Jumamosi, 21 Muharram 1446 | 2024/07/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Sera ya Serikali ya Kisekula nchini Uturuki inayokula Njama Dhidi ya Mapinduzi ya Ash-Sham ndiyo Sababu ya Kulipuka kwa Kiota cha Mapinduzi katika Ukombozi

Kauli za maafisa nchini Uturuki kuhusiana na maridhiano na utawala uliopitiliza na kufunguliwa kwa mipaka kwa ajili ya maandalizi ya uhalalishaji mahusiano na utawala huo, na vitendo vinavyouandama vya ubaguzi wa rangi dhidi ya watu wa Syria hasa wa Kayseri ni matokeo ya kimaumbile ya maneno ya uchochezi dhidi ya watu wa Syria, wakimbizi wanaoukimbia utawala wa Assad, na wanasiasa nchini Uturuki, wawe wenye mamlaka au wa upinzani, yote haya si lolote bali ni kuonyesha sura halisi ya utawala wa Uturuki, ambao unatekeleza mpango wa Marekani katika eneo hilo kufikia kile wanakiita suluhisho la kisiasa na kurudisha yale mabaki ya mji uliokombolewa kwenye kumbatio la utawala wa kihalifu.

Soma zaidi...

Maadui wa Mapinduzi Wanaogopa Vuguvugu la Ummah na Wanaonya kuhusu Kupoteza Udhibiti

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Hakan Fidan, ameonya juu ya kuongezeka kwa taharuki nchini Syria, na kulitaja kuwa eneo jengine hatari linaloonyesha mwelekeo wa kupamba moto. Amefahamisha kuwa kadhia ya Syria inahitaji mkabala wa kina ili kufikia suluhu endelevu. Kauli hii aliitoa wakati wa ufunguzi wa mkutano wa sita wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Baraza la Ushirikiano wa Ghuba (GCC), uliofanyika jijini Doha mnamo tarehe 9 Juni 2024.

Soma zaidi...

Faili ya "Kutekwa nyara na Kutoweka" ni Sanduku Jeusi Linalofichua Kiwango cha Uhalifu wa Uongozi wa Shirika la HTS

Mnamo tarehe 14/5/2024, kikao kilichofanywa na kundi la familia na jamaa za watu waliotekwa nyara katika magereza ya usalama ya Hay’at Tahrir al-Sham (HTS) kilitawanywa kwa njia ya kijambazi na ladha ya Assad. Kikao hicho kilikuja baada ya uahirishaji mambo mengi na shirika la HTS kuhusiana na hasa suala hili.

Soma zaidi...

Madai ya Tovuti ya France 24 ni ya Uongo na ya Kashfa katika Jaribio la Mbaya la Kuficha Harakati ya Amani katika eneo la Kaskazini lililo Kombolewa

Katika ripoti ya kushangaza ya vyombo vya habari juu ya ukamataji na maandamano ambayo yamefanyika katika maeneo yaliyokombolewa kwa zaidi ya miezi miwili, waangalizi wa France 24 walitushangaza kwa mkusanyiko wa uwongo wa makusudi ambao chaneli kama France 24 haifai kufanya isipokuwa ikiwa wahariri wake bado wangali chini ya athari ya mshtuko wa maandamano yaliyozuka katika nchi yao iliyokumbwa na mgogoro.

Soma zaidi...

Njama Mpya Inatayarishwa Dhidi ya Mapinduzi Yanayohitaji Kuingiliwa Upya na Ujasusi wa Hay'at Tahrir al-Sham

Mnamo Jumapili tarehe 7/5/2023, Hay'at Tahrir al-Sham (HTS) alikamata idadi ya wanachama wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Syria, akiwemo Mkuu wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Syria, Ahmed Abdul Wahhab, Mjumbe wa Afisi ya Habari, Nasser Sheikh Abdul Hai, na baadhi ya wabebaji wa Dawah katika maeneo ya Idlib.

Soma zaidi...

Tetemeko la Ardhi Limefichua Sura Halisi ya Jumuiya ya Kimataifa na Mashirika Yake ya Kimataifa

Watu wa Ash-Sham waliamka alfajiri siku ya Jumatatu, 6/2/2023 na tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa nyuzi 7.8 kwenye kipimo cha Richter, ambalo lilidumu kwa karibu dakika mbili, na kuacha uharibifu wa kutisha katika maeneo mengi ya miji ya Syria, kwani idadi ya waliokufa katika tetemeko hilo ilifikia 3,581, na zaidi ya majeruhi 12,400.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu