Jumamosi, 23 Dhu al-Hijjah 1445 | 2024/06/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mumewaachia Nini Wananchi Baada ya Mkate?! Dumisheni Usaidizi wenu na Muregeshe Haki za Watu

Dkt. Mostafa Madbouly, Waziri Mkuu, alitangaza ongezeko la bei ya mkate iliyofadhiliwa kutoka piaster 5 hadi piaster 20 kuanzia Juni ijayo. Madbouly aliongeza katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo kwamba gharama ya mkate kwa serikali inafikia piasters 125, lakini iliuzwa kwa piaster 5 pekee, hivyo serikali ina gharama ya ruzuku ya pauni bilioni 120.

Soma zaidi...

Mkataba wa Khiyana Unalinda Umbile la Kiyahudi na Kulifanya Jeshi la Misri kuwa Mshirika katika Uhalifu wake, Kumwaga Damu ya Wanajeshi wa Kinanah

Mwanajeshi mmoja wa Misri aliuawa katika makabiliano ya risasi kati ya wanajeshi wa 'Israel' na Misri kwenye kivuko cha Rafah mnamo siku ya Jumatatu, kama ilivyothibitishwa na Shirika la Utangazaji la 'Israel'. (Sky News Arabia, 27/5/2024).

Soma zaidi...

Mashujaa wa Utawala wa Misri Hawaelekezwi Dhidi ya Umbile la Kiyahudi Badala yake Unaendelea na Juhudi zake katika Kuzingira, Kunyima Chakula, na Kuua Watu wa Gaza!

Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani iliitaka Misri mnamo siku ya Jumatano kufanya kila iwezalo kuhakikisha mtiririko wa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza. Wakati huo huo, Cairo ilieleza kuwepo kwa chama cha Kipalestina katika kivuko cha Rafah ili kupokea msaada huo.

Soma zaidi...

Je! Uhalifu Uliopita Haukutosha Kukomesha Makubaliano ya Khiyana? Au Kukomeshwa kwake Kunahitaji Mauaji Makubwa Zaidi?

Operesheni "ndogo" ya kijeshi iliyofanywa na jeshi la umbile la Kiyahudi huko Rafah ya Palestina hivi karibuni ilifanya mazungumzo mapya juu ya hali ya Misri ya kuamiliana na mpango wa umbile la Kiyahudi endapo kutatokea "uvamizi kamili wa Rafah," kwa kuzingatia maonyo ya mara kwa mara ya Misri kuhusu "madhara ya uvamizi wa mji huo kwa Wapalestina,” na hakikisho kutoka kwa umbile la Kiyahudi la "kuendelea kwa operesheni hiyo."

Soma zaidi...

Kinachopaswa kufanywa na Misri na Jeshi Lake ni Kuvunja Mipaka na Kuling'oa Umbile la Kiyahudi, Sio Kutafuta Usitishaji Vita na Kutoa Misaada!

Balozi Ahmed Abu Zaid, msemaji rasmi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri, alisisitiza kuwa ‘Israel’ lazima ikomeshe ukiukaji wake, akithibitisha kuwa Israel inakiuka sheria za kimataifa. Alidokeza kuwa maamuzi ya haki ya kimataifa yanaifunga ‘Israel’.

Soma zaidi...

Ni Nani Atakayefuta Aibu Yenu, Enyi Wanajeshi wa Kinana?!

Baada ya mkuu wa ujasusi wa Misri kuwaonya Hamas juu ya ulazima wa kukubali makubaliano ya kubadilishana wafungwa yaliyoandaliwa chini ya mwavuli wa Marekani ndani ya wiki mbili, na kisha tangazo la redio ya jeshi la umbile la Kiyahudi kwamba Misri ingekubali kuivamia Rafah kwa masharti ya kuhakikisha kuwa Wapalestina hawafurushwi hadi Sinai, pia mnamo Jumapili asubuhi, tarehe 11/2/2024, redio hiyo ilinukuu maafisa wa Misri wakiufahamisha upande wa 'Israel' wa kutoupinga uvamizi wa kijeshi wa Rafah katika mji wa Rafah kwa sharti la kuepuka majeruhi ya raia wa Palestina.

Soma zaidi...

Kwa nini Rafah Inapigwa Mabomu na Kuzingirwa na Serikali ya Misri?!

Katika matangazo ya moja kwa moja kwenye Chaneli ya Al Jazeera mnamo Jumatatu asubuhi, Februari 12, 2024, msemaji wa Wizara ya Afya, Ashraf al-Qudra, alizungumza na Al Jazeera akielezea uharibifu uliotokea huko Rafah na nyumba zilizolipuliwa, ambazo zilikuwa zinakaliwa na wakaazi na watu waliohamishwa makao yao.

Soma zaidi...

Serikali ya Misri Yawapa Watu Asali huku Wakinywa Sumu Mikononi Mwake!

Msemaji wa Afisi ya Rais wa Jamhuri, Ahmed Fahmy, alithibitisha kuwa dola hii imepata mafanikio mengi katika ngazi na nyanja zote na kueleza kuwa serikali inajitahidi kukabiliana na changamoto hizo akisema: “Ni jambo la kimaumbile kwa wananchi kuhisi afueni inayotokea wakati utabikishaji umekamilika na juhudi zote kuwekwa wazi.”

Soma zaidi...

Mayahudi Wamefichua Mzingiro wa Utawala wa Misri kwa Watu wa Gaza na Kuwa ni Mshirika katika Uhalifu wake Dhidi Yao!

Afrika Kusini ilifungua kesi dhidi ya umbile la Kiyahudi mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki, na umbile la Kiyahudi likajibu kwa kukana mashtaka hayo, likijua kuwa hata ikiwa litakiri na kuhukumiwa na Mahakama ya Kimataifa, hakuna mtu atakayeweza kulishambulia au kulitia hatiani.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu