Njama Endelevu, Iliyoimarishwa ya Kimataifa ya Kuzuia Mapinduzi ya ash-Sham yasifikie Malengo na Misingi yake
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mwenyezi Mungu (swt) alipowapa watu wa ash-Sham baraka za kumwangusha dhalimu mhalifu wa Syria, asubuhi ya tarehe 8 Disemba 2024, licha ya mipango na njama kubwa zilizopangwa na ulimwengu wote wa Magharibi, ukiongozwa na Marekani, ili kuyabatilisha mapinduzi na kuyazuia yasifikie lengo lake, ulikuwa ni utashi, azma, na Iman ya watu ash-Sham, kwa zana zao hafifu na za kawaida, ambapo hatimaye walishinda dhidi ya jumuiya ya kimataifa.