Jumamosi, 23 Dhu al-Hijjah 1445 | 2024/06/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Marufuku ya Hijab ya Ubelgiji: Kutopendelea upande wowote kama Haki mpya ya Kimungu (Droit Divin)

Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu (ECHR) imeidhinisha marufuku ya Ubelgiji ya kuvaa hijab shuleni, uamuzi ambao umezusha mijadala kuhusu uhuru wa kidini na usekula barani Ulaya. Mahakama ilipata kwamba marufuku hiyo, iliyokusudiwa kuhakikisha ‘kutopendelea upande wowote’ katika elimu ya umma, haikiuki Mkataba wa Ulaya wa Haki za Kibinadamu. Kesi hiyo ilianzishwa na mwanafunzi mmoja Muislamu ambaye alidai kuwa sera hiyo inakiuka haki zake za uhuru wa dini na elimu. Hata hivyo, ECHR iliamua kwamba marufuku hiyo ilihalalishwa na haja ya kudumisha ‘kutopendelea upande wowote,’ kama ilivyotarajiwa.

Soma zaidi...

Zama za Mitandao ya Kijamii: Ufichuaji wa Uongo

Kuibuka kwa mitandao ya kijamii, watu wamejikuta wakiweza kuunganika na walioko maeneo mengine ya dunia. Hili liliyapa faida makampuni na serikali hadi ilipotumika dhidi yao. Wakati mauwaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina yalipoanza, watu wa Gaza waliweza kuunganika kwenye majukwaa kama ya TikTok na kuchapisha picha na video juu ya hali ya sasa.

Soma zaidi...

Katika Historia nzima ya Kijeshi ya Kiislamu, Makamanda wa Kijeshi wa Kiislamu Waligeuza Mawimbi ya Vita katika Hali Mbaya. Wako wapi Warithi wa Waheshimiwa wa Leo?

Mtume wetu (saw) ndiye kielelezo pekee kwa maafisa wetu wa kijeshi katika kubadili wimbi la vita. Pindi idadi kubwa ya Waislamu ilipozidiwa na shambulizi la kushtukiza la adui katika Vita vya Hunain, Waislamu waliangukia chini ya shambulizi hilo katika wakati dhaifu na wakavunja muundo. Wimbi la vita lilibadilika kwa muda mfupi na kushindwa kulianza kuonekana.

Soma zaidi...

Mauaji ya Halaiki ya Kimya nchini Congo: Kimya cha Magharibi na Usaidizi kwa Jina la Faida

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ni nyumbani kwa usambazaji mkubwa zaidi wa cobalt, chuma muhimu kinachotumika katika utengenezaji wa betri za lithiam-ion kwa ajili ya simu, tablets na magari ya umeme. Mnamo 2022, akiba ya cobalt ya Congo ilikadiriwa kuwa karibu tani milioni nne za metric, ambazo ziko mashariki mwa nchi, huku akiba ya kimataifa ikiwa ni tani milioni 8.3.

Soma zaidi...

Unafiki wa Ulimwengu wa Kimagharibi: Uamuzi wa ICJ juu ya 'Israel' na Madai ya Uhusiano wa UNRWA na Hamas

Uwanja wa kimataifa mara nyingi hushuhudia dhihirisho la unafiki, hasa linapokuja suala la hatua za dola za Magharibi katika kushughulikia mizozo katika Ulimwengu wa Kiislamu. Matukio mawili ya hivi majuzi, kwa mara nyengine tena, yameleta jambo hili katika mwelekeo mkali: uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kuhusu 'Israel' ambao ulianzishwa na Afrika Kusini mnamo Disemba 29, 2023, na madai yasiyo na msingi yaliyotolewa na 'Israel' kuhusu UNRWA (Shirika la Umoja wa Mataifa la Usaidizi na Kazi kwa Wakimbizi wa Palestina)  kuwa na mafungamano na Hamas.

Soma zaidi...

Kauli Mbiu Tupu na Miito ya Faragha

Wakati wa simu ya faragha kati ya Benjamin Netanyahu na Joe Biden, Netanyahu alisisitiza maoni yake ya awali kuhusu kukataa wazo la kuunda dola ya Palestina. Netanyahu amesema hivi karibuni, “Sitalegeza msimamo juu ya udhibiti kamili wa usalama wa 'Israel' kwenye eneo lote la magharibi mwa Mto Jordan - na hili linaenda kinyume na dola ya Palestina.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu