktoba hii.

Soma zaidi...

Kilio cha Haraka cha Msaada, Enyi Ummah wa Kiislamu!

Wanawake na watoto wa Gaza wanalilia msaada... wanawake na watoto wa Sudan wanalalamika... wanawake na watoto wa Uyghur huko Turkestan Mashariki wanateseka na kupiga kelele... Wanawake wa Kiislamu na watoto wao kila mahali wanapaza kilio baada ya kilio, wakiita: Je, kuna mtu yeyote wa kusaidia? Je, kuna mtu yeyote wa kuitikia wito? Je, kuna mtu yeyote wa kujibu?!

Soma zaidi...

Jeshi la Bangladesh Lazima Likatae Kuwa Rafiki wa Wakoloni kwa Jina la kile kinachoitwa Ulinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa na Kurudisha Hatima Yake kama Walinzi wa Ummah

Jeshi la Bangladesh linathibitisha shambulizi baya la droni kwenye kambi ya Umoja wa Mataifa katika eneo la Abyei nchini Sudan mnamo 13 Disemba 2025. Shambulizi hili liliwaua walinda amani sita wa Bangladesh na kuwajeruhi wengine wanane. Wakati huu wa kuhuzunisha moyo hauhitaji maombolezo tu, bali pia tathmini mpya muhimu ya misheni ambayo kwayo walitoa maisha yao.

Soma zaidi...

Je, Vikosi vya Kiislamu vya Jeshi la Pakistan Sasa, Chini ya Uongozi wa Jenerali wa Marekani, Vitawalinda Mayahudi na Kuupokonya Silaha Upinzani wa Palestina?

Gazeti la Dawn liliripoti kwenye tovuti yake mnamo tarehe 13 Disemba, 2025 kwamba majeshi ya Waislamu huenda yakatumwa kuanzia mwezi ujao kwa ajili ya “Kikosi cha Kimataifa cha kuleta Utulivu” mjini Gaza. Hapo awali, mtawala kibaraka wa Marekani Shehbaz Sharif alikuwa tayari ametoa idhini “ya kikanuni” kwa kutumwa kwa vikosi vya Pakistan huko Gaza. Hata hivyo, wakiogopa upinzani mkali wa umma, watawala wa Waislamu mmoja baada ya mwengine wamekuwa wakionyesha kutokuwa na msaada kwao mbele ya Amerika. Hivyo sasa shetani Trump na wafuasi wake, watawala wa Waislamu, wanaunda njama mpya za kutumia vikosi vyetu vya Waislamu vya mujahid kuwalinda Mayahudi na kuwanyang'anya silaha Hamas na vikosi vyengine vya upinzani vya Palestina.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wamzuru Sheikh wa Twarika ya Sammaniyah katika Mji wa Wad Madani

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ulitembelea Sheikh wa Twarika ya Sammaniyah katika Jimbo la Al-Jazirah jana, Jumamosi, 13/12/2025. Ujumbe huo uliongozwa na Ustadh Mahdi Muhajir, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, akifuatana na Ustadh Abdulaziz Ibrahim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na mhandisi Walid Kamil.

Soma zaidi...

Mashirika ya Mamlaka ya Palestina na Majambazi Wao Yamkamata Mwanafunzi Saif Abu Al-Hawa

Mamlaka ya Palestina (PA), ambayo ni tiifu kwa Mayahudi, ilimkamata mwanafunzi Saif Abu al-Hawa alipokuwa akiondoka Chuo Kikuu cha Bethlehem mnamo Jumanne, 9 Disemba 2025. Kwa kutumia majambazi wasaliti na kisha kikosi kutoka kwa vyombo vya usalama vya PA, katika tukio linaloakisi mbinu za ujambazi na vitisho vya PA dhidi ya watu wa Palestina, hawazuiwi na Dini wala sheria, wala hata utakatifu wa chuo kikuu ambacho Saif alitoka. Kisha alifikishwa mbele ya mahakama mnamo Alhamisi, ambapo jaji aliongeza kifungo chake kwa siku kumi na tano, licha ya kwamba hakufanya uhalifu wowote. Kosa lake pekee lilikuwa kutaja Hukm Shari’ kwamba Waislamu hawaruhusiwi kushiriki katika sherehe za sikukuu za Kikristo!

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu