Kauli za Netanyahu kuhusu "Israel Kubwa" ni Tangazo la Vita ambalo linafuta Mikataba, na, kwa sababu hiyo, Majeshi Yanasonge, na Jambo jengine lolote lisokuwa hilo ni Usaliti
- Imepeperushwa katika Jordan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Huyu hapa mhalifu wa kivita Netanyahu anatangaza waziwazi na bila kufasiriwa kwa watawala waoga wa Kiarabu na wasemaji wao, akisema katika mahojiano na chaneli ya Kiebrania i24: “Mimi niko kwenye misheni ya vizazi na kwa jukumu la kihistoria na la kiroho, ninaamini kwa dhati ruwaza ya Israel Kubwa, ambayo ni pamoja na Palestina ya kihistoria na sehemu za Jordan na Misri.” Mhalifu Smotrich alikuwa amemtangulia kwa kauli zile zile na kunyakua sehemu za nchi za Kiarabu zinazoizunguka Palestina, ikiwemo Jordan. Katika muktadha huo huo, adui namba moja wa Uislamu na Waislamu, Rais Trump wa Marekani, alimpa idhini ya upanuzi wake akisema, “Israel ni sehemu ndogo sana ikilinganishwa na ukubwa wa ardhi hizo, na najiuliza ikiwa inaweza kupata ardhi zaidi kwa sababu kweli ni ndogo sana.”