Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 585
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo tarehe 5/12/2025, Trump alitangaza kwa umma hati mpya ya Mkakati wa Usalama wa Kitaifa wa Marekani yenye kurasa 33. Kuna tofauti gani kati ya hati hii na zile zilizotangulia, kama vile mkakati wa Biden?
Baada ya vikosi vya Baraza la Mpito la Kusini (STC) nchini Yemen, vikiongozwa na Aidarus al-Zubaidi, mjumbe wa Baraza la Rais, kupeleka vikosi vyao huko Hadramawt na al-Mahrah, hali ikawa ngumu sana. Rais wa STC Rashad al-Alimi alisitisha makubaliano ya pamoja ya ulinzi na Imarati na kudai kwamba iondoe vikosi vyake kutoka Yemen ndani ya masaa 24. Saudi Arabia ilimuunga mkono mara moja na kushambulia silaha za Imarati katika Bandari ya Mukalla. Kisha Saudi Arabia ilidai kwamba Imarati itii matakwa ya Rashad al-Alimi na kuondoa vikosi vyake kutoka Yemen. Imarati baadaye iliondoka, na hatimaye, al-Zubaidi alikimbilia Imarati. Kwa hivyo, ni nini kilicho nyuma ya kuongezeka huku kwa mgogoro wa Yemen? Je, Uingereza inapoteza washirika wake nchini Yemen? Na je, mzozo huu una vipimo vya kimataifa?
Ummah umekuwa katika mzunguko wa migogoro kwa miaka 105. Mzunguko wa migogoro ambao umeathiri Ummah ni ule ambao umekuwa wa kimakusudi na wenye shabaha katika kusababisha aina mbalimbali za ukandamizaji na mateso kwa watu na mazingira. Leo, tunashuhudia mauaji kadhaa ya halaiki: Gaza na Palestina, Kashmir, Turkistan Mashariki, Sudan, na vitendo vya vurugu vya kudumu nchini Nigeria, Ethiopia, Syria, Lebanon, Congo, na Venezuela. Orodha hii inaweza kuendelea kwa sababu kila siku mji au nchi mpya inasogezwa karibu na janga kubwa na Magharibi ya kikoloni, yaani Amerika, ambayo hupora na kuyumbisha nchi baada ya nchi ili kuhakikisha kwamba udhibiti wake unabaki imara.
Matukio yanatokea kwa kasi kubwa kaskazini mashariki mwa Syria, na Vikosi vya Kidemokrasia vya Syria (SDF) vinapoteza udhibiti wa maeneo hayo kwa kasi kubwa, huku serikali ya Syria ikiyachukua. Yote haya yalitokeaje? Hili linapaswa kuelewekaje ikizingatiwa kwamba serikali na SDF ni vibaraka wa Amerika? Na licha ya idhini ya Marekani kwa serikali ya Syria kuwa wazi kama mwanga wa mchana katika kuteka maeneo hayo, utawala wa Trump unapanga nini nchini Syria au viunga vyake?
Waislamu ni Ummah mmoja, tofauti na watu wengine; Mola wao Mlezi ni Mmoja, Dini yao ni moja, Mtume wao ni mmoja, Kibla chao ni kimoja, na Kitabu chao ni kimoja.
Hizb ut Tahrir Amerika ilifanikiwa kufanya kongamano lake la kila mwaka kwa mwaka huu 1447 H (2026 M), kama sehemu ya kampeni ya kimataifa iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kuvunjwa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab, 1342 H. Kongamano hilo lilitumika kama wito kwa Waislamu kote duniani kutambua na kutimiza wajibu wao wa kuregesha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah kwa njia ya Mtume wetu Muhammad (saw).
Hizb ut Tahrir / Amerika ilifanya kwa mafanikio Kongamano lake la kila mwaka la Khilafah kama sehemu ya kampeni ya kimataifa kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kufutwa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab, 1342 H. Kongamano hilo lilitumika kama wito kwa Waislamu kote duniani kutambua na kutimiza wajibu wa kuregesha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu, kama ulivyoamriwa na Mwenyezi Mungu (swt), kupitia kusimamisha tena Khilafah kwa njia ya Mtume wetu Muhammad (saw).
Katika kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah iliyotokea mnamo Rajab 1342 H / Machi 1924 M, jana, Jumapili, 29 Rajab 1447 H / 18 Januari 2026 m, Hizb ut Tahrir / Tanzania ilifanya semina fupi katika Masjid Taqwa, Ilala Bungoni katika jiji la Dar es Salaam.