Jumatano, 14 Muharram 1447 | 2025/07/09
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mpango wa Mosaic: Kubadilisha Chapa Mkakati Uliofeli na Jaribio Jipya la Kuidhibiti Taliban

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hivi karibuni lilifanya kikao maalum kujadili hali ya Afghanistan. Katika mkutano huu, Roza Otunbayeva, mkuu wa Misheni ya Misaada ya Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan (UNAMA), aliwasilisha mfumo mpya wa kina unaoitwa "Mpango wa Mosaic." Alisisitiza kuwa mpango huu haulengi "kusawazisha hali nchini Afghanistan," bali unalenga kuendeleza maslahi ya kweli ya watu wa Afghanistan.

Soma zaidi...

Marekani Yapanga Mpango Mpya baada ya Mpango wa Awali Kufichuliwa na Kutibuliwa na Umma

Makundi yenye silaha ya Rohingya yameanza kusajili kutoka kambi za wakimbizi za Cox's Bazar kusaidia katika mapigano dhidi ya Jeshi la Arakan huko Rakhine. Taarifa hiyo ilifichuliwa katika ripoti moja ya Shirika la Kimataifa la kutatua Migogoro yenye kichwa "Bangladesh/Myanmar: Hatari za Waasi wa Rohingya". Ripoti hiyo inabainisha kuwa, baada ya Jeshi la Arakan kupata ushindi dhidi ya jeshi la Myanmar huko Rakhine, makundi ya Rohingya yamezidi kuwa changamfu na yamekubali kufanya kazi kwa pamoja dhidi ya Jeshi la Arakan, kundi ambalo lenye Mabudha wengi wa Rakhine kuwa kambi yake. (The Business Standard, 18 Juni 2025)

Soma zaidi...

Erdoğan anapaswa Kuhutubia Umma wenye Ikhlasi na sio Walinzi wa Sykes-Picot kwa Umoja na Udugu wa Kiislamu!

Akihutubia Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu jijini Istanbul, Rais Recep Tayyip Erdoğan ametoa wito wa kuwepo umoja na udugu mkubwa zaidi miongoni mwa nchi za Kiislamu. Erdoğan pia alisema, "Hatutaruhusu kuanzishwa kwa agizo jipya la Sykes-Picot katika eneo letu mipaka kuchorwa kwa damu." Na alisisitiza kwa mara nyengine kwamba suluhisho liko katika "diplomasia na mazungumzo".

Soma zaidi...

Umebarikiwa kwa Nguvu, Umedhoofishwa na Mgawanyiko

"Pentagon yasema Marekani haitaki kuanzisha vita na Iran" - hii, baada ya kudondosha mabomu kumi na nne aina ya bunker-buster kwenye vituo vitatu vya nyuklia ndani ya ardhi ya Iran. Kauli kama hiyo si ya kinafiki tu - ni ya kuchukiza. Inaakisi mawazo ya kiburi, ya kikoloni. Mtu yeyote mwenye akili timamu anawezaje kuamini kwamba vita sio nia pindi taifa linapofanya mashambulizi yaliyoratibiwa kwa taifa jengine?

Soma zaidi...

Vita vya Amerika na umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran: Kimya cha Watawala na Kujisalimisha kwa Murshed

Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza makubaliano kamili kati ya Israel na Iran juu ya usitishaji kamili wa mapigano. Katika jukwaa lake la Kijamii la Truth, Trump alisema: "PONGEZI KWA KILA MTU! Imekubaliwa kikamilifu na kati ya Israel na Iran kwamba kutakuwa na Usitishaji Vita Kamili na Jumla (katika takriban saa 6 kutoka sasa, wakati Israel na Iran zitakapomaliza na kukamilisha misheni zao zinazoendelea, za mwisho!), kwa masaa 12, ambapo Vita vitazingatiwa, VIMEMALIZIKA! Trump alisifu pande zote mbili, akisema: "Misuli, Ujasiri, na Ujasusi kumaliza" mzozo na kusema kwamba ulimwengu na Mashariki ya Kati ndio "WASHINDI halisi".

Soma zaidi...

Wadhifa wa Rais eneo la Asia ya Kati ni Sawia na Ufalme

Shirika la habari la Radio Liberty liliripoti mnamo tarehe 29 Mei: "Putin alifanya mazungumzo na Rustam Emomali, mwenyekiti wa bunge kuu la Tajikistan. Katika mfumo wa ziara yake rasmi jijini Moscow, Mwenyekiti wa Majlisi Milli Majlisi Oli ya Tajikistan na Meya wa Dushanbe Rustam Emomali walifanya mazungumzo na Rais wa Urusi Vladimir Putin, Spika wa Baraza la Federali Valentina Matvienko na Mwenyekiti wa Jimbo la Duma Vyacheslav Volodin.

Soma zaidi...

Ziara ya Usaliti

Katika wakati ambapo ulimwengu wa Kiislamu unavuja damu—kuanzia Gaza hadi Kashmir, hadi barabara za Tehran—ziara ya Jenerali Asim Munir kwa Rais wa Marekani Donald Trump si tu kwamba ni uziwi bali ni usaliti wa kiasi kikubwa. Mkutano huo, uliofanyika katika Ikulu ya White House na uliandaliwa na Trump kama ishara ya kushukuru dori ya Munir katika kutuliza hali iliyokaribia vita na India, inasifiwa na sehemu za utawala wa Pakistan kama hatua ya kimkakati ya kidiplomasia.

Soma zaidi...

Jinsi Viongozi wa Waislamu Wanavyoitelekeza Gaza kwa ajili ya Diplomasia na Miamala

Rais wa Indonesia Prabowo Subianto alihimiza kusitishwa kwa mapigano mara moja kati ya 'Israel' na Hamas, na akatoa wito wa kusitishwa kwa mzozo wa 'Israel' na Iran. Akizungumza nchini Singapore na Waziri Mkuu Lawrence Wong, Prabowo alisisitiza haja ya azimio la amani kupitia diplomasia. Alionyesha wasiwasi wake mkubwa juu ya vifo vya raia huko Gaza na kuongezeka kwa mvutano katika Mashariki ya Kati. Zaidi ya hayo, alizungumzia mzozo wa Myanmar, akisisitiza kujitolea kwa ASEAN kwa Makubaliano ya Mambo Tano ya kukomesha vurugu na kukuza mazungumzo jumuishi. Indonesia na Singapore zilikubali kuendelea kuunga mkono ushirikiano wa amani nchini Myanmar na kuzingatia kanuni za ASEAN za uthabiti wa kikanda na juhudi za kibinadamu.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu