Jumanne, 19 Rabi' al-thani 1446 | 2024/10/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Uholanzi: Matembezi mjini Amsterdam “Miaka 75, na Mwaka Mmoja wa Mauaji ya Halaiki mjini Gaza!”

Hizb ut Tahrir / Uholanzi iliandaa matembezi katika mji mkuu wa Uholanzi, Amsterdam, kwa mnasaba wa kupita mwaka mmoja kamili wa vita vya mauaji ya Halaiki dhidi ya Waislamu wa mji wa Gaza Hashem, kunusuru na kuiombea nusra na Izza Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina) na Gaza.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Indonesia: Amali kubwa kwa Mnasaba wa Kupita Mwaka Mmoja wa Mauaji ya Halaiki mjini Gaza!

Hizb ut Tahrir / Indonesia iliandaa amali kubwa katika mji mkuu wa Indonesia, Jakarta, na katika mji mkubwa wa pili nchini Indonesia wa Surabaya, ambapo maelfu ya Waislamu walikusanyika na kutaka kuhamasishwa kwa majeshi ya Waislamu ili kuwanusuru Waislamu katika Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina) na kuukomboa Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa na Palestina yote inayokaliwa kwa mabavu.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Ukombozi: “Kwa Khilafah, Majeshi yatasonga kuikomboa Palestina!”

Baada ya swala ya Ijumaa, matembezi ya hamsini na tatu yalifanyika katika mji mkuu, Tunis, mbele ya Msikiti wa Al-Fatah, matembezi makubwa yaliyoitishwa na Hizb ut-Tahrir / Wilayah Tunisia, kwa watu wa Al-Khadra, na yenye kichwa “Kwa Khilafah, Majeshi yatasonga kuikomboa Palestina.”

Soma zaidi...

Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir: Kongamano la Kimataifa “Mwaka Mmoja Umepita Enyi Majeshi!”

Mwaka mmoja umepita tangu Kimbunga cha Gaza, ambacho kimetikisa misingi ya hadhara ya Magharibi na kuponda ponda simulizi ya jeshi lisiloweza kushindwa. Mwaka mmoja wa uchinjaji na mauaji ya halaiki ya watu wa Gaza yametekelezwa na nchi za Magharibi zenye chuki na zingali zinaendelea kutekeleza kwa kulitumia umbile nyakuzi. Mwaka mzima wa kula njama na kufanya biashara ya umwagaji damu ambayo watawala wa Waislamu wamegeuka kuwa waovu, na kuwaongezea fedheha.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Amali Kubwa “Mwaka Mzima umepita, na Nchi 57 Hazijachukua Hatua Yoyote!”

Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Uturuki iliandaa baada ya swala ya Ijumaa matembezi na visimamo vikubwa katika miji 16 kote nchini Uturuki, kama ambavyo Hizb pia iliandaa makongamano, vikao na mikutano mikubwa chini ya kichwa: “Mwaka Mzima umepita, na Nchi 57 Hazijachukua Hatua Yoyote!”

Soma zaidi...

Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir: Kitengo cha Wanawake “Kongamano la Kimataifa la Wanawake: Ukombozi wa Palestina... Changamoto na Bishara Njema”

Mwaka mzima umepita tangu kuanza kwa Kimbunga cha Al-Aqsa na vita vikali vilivyofuata huko Gaza. Tangu tarehe 7 Oktoba mwaka jana, watu wa Gaza wamevumilia mitihani mikubwa, wakiishi katika machungu, mateso, na majanga yasiyohesabika.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Ukombozi: “Enyi Waislamu, Je, Mtawaacha Watu wa Palestina peke yao na Hali Umma una Majeshi yenye Nguvu?”

Baada ya Swala ya Ijumaa, katika mji mkuu, Tunis, yalifanyika matembezi ya hamsini yaliyoitishwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia, kwa watu wa Zaytouna, kwa ajili ya kuwanusuru watu wa Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina) na Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa ulio mateka, na kichwa chake kilikuwa, “Enyi Waislamu, je, mtawaacha watu wa Palestina peke yao na hali Umma una majeshi yenye Nguvu?!”

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Mkutano na Waandishi wa Habari: “Uchaguzi ni njia ya Kuendeleza Mfumo wa Kisekula ambao ni Wajib Ubadilishwe kwa Kusimamisha Khilafah”

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia ilifanya mkutano na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano huko Ariana katika mji mkuu, Tunis, saa 10:30 asubuhi kwa saa za eneo, wenye kichwa “Uchaguzi ni njia ya Kuendeleza Mfumo wa Kisekula ambao ni Wajib Ubadilishwe kwa Kusimamisha Khilafah”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu