Jumatatu, 23 Shawwal 1446 | 2025/04/21
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Je, Mafanikio kwa Waislamu yanaweza Kupatikana kupitia Siasa za Kidemokrasia?

Kutokana na mauaji makubwa ya halaiki yanayotokea Gaza na dori ya Marekani katika kusaidia na kuunga mkono yaendelee, kumekuwa na mijadala mingi miongoni mwa Waislamu kuhusu jinsi ya kujihusisha zaidi kisiasa na jinsi jamii ya Kiislamu inavyoweza kuwa mstari wa mbele katika kuunda siasa za Marekani ili kubadilisha dunia kuwa bora. Ndani ya mijadala hii, mengi yanasemwa kuhusu kujishughulisha na uraia, kujiunga na kuunga mkono wagombea mahususi wa kisiasa, kunyima kura zao kama aina ya adhabu, na hatimaye kupata Waislamu zaidi, au "washirika" kwenye nyadhifa katika ngazi za dola na majimbo. Kuna gumzo hata miongoni mwa kina dada wakidai kwa furaha kwamba wanajaribu kumlea kijana au binti yao kuwa Rais wa kwanza wa Marekani Muislamu. Haya yanawekwa kama mafanikio sio tu kwa Waislamu wa Amerika, lakini Waislamu kote ulimwenguni. Huu unawekwa kama mpango wa mafanikio licha ya ukweli kwamba vyama vyote vya kisiasa, iwe vya rangi ya samawati, nyekundu, au kijani vinaunga mkono umbile la Kizayuni, au dola zengine zenye kufanya mauaji ya halaiki mithili ya China na India.

Soma zaidi...

Umbile la Kiyahudi Linaweka Kielelezo Hatari - lakini kwani ni wa Kwanza Kufanya Hivyo?

Matendo ya umbile la Kiyahudi yanatia wasiwasi wachambuzi kote ulimwenguni ambao wanashangaa kutojali kwao waziwazi sheria ya kimataifa kunamaanisha nini kwa mustakabali wa maadili yote ambayo wanayaenzi mno. Sababu ya hii ni kwa sababu ya umuhimu ambao ‘kielelezo’ kinashikilia katika sheria ya Kimagharibi. Inastahili kusaidia kuhakikisha kuwa kuna uthabiti, kutegemewa, na kutabirika katika maamuzi ya mahakama ili kuongeza imani katika mfumo wa mahakama.

Soma zaidi...

Mkutano wa SCO jijini Islamabad: Siasa za Jiografia ndani ya Kivuli cha Uhasimu wa Marekani na China

Chini ya ulinzi mkali jijini Islamabad, Mkutano wa 23 wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai (SCO) ulianza kwa kishindo cha kawaida. Mkutano huo uliohudhuriwa na dola zenye nguvu kama China, Urusi, India, Pakistan, Iran na baadhi ya jamhuri za Asia ya Kati, ulimalizika kwa kutiwa saini hati nane, zinazohusu bajeti ya shirika hilo, shughuli za sekretarieti ya SCO, na juhudi za kukabiliana na ugaidi katika kanda. Jambo kuu lililoangaziwa lilikuwa ni kuidhinishwa kwa China kama Mwenyekiti kwa kipindi cha 2024-2025.

Soma zaidi...

Wakenya Amkeni

Kenya, shamba la kikoloni, kwa mara nyingine imo katika mchafuko na mtikisiko kwa kuwa mchezo wa bahati nasibu wa kidemokrasia umezunguka nyuzi 360! Walioko madarakani na walioko barabarani wakiandamana wanalaumiana, huku madai yakielekezwa kwa Mswada wa  Kifedha wa 2024 ulioandaliwa kwa maelekezo ya Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) (Business Daily, 28 Juni 2024)! Mswada huo unapendekeza mikakati ya kuzidisha ukusanyaji wa ushuru ambao unatajwa kuwa ni wenye kukandamiza na kuwadidimiza  raia katika umasikini zaidi!

Soma zaidi...

Hatuwezi Kuishi bila Mfumo wa Sasa wa Ulimwengu

Imani kwamba hatuwezi kuishi bila mfumo wa sasa wa ulimwengu labda ndio kikwazo kikubwa kwa usalama wa watu wa Palestina. Iwe kwa kujua, au kutojua, imani hii inaonekana kushikiliwa na watu kote ulimwenguni huku wakiendelea kujaribu kutumia njia za kidemokrasia kuwasaidia watu wa Palestina, licha ya ukweli kwamba wamewafelisha watu kote ulimwenguni.

Soma zaidi...

Barakoa Zimepomoka: Miaka 76 ya Ukaliaji Kimabavu wa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina

Palestina haitakombolewa kwa kujifunza kuhusu historia yake. Kususia, kutengwa na vikwazo havitaikomboa Palestina. Palestina haitakombolewa kwa msaada wa chakula. Palestina itakombolewa wakati wana shupavu wa Umma katika majeshi ya Waislamu watakapowaasi watawala wasaliti, wakavunja minyororo yao na kuandamana kuelekea Al Quds.

Soma zaidi...

Kuporomoka kwa Lazima Kulikokaribia

Mfalme Abdullah II wa Jordan hivi majuzi alitembelea Ikulu ya White House kupokea maelekezo kuhusu dori yake katika mauaji ya halaiki yanayoendelea Gaza. Biden alikuwa makini kuushirikisha utawala wa Jordan katika mipango yake ya kusuluhisha usitishaji vita kati ya umbile la Kizayuni na Hamas.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu