Alhamisi, 01 Muharram 1447 | 2025/06/26
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Majibu ya Aibu ya Tawala katika Nchi za Waislamu kwa Uvamizi wa Umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran!

Yeyote anayetazama miitikio ya tawala zilizopo katika ardhi za Waislamu kwa mashambulizi ya umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran atahisi huzuni kubwa na masikitiko kwa hali ya sasa ya Waislamu. Wengine wamelaani na kushutumu pekee; wengine wameonyesha hofu ya machafuko katika eneo hilo kutokana na mashambulizi haya. Baadhi walieleza kuwa ni ongezeko la hatari; wengine walielezea wasiwasi wao juu ya athari zake kwa kadhia ya Palestina. Wengine hata walitangaza kuwa tayari kufanya upatanishi kati ya Iran na umbile la Kiyahudi. Walio bora zaidi walionyesha nia ya kuiunga mkono Iran katika majukwaa ya kimataifa, huku baadhi ya nchi hizo hizo zikifungua anga zao kwa ndege za umbile la Kiyahudi kuruka juu, kuipiga Iran kwa mabomu, kuua na kuharibu, na kisha kuregea bila hata risasi moja kufyatuliwa kwao! Wengine walinasa makombora na droni za Iran zilizolenga kushambulia umbile la Kiyahudi, na hivyo kuwaepusha na kupigwa!

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Adui Yenu Anaujua Uzito Wenu Vizuri Kuliko Mnavyoujua nyinyi, na Anakuogopeni Nyinyi na Anakuchukulieni Kwa Umakini Mara Elfu!

Siku baada ya siku, matukio na misimamo inafichua ushahidi mwingi wa dola za kikoloni za kikafiri kuwaogopa Waislamu, ikiwemo umbile vamizi la Kiyahudi. Pia inaonyesha kwamba wanapoamiliana na Waislamu, wanawachukulia kwa uzito mara elfu moja. Baada ya zaidi ya karne moja, baada ya kuvunjwa kwa Khilafah, kugawanyika kwa Waislamu na kuwa maumbo dhaifu, nyenyekevu, ikifuatwa na udanganyifu na uvamizi wa kifikra, kujitenga kwa Waislamu na imani yao, kuporwa mali ya Waislamu, kupanuka kwa ushawishi wa wakoloni hao makafiri katika ardhi zao, na kudhoofika kwao na kudhalilika, baadhi wanasema: Waislamu kamwe hawatainuka tena, na baada ya haya yote, tunasikia na kuona kauli kutoka kwa viongozi wa Magharibi na viongozi wa umbile vamizi la Kiyahudi, ambazo zinaonyesha hofu yao ya Uislamu na hofu iliyojaa nyoyoni mwao kutoka kwa Waislamu katika hali hii.

Soma zaidi...

Pongezi kwa Idd Al-Adha Iliyobarikiwa 1446 H

Hizb ut Tahrir inatoa pongezi na baraka nyingi zaidi kwa Umma wetu mpendwa wa Kiislamu, wenye subira na wenye kukubali malipo licha ya maafa na majanga yote unaopitia, maafa na majanga ambayo ni mzigo mzito hata kwa kundi lililo imara zaidi la wanadamu, hususan watu wetu wenye subira mjini Gaza na katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, katika Sikukuu ya Idd ul-Adha. Tunamuomba Mwenyezi Mungu azijaalie siku za Idd hii kuwa ni utulivu katika nyoyo zao na wanyanyuliwe daraja mbele ya Mola wa walimwengu wote.

Soma zaidi...

Ni Nani atakayewatetea Wanawake wa Sudan na Darfur?

Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (Médecins Sans Frontières) limeonya kuwa wanawake na wasichana katika jimbo la Darfur nchini Sudan wako katika hatari ya karibu kila mara ya unyanyasaji wa kijinsia. Mizani halisi ya mgogoro huu inasalia kuwa vigumu kubainisha, kwani huduma bado ni chache na watu wanakabiliwa na vikwazo katika kutafuta matibabu au kuzungumza kuhusu masaibu yao. Hata hivyo, manusura wote waliozungumza na timu za MSF huko Darfur na kuvuka mpaka nchini Chad walisimulia hadithi za kutisha za ghasia za kikatili na ubakaji. Huku wanaume na wavulana pia wakiwa hatarini, kiwango cha mateso kinapita maelezo.

Soma zaidi...

Tangazo la Matokeo ya Kuutafuta Mwezi Muandamo wa Shawwal 1446 H Pongezi kwa Idd Al-Fitr Iliyobarikiwa

Ummah umepitia mateso ya kubaki chini ya nira ya tawala za vibaraka. Umeshuhudia kwa macho yake wenyewe watawala wakifuja mali zake kwa makafiri, wakoloni wa Magharibi, kuzitelekeza kwao na sababu zake, kuzuia kwao majeshi kusonga ili kuinusuru Palestina kutoka kwenye makucha ya Mayahudi wahalifu, uingiliaji wa wazi wa Magharibi katika dini yake na uadilifu wake, na jaribio la kuulazimisha kulishuhudia  umbile la Kiyahudi, na kuuacha na chaguo kati ya uhalalalishaji mahusiano au kifo. Mandhari na matukio haya yote yameufanya utambue kwamba bila ya utawala wa Uislamu, utabakia kukoloniwa, kulengwa, na kudhalilishwa. Kukinaika kwake kwa haja ya dola ya Khilafah kumeimarishwa, na kwa hakika, Khilafah imekuwa ni kiu yake.

Soma zaidi...

Marekani Yatoa Tahadhari kuhusu Alfajiri ya Khilafah Rashida kwa Njia ya Utume

Kila wakati Umma unapopiga hatua kuelekea ukombozi kutoka kwenye nira ya ukoloni unaolemea sana kifua chake, na kutaka kujikomboa kutoka kwenye himaya ya Magharibi, dola za Magharibi hutoa tahadhari, zikihofia kwamba juhudi za waumini wa kweli wa Ummah zitafikia kilele kwa kuasisiwa Khilafah Rashida, kama ilivyotolewa bishara njema na Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw). Kwa hivyo, Amerika na muungano wake wa Makruseda walijipanga, baada ya kukimbia kwa dhalimu wa Syria, Bashar al-Assad, na kuingia kwa wanamapinduzi jijini Damascus. Walituma mjumbe baada ya mjumbe, wakuu pamoja na wa vyeo vya chini, wanaowakilisha serikali zao, ili kudhibiti tukio ambalo Amerika na muungano wake wa Makruseda walikadiria kuwa muhimu. Endapo maji yatazidi unga, matokeo hayatakuwa mazuri kwa makafiri.

Soma zaidi...

Marekani Yaanzisha Mashambulizi ya Kikatili kwa Yemen Huku Majeshi Yetu Yakitulia tuli, Yakishindwa Kuinusuru Yemen na Gaza!

Kwa siku nyingi sasa, Amerika imekuwa ikianzisha mashambulizi ya kikatili kwa watu wetu nchini Yemen, kwa kutumia kile Rais wa Marekani Trump alichoeleza kuwa "nguvu kuu mbaya." Alikuwa amewatisha hapo awali, akichapisha, “JAHANAM ITANYESHA JUU YENU KWA NAMNA AMBAYO KWAME HAMJAWAHI KUONA KABLA!!”

Soma zaidi...

Mkutano wa Cairo, kama Watangulizi wake, Unadhihirisha Usaliti wa Watawala wa Kiarabu na Kuitelekeza kwao Gaza na Watu wake!

Gaza haihitaji mipango zaidi inayoiweka chini ya ukaliwaji kimabavu na udhibiti wa Mayahudi. Kinachohitaji kwa hakika ni hatua ya dhati kutoka kwa Ummah na majeshi yake ili kuinusuru na kuikomboa kutokana na mitego ya Mayahudi na Marekani. Bila haya, tutaendelea kuwahesabu mashahidi na majeruhi, tukishuhudia unajisi na kiburi cha Mayahudi—wakati wote huku watawala wa Waislamu wakiendelea kuusaliti Umma na utumwa wao kwa Amerika.

Soma zaidi...

Watawala wa India Wanatumia Sheria ya (Kuzuia) Shughuli zisizo halali ya 1967 kupiga Vita Uislamu na Waislamu, wakimwemo Mashababu wa Hizb ut Tahrir

Katika kampeni yake inayoendelea dhidi ya Hizb ut Tahrir, Shirika la Kitaifa la Upelelezi la India lilimkamata Bava Bahrudeenand Kabeer Ahmed Aliyar mnamo 3 Februari 2025, baada ya miezi kadhaa ya unyanyasaji. Vyombo vya habari vya India viliripoti kwamba "walikula njama na wengine kueneza fikra ya Hizb ut Tahrir huko Tamil Nadu, ambalo ni shirika lililopigwa marufuku." Kisha mamlaka zikanasibisha kesi yao na kesi inayoendelea ya Dkt. Hameed Hussain chini ya Sheria ya (Kuzuia) Shughuli Zisizo Halali (UAPA) ya 1967!

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Msiikubali Marekani kama Mpatanishi, Kwa Maana sio tu kuwa ina Upendeleo; bali, ni Sehemu ya Mzozo!

Mnamo Januari 15, makubaliano yalifikiwa kusitisha vita dhidi ya Gaza kati ya umbile la Kiyahudi na harakati ya Hamas. Makubaliano hayo yalianza kutekelezwa mnamo Januari 19 mwezi huo huo na yalisimamiwa na nchi tatu: Amerika, Misri na Qatar. Tangu wakati huo hadi leo, umbile la Kiyahudi limetekeleza ukiukaji mwingi wa makubaliano haya na limeshindwa kutimiza wajibu wake mwingi, kama ilivyo kawaida kwa Mayahudi katika khiyana na uvunjaji ahadi na makubaliano.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu