Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 603
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan imeongeza amali zake za umma katika miezi ya hivi karibuni, ikiuhimiza Ummah kufanya kazi nayo ili kusimamisha jengo tukufu la Uislamu: Khilafah Rashida kwa njia ya Utume.
Waziri wa Fedha wa Ufaransa Roland Lescure alisema kwamba serikali haziwezi kuamua kama zitoe akiba ya ziada ya mafuta ya kimkakati ili kupunguza usumbufu unaosababishwa na vita vya Iran hadi muda unaowezekana wa mzozo huo utakapokuwa wazi. Katika muktadha huo huo, mashambulizi ya awali ya makombora ya Iran kwenye kituo cha gesi cha Ras Laffan nchini Qatar, mojawapo ya vituo vikubwa zaidi vya gesi asilia vilivyoyeyushwa duniani, yalisababisha kupungua kwa kasi kwa akiba ya gesi ya Uingereza. Akiba ya gesi asilia nchini Uingereza ilishuka hadi viwango vya kutosha kukidhi matumizi ya ndani kwa muda usio zidi masaa 48.
Utajiri na rasilimali za Ummah zinaendelea kufujwa ili kutajirisha Magharibi, huku ndani ya nchi, zikitumika kwa anasa zinazowaweka Waislamu mbali na mfumo wa maisha wa Kiislamu. Mnamo Alhamisi, 21/5/2026, Mamlaka Kuu ya Burudani ya Saudi Arabia ilitangaza muungano mpya wa Saudi Arabia na Misri unaolenga kujenga mfumo jumuishi wa matukio makubwa katika eneo hilo, unaounganisha nchi hizo mbili kwenye njia moja ya kuvutia wasanii na nyota wa kimataifa! Wakati huo huo, mnamo Jumatano, 20/5/2026, nchi za Baraza la Ushirikiano la Ghuba (GCC) na Uingereza zilitangaza makubaliano ya kihistoria na makubwa ya biashara huria yenye thamani ya takriban dolari bilioni 5, na kuifanya Uingereza kuwa taifa la kwanza la G7 kusaini makubaliano kama hayo na kambi ya Ghuba.
Hivi majuzi, Rais wa Urusi Vladimir Putin alitembelea China, na mwishoni mwa ziara hiyo taarifa ya pamoja ya zaidi ya nukta arubaini ilitolewa. Ndani yake, nchi hizo mbili zilitangaza mikataba na makubaliano kadhaa. Hata hivyo, kinachoonekana katika taarifa hiyo ni wito wa nchi zote mbili wa mpangilio mpya wa ulimwengu wa nchi nyingi. Pia inaeleweka kwamba ziara ya Putin nchini China ilikuja baada ya ziara ya Rais wa Marekani Donald Trump nchini China, na baada ya ziara ya Putin kukamilika ilitangazwa kwamba rais wa China anakusudia kutembelea Korea Kaskazini.
Serikali ya Shaea Al-Zandani mnamo Jumanne, 19/05/2026, ilianzisha hatua mpya ya kiuchumi ambapo ilipandisha bei ya dolari ya ushuru wa forodha kwa zaidi ya 100%, kutoka riyali 750 hadi riyali 1,550, na kuongeza bei ya chombo cha dizeli cha lita 20 kwa 24.5%, ikiruka kutoka riyali 29,500 hadi 36,000. Kisha ilijaribu kuwaziba macho watu wa Yemen kwa kuidhinisha posho ya gharama ya maisha ya 20% kwa wafanyikazi wa sekta ya umma, pamoja na kuwapa nyongeza yao ya kila mwaka inayostahili kwa miaka ya 2021-2024, na kufanya marekebisho ya viwango vya kazi ambayo yalikuwa yamesimamishwa kwa zaidi ya miaka 13.
Siku hizi Idd al-Adha inafika, ambapo furaha na huzuni zimechanganyika. Furaha katika mwitikio wa waumini kwa wito wa Mwenyezi Mungu wa Hijja, wakiitikia wito wake katika mkusanyiko unaowaunganisha kutoka pembe zote za dunia, pamoja na makabila na rangi zao mbalimbali, kwa kutii amri ya Mwenyezi Mungu na kupata radhi Zake. Na huzuni kubwa inawakumba nyoyo zao kwa masaibu yao tangu kupoteza nguvu yao na kuvunjwa kwa dola yao mikononi mwa mhalifu Mustafa Kemal. Ni Idd ya aina gani huku Gaza ikiendelea kutokwa na damu?! Idd ya aina gani huku kambi na meli za kivita za maadui wa Umma zikiwa katikati ya ardhi zake?! Idd ya aina gani huku wanawake huru wa Waislamu wakidhalilishwa huko Palestina, Turkestan Mashariki, Myanmar, na India?!
Assalamu alaikum wa Rahmatullah wa Barakatahu. Namuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu kwamba ujumbe wangu utakufikia ukiwa na afya njema zaidi. Swali langu, ewe Sheikh muheshimiwa, ni hili: Hii ni Hadith sahih iliyopokewa na Masheikh wawili (Bukhari na Muslim) kutoka kwa Mtume (saw) yenye lafudhi: وَإِنَّ اللَّهَ لَيُؤَيِّدُ هَذَا الدِّينَ بِالرَّجُلِ الْفَاجِرِ “Hakika, Mwenyezi Mungu huenda akaipa nguvu dini hii hata kupitia mtu muovu.”