Kuongezeka kwa Umwagaji damu kwenye Mpaka wa Pakistan na Afghanistan na Kushindwa kwa Pande zote mbili Kushikamana na Hukmu ya Mwenyezi Mungu
- Imepeperushwa katika Pakistan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mbali na sera ya “kujizuia” iliyotabanniwa na serikali za sasa za Pakistan na Afghanistan kwa maadui wa Umma – Mayahudi, Mabaniani, na Waamerika – Pakistan pamoja na Afghanistan zilitangaza kwamba makumi ya wanajeshi kutoka kila upande walikuwa wameuawa katika mapigano ambayo yalizuka kwenye mpaka wao wa pamoja. Makabiliano hayo yalianza mnamo Jumamosi jioni kwa operesheni iliyoanzishwa na vikosi vya Taliban, na kusababisha Islamabad kuapa kutoa jibu kali. Kabul, kwa upande wake, ilitangaza kuwa vikosi vyake vilifanya operesheni dhidi ya vikosi vya usalama vya Pakistan ili kulipiza kisasi kwa ukiukaji wa mara kwa mara na uvamizi wa anga unaofanywa na jeshi la Pakistan katika eneo la Afghanistan.