Kati ya Usaliti wa Palestina na Kashmir na Utumwa kwa Amerika Asim Munir Anafanya Nini Mbele ya Firauni Wa Zama Zetu, Trump?
- Imepeperushwa katika Pakistan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Katika wakati ambapo Amerika inapigana vita dhidi ya jirani Muislamu, Iran, kwa kutumia mkono wake mchafu katika eneo hilo, umbile la Kiyahudi, Rais wa Marekani, Donald Trump, alimkaribisha Mkuu wa Majeshi wa Pakistan mnamo Jumatano, 18 Juni 2025, kwa chakula cha mchana katika mkutano ambao haujawahi kushuhudiwa katika Ikulu ya White House. Kinachotia shaka kuhusu mkutano huu, na muda wake, ni kwamba ni mara ya kwanza kwa rais wa Marekani kumkaribisha mkuu wa jeshi la Pakistan katika Ikulu ya White House, bila ya kuwepo kwa afisa yeyote mkuu wa kiraia wa Pakistan, kuashiria umuhimu wa mkutano huo, na unyeti wa mada yake.