Hotuba ya Rais Erdoğan ya Umoja wa Mataifa: Maneno Yaso Vitendo
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Rais Recep Tayyip Erdoğan, katika hotuba yake kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, alielezea kile kinachotokea Gaza kama “mauaji ya halaiki,” alisisitiza kuwa Israel inaua watoto kila siku, na kutoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua. Akisambaza picha kutoka Gaza, Rais Erdoğan alisema: “Hakuna vita mjini Gaza ... Huu ni uvamizi, uhamishaji, ufukuzaji, mauaji ya halaiki na uharibifu wa maisha.”