Enyi Waislamu: Je, bado mna matumaini kwa Watawala wenu Ruwaibidha?!
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Umbile la Kiyahudi bado linatekeleza uhalifu wake dhidi ya watu wa Gaza, hivyo makumi ya mashahidi huongezeka kutokana nao kila siku. Pia bado linapiga mzingiro wake juu ya Gaza, hivyo watu wake wanakufa kwa njaa, kwa kuwa hawana chakula, vinywaji, dawa, au makao, licha ya jitihada fulani za kupeleka misaada kwao kwa uoga! Lakini mamia ya maelfu hawapati tonge ambalo kwalo wanaweza kuzuia njaa zao au kunyamazisha njaa ya watoto wao, kwa hiyo wamekuwa wanakufa kwa njaa mbele yao na mbele ya macho ya ulimwengu wote bila msaidizi au mwenye kuwanusuru.