Jumanne, 15 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/07
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kauli za Uhalalishaji Mahusiano ni Tangazo la Wazi la Kuoanishwa na Adui na Kujitenga na Ummah

Siku za hivi karibuni zimeshuhudia msururu wa kauli zilizotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Badr Abdelatty wakati wa ushiriki wake katika makongamano ya kimataifa. Maarufu zaidi kati ya kauli hizi ni msisitizo wake juu ya “umuhimu wa 'Israel' kuishi kwa amani na kuoanishwa ndani ya eneo hili,” na “utayari kamili wa kuhalalisha mahusiano na ‘Israel’" pamoja na Saudi Arabia na nchi zengine, na kauli yake kwamba “suluhisho pekee kwa mustakbali ni kuanzishwa kwa dola ya Palestina isiyo na kijeshi inayoishi kwa amani na ‘Israel’.” Kauli hizi waziwazi zinaakisi mwelekeo unaofuatwa na tawala zilizoko katika nchi za Kiislamu: njia iliyojaa uhalalishaji mahusiano na umbile nyakuzi, na hata juhudi za kulilinda na kulioanisha ndani ya eneo hili, kuhudumia mradi wa kikoloni wa Magharibi.

Soma zaidi...

Suluhisho la Dola Mbili ni Kejeli ya Karne isiyo na Aibu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh inashutumu vikali kile Prof. Yunus alisema kwenye Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa, “Ni kwa msingi wa mipaka ya kabla ya 1967 tu, na Israel na Palestina wakiishi bega kwa bega kwa amani, haki inaweza kutendeka”. Wakati watu wa Palestina wanaangamizwa mbele ya macho yetu na Mayahudi kunyakua 78% ya Palestina kinyume cha sheria, ni vipi haki inaweza kutendeka kwa kuruhusu ‘Israel’ kuishi bega kwa bega na Palestina! Kwa nini tunaita makundi machache ndani ya umbile haramu la Kiyahudi kuwa ni dola (Palestina), lakini haina hata jeshi lake?

Soma zaidi...

Baada ya Mashambulizi ya Umbile la Kiyahudi kwa Sumud Flotilla Wito wa Dharura kwa Maafisa na Askari katika Majeshi ya Waislamu Jeshi Husagwa sagwa na Jeshi Pekee

Enyi Wanajeshi: Mumeshuhudia shambulizi la umbile la Kiyahudi dhidi ya Sumud Flotilla iliyosafiri bahari ili kuvunja kuzingirwa kwa kaka na dada zenu mjini Gaza, na mkasikia vilio vyao vya kuomba msaada, na mkaona kwa macho yenu uovu wa watawala, ufisadi wao, ukosefu wao wa hisia, na kufeli kwao kuinusuru Gaza na wanaharakati wa flotilla. Imekudhihirikieni pia kwamba watawala hao walimfanyia khiyana Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kuwaangusha Waumini walipoangusha hadharani kile walichokiita “chaguo la vita” kwa kunyenyekea matamanio ya viongozi wa ukafiri.

Soma zaidi...

Rais wa Lebanon Atoa Wito wa Kuidhinishwa Haraka kwa Mpango wa Trump wa Gaza!

Enyi Watu wa Lebanon, Enyi Watu wa Palestina, Enyi Umma wa Uislamu: Rais wa Lebanon alitoa wito wa kuidhinishwa haraka kwa mpango wa Trump wa kusimamisha vita mjini Gaza, akijua kwamba ni mpango wa kufikia maslahi ya umbile la Kiyahudi, ambalo limeshindwa kulazimisha kupitia nguvu ya silaha, kama vile kujisalimisha kwa mujahidina, kuachiliwa huru kwa wafungwa wa Kiyahudi na malengo mengine. Ili kufikia malengo haya kwa umbile halifu kupitia ujanja wa Trump.

Soma zaidi...

Mpango wa Trump ni Uvamizi wa Kikatili wa Kijeshi Ambao Unahitaji Haraka Kubadilishwa kwa Watawala Wanaokubaliana na Mpango Wake

Katikati ya miaka miwili ya vita vya mauaji ya halaiki vinavyoendelea mjini Gaza, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza mpango wa kina unaolenga kumaliza vita katika Ukanda wa Gaza na kufikia “amani ya kudumu” katika Mashariki ya Kati. Mpango huu ulitangazwa wakati wa mkutano wa pamoja wa waandishi wa habari uliofanyika mnamo Jumatatu, 29/9/2025, na mhalifu aliyelaaniwa Benjamin Netanyahu katika Ikulu ya White House. Alisema, “Leo tunalifanyia kazi suluhisho la kina kwa kadhia ya Palestina, sio Gaza pekee.” Miongoni mwa mambo muhimu zaidi katika mpango wake ni mpango wa “kuanzisha chombo kipya cha kimataifa cha uangalizi wa Ukanda wa Gaza kinachoitwa Baraza la Amani.” Aliongeza, “Mimi binafsi nitakuwa mwenyekiti wa baraza hili huko Gaza, kwa ushiriki wa Tony Blair.” Alisisitiza kwamba “washirika wetu wa Kiarabu na Waislamu wako tayari kuchukua majukumu yao kwa Gaza,” na kwamba “ufadhili ni muhimu ili kuruhusu mafanikio mjini Gaza, na tutajenga mustakabali salama zaidi kwa wote.”

Soma zaidi...

Mpango wa Trump ni Sumu Hatari, Ukaliaji Kimabavu wa Marekani na Umoja wa Mataifa wa Gaza, na Uhalifu Mkubwa Uliofanywa na Watawala wa Waislamu

Kujisalimisha na kutoa silaha, kuregeshwa kwa mateka na mabaki ya wafu, na uvamizi unaoongozwa na Marekani, inayoongozwa na Trump kwa jina la Baraza la Amani, likisaidiwa na mwenye chuki dhidi ya Uislamu, Tony Blair, na kutekelezwa na tawala za eneo hili – hizi ndizo sifa za mpango mpya wa Trump, ambao aliutangaza. Amewashukuru viongozi wa nchi za Kiarabu na Kiislamu na washirika wake barani Ulaya kwa mwitikio wao wa dhati kwake, na kutangaza kuwa viongozi wa eneo hilo wanashiriki kikamilifu katika mpango huo wa amani.

Soma zaidi...

Uacheni Umma Ufanye Uamuzi Wake, Enyi Watawala Waoga!

Hatukushangazwa, wala Umma wa Kiislamu haukushangazwa na ukaribishaji wa watawala wasaliti wa Waislamu wa mpango wa rais wa Marekani Donald Trump wa kuipoteza Gaza, kwani wao wametuzoezesha sisi kuwa waoga, badala ya kula njama na wakoloni makafiri dhidi ya masuala yetu. Trump alikuwa amekutana na baadhi yao jijini New York kando ya mikutano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, mnamo Jumanne tarehe 23/9/2025, na wakamsifu na kutangaza kumtegemea yeye kumaliza vita dhidi ya Gaza. Mara tu Trump alipotangaza mpango wake wa ukoloni, waliharakisha kuukaribisha. Wasingewezaje kuukaribisha, wakati hakuna hata mmoja wao aliyesubutu kufanya vyenginevyo, kwa kuwa wamepoteza ari na ushujaa wa wanaume.

Soma zaidi...

Simama pamoja na Watu Wasioteteleka wa Gaza, Sio na Trump Mwenye Kiburi!

Miaka miwili imepita tangu mauaji ya halaiki yanayofanywa na umbile nyakuzi la Kiyahudi huko Gaza, ambalo liliyafanya ili kuficha kushindwa kukubwa lilikokupata mnamo Oktoba 7, 2023. Miaka miwili ambayo kila siku ilishuhudia mauaji mapya na ukatili usioelezeka, na dunia nzima imeshuhudia ukatili wa Mayahudi wanyakuzi ambao unakinzana na akili. Watoto, watoto wachanga, nyumba, shule, misikiti na hospitali zililengwa. Watawala wa nchi za Kiislamu walikutana mara kwa mara, wakazungumza, wakalaani, na kisha kutawanyika. Kila shutma iliwashajiisha Mayahudi kufanya uvamizi na mauaji makubwa zaidi. Umbile la Kiyahudi lilifikia hatua ya kuzuia kuingia kwa kipande cha mkate au tama la maji ndani ya Gaza kwa miezi mingi mirefu.

Soma zaidi...

Katika Ziara ya Amerika: Yote yako Pamoja – Kufedheheshwa, Kusihi, Uhalali, Makubaliano, na Majukumu Mapya!

Ziara ya Rais Erdoğan wa Uturuki nchini Marekani kushiriki katika mikutano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ilikuwa mandhari ya kufedhehesha, sio kwake tu bali kwa viongozi wote wa dola pia. Rais mwenye kiburi wa Marekani Donald Trump alitoa hotuba mbele ya Baraza Kuu ambapo alitangaza kwamba “Marekani imebarikiwa kuwa na uchumi imara zaidi, mipaka yenye nguvu zaidi, jeshi lenye nguvu zaidi...” na kwamba ndani ya miezi minane ya utawala wake aliitoza dunia kodi ya ziada ya kiasi cha dolari trilioni 17, na kwamba Marekani iko katika nafasi nzuri huku nchi zengine “zinaenda kuzimu.” Alisema kuwa maamuzi ya Umoja wa Mataifa hayana maana, na kudai kwamba alimaliza vita saba ndani ya miezi saba. Aliitaja tarehe saba ya Oktoba 2023 kama “unyama wa magaidi wa Hamas,” akizingatia kuwa suluhisho liko katika kuachiliwa huru mara moja kwa wafungwa, na kuongeza kuwa dini inayonyanyaswa zaidi duniani ni Ukristo.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu