Serikali ya Tunisia Itaendelea na Uzembe Wake Hadi Lini na Kuruhusu Malori Haya ya Kifo Kuchukua Maisha ya Wafanyikazi wa Kike wa Mashamba?
- Imepeperushwa katika Kitengo cha Wanawake Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Ghadhabu na hasira ziliongezeka nchini Tunisia wiki iliyopita kufuatia ajali nyingine mbaya, wakati huu katika wilaya ya Mazouna katika jimbo la Sidi Bouzid. Ajali hiyo iliwaacha wafanyikazi kadhaa wa kike wa shambani wakiwa wamejeruhiwa na wawili wakiwa wamekufa katika eneo la tukio. Tunisia inashuhudia kujirudia kwa matukio kama hayo kutokana na serikali kushindwa kukomesha usafiri usiodhibitiwa na kuboresha hali mbaya ya wafanyikazi wa kike wa mashamba! Bila shaka, serikali hii inakwepa kutoa tarakimu na takwimu sahihi zinazoonyesha ukubwa wa janga hilo!



