Ijumaa, 08 Jumada al-thani 1447 | 2025/11/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Enyi Waislamu: Maisha Yenu Yanawezaje Kuwa Mazuri Wakati Wanawake Walio Huru Wako Katika Magereza ya Mayahudi, Wakiteswa na Heshima Zao Zikivunjwa?!

Kituo cha Haki za Kibinadamu cha Palestina kilifichua, kulingana na ushuhuda mpya uliokusanywa na mawakili na watafiti wa kituo hicho kutoka kwa wafungwa kadhaa walioachiliwa huru kutoka Ukanda wa Gaza kutoka magereza na vituo vya uzuizi vya umbile la Kiyahudi, utaratibu na mpangilio wa mateso ya kingono, ikiwemo ubakaji, kuvua nguo, kulazimishwa kurekodi filamu, na unyanyasaji wa kingono kwa kutumia zana na mbwa, pamoja na udhalilishaji wa kisaikolojia wa makusudi unaolenga kuponda utu wa binadamu na kufuta kabisa kitambulisho cha mtu binafsi.

Soma zaidi...

Uingereza, kupitia Wafuasi wake na Mabwege wake, Imarati na Serikali ya Al-Alimi, Yamezea Mate Aden na Bahari Nyekundu, Lakini Je, Kuna Mtu Yeyote Aliye Tayari Kuifukuza?

Vyombo vya habari ndani na nje ya Yemen vilisambaza, mnamo Jumanne, 18/11/2025, habari za kuwasili kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza anayeshughulikia Masuala ya Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, Hamish Falconer, mjini Aden; ambapo alikutana na Rashad Al-Alimi, Mwenyekiti wa Baraza la Rais lenye wanachama wanane, na waziri huyo wa Uingereza pia alikutana na Waziri Mkuu Salem bin Buraik na Waziri wa Mambo ya Nje Dkt. Shaya Zindani, na mawaziri kadhaa, na Mwewe huyo aliandamana na Balozi wa Uingereza mjini Aden, Abda Sharif.

Soma zaidi...

Kwa Kuongezeka kwa Ajali za Barabarani, Pindi Uchungaji unapokuwa Haupo na Kubadilishwa na Kulaumu na Kurushiana Lawama!

Mnamo Jumatano, 5 Novemba 2025, ajali mbaya ya barabarani ilitokea katika Barabara ya Al-Arqoub katika wilaya ya Shuqra, jimbo la Abyan, kusini mwa Yemen, ambayo ilisababisha kuchomeka kwa basi la usafiri wa umma lililokuwa njiani kuelekea Aden, likitoka mji wa Jeddah, mali ya Kampuni ya Saqr Al-Hijaz, na lililokuwa limebeba abiria 42.

Soma zaidi...

Amerika, Kutafuta Kuiondoa Darfur, Yaibua Suala la Abyei na Kutishia na Kuonya!

Baada ya kutenganishwa kwa Sudan Kusini na kaskazini mwaka wa 2011, eneo la Abyei liliachwa na utata na kutokuwa la upande wowote — Kusini au Kaskazini — hakukutatuliwa, ilhali kura ya maoni ilitakiwa kufanyika Abyei mwaka wa 2011, sambamba na kura ya maoni ya Sudan Kusini, ili kubaini uhusiano wa eneo hilo na Kaskazini au Kusini, lakini kura ya maoni haikufanyika kwa sababu ya mzozo wa dola hizo mbili kuhusu nani ana haki ya kupiga kura katika kura ya maoni! Eneo hilo linakaliwa na makabila ambayo ni ya Kusini, yaani kabila la Dinka Ngok, na mengine ambayo ni ya Kaskazini, yaani kabila la Misseriya, na bila shaka Wadinka hawatakubali kutenganishwa na mazingira yao ya kikabila ili kuwa na dola ya Kaskazini kwa sababu wangekuwa kiungo dhaifu zaidi katika Dola ya Sudan, na vivyo hivyo Wamisseriya hawatakubali kutenganishwa na mazingira yao ya kikabila ili kuwa na dola ya Kusini kwa sababu wao pia wangekuwa kiungo dhaifu zaidi katika dola hiyo.

Soma zaidi...

Je, Kukamatwa kwa El Fasher Ndio Mwisho wa Mpango, Au Bado Kuna Mishale Zaidi Yenye Sumu Kwenye Ala?

Sudan imeshuhudia mabadiliko makubwa katika vita vyake, ambavyo vimekuwa vikiendelea kwa zaidi ya miaka miwili, huku Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vikichukua udhibiti wa El Fasher, ngome ya mwisho ya jeshi la Sudan katika eneo la Darfur magharibi mwa Sudan. Hii imeimarisha udhibiti wao katika eneo hilo. Mapigano sasa yamejikita katika eneo jirani la Kordofan.

Soma zaidi...

Dharau ya Amerika kwa Raia Wake Yenyewe Yawaacha Wanawake na Watoto na Njaa

SNAP (Programu ya Usaidizi wa Lishe ya Ziada) ni mpango wa shirikisho unaowasaidia watu binafsi, familia, na wale wenye ulemavu kupata manufaa ya kielektroniki ambayo hutumika kwa chakula, vinywaji visivyo na kileo, na mimea kukuza chakula chao wenyewe. Inaripotiwa kuwa kuna Wamarekani milioni 42 ambao hutegemea manufaa ya SNAP kujilisha wao wenyewe na familia zao. 54% ya watu wazima wanaopokea manufaa ya chakula ni wanawake, hasa kina mama wasio na waume, na 39% ni watoto, ambayo ina maana kwamba takriban mtoto 1 kati ya 5 hutegemea manufaa haya ili kuhakikisha hawalali njaa.

Soma zaidi...

Ukumbusho kwa Waislamu kuhusu Utakatifu wa Muislamu: Damu Yake, Mali Yake, na Heshima Yake

Vyombo vya habari vilisambaza habari za uhalifu wa kutisha uliotokea katika mji wa Al-Fashir nchini Sudan, wa mauaji, ubakaji, na uhamishaji uliosababisha maelfu ya familia kuhama. Na swali linalojitokeza ni: je, inawezaje kuwa rahisi kwa Muislamu anayeshuhudia kwamba hakuna mola wa haki ila Mwenyezi Mungu na kwamba Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na anaamini Siku ya Mwisho—inawezaje kuwa rahisi kwake damu ya ndugu yake Muislamu, mali yake, na heshima yake?!

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu