Alhamisi, 21 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/11
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Enyi Waislamu: Je, bado mna matumaini kwa Watawala wenu Ruwaibidha?!

Umbile la Kiyahudi bado linatekeleza uhalifu wake dhidi ya watu wa Gaza, hivyo makumi ya mashahidi huongezeka kutokana nao kila siku. Pia bado linapiga mzingiro wake juu ya Gaza, hivyo watu wake wanakufa kwa njaa, kwa kuwa hawana chakula, vinywaji, dawa, au makao, licha ya jitihada fulani za kupeleka misaada kwao kwa uoga! Lakini mamia ya maelfu hawapati tonge ambalo kwalo wanaweza kuzuia njaa zao au kunyamazisha njaa ya watoto wao, kwa hiyo wamekuwa wanakufa kwa njaa mbele yao na mbele ya macho ya ulimwengu wote bila msaidizi au mwenye kuwanusuru.

Soma zaidi...

Mbwa Mwitu Hapaswi Kulaumiwa kwa Uvamizi wake ikiwa Mchungaji ndiye Adui wa Kondoo

Watoto watatu walifariki katika Jimbo la Khartoum baada ya kupokea dozi ya chanjo ya ukambi. Wizara ya Afya imefungua uchunguzi kuhusu dhurufu za vifo vyao. Sudan Tribune iligundua kuwa watoto wawili walikufa ndani ya saa moja baada ya kupokea chanjo ya ukambi, huku mtoto wa tatu akifa siku tisa baada ya kusaidiwa kupumua katika Hospitali ya Al-Balak mjini Omdurman. (Sudan Tribune, Agosti 5, 2025)

Soma zaidi...

Tarehe 5 Agosti 2024 ni Siku ya Uasi wa Watu dhidi ya Dhalimu na Utawala wa Kidhalimu, ambao ungali Unaendelea; kinachojulikana kama 'Tangazo la Julai' ni Hati ya Usaliti wa Vyama vya Kisiasa vinavyounga mkono Marekani ili kuangamiza Uasi wa Watu

Wananchi wakiwa wamekata tamaa sana, wamepita mwaka mmoja tangu kuanguka kwa Hasina katika uasi mkubwa dhidi ya dhalimu Hasina na utawala dhalimu mnamo Agosti 5, 2025. Kwa sababu baada ya kuanguka kwa dhalimu Hasina, vibaraka wa Marekani na vyama vya kisiasa vyenye uchu wa madaraka vimechukua mshiko wa kubainisha hatima ya watu na kuweka vikwazo katika kutekeleza matumaini na matarajio ya watu na wameendelea na majaribio yao maovu na kuteka nyara uasi huo. Kinachojulikana kama 'Tangazo la Julai' ni hatua isiyo na aibu ya jaribio hili ovu. Watu wamekataa utumwa wa Marekani na sarakasi za kisiasa kwa chuki. Yaliyo mbali na kuakisi matarajio ya watu, Tangazo hili la Julai halitambui hata matukio kama vile njama ya India huko Pilkhana na mauaji ya halaiki ya watu wanaopenda Uislamu huko Shapla Chattar.

Soma zaidi...

Kashmir Haiwezi Kukombolewa Bila Kubadilisha Uongozi Unaopoteza Fursa ya Dhahabu ya Kuikomboa Kashmir, kwa ajili ya Kumfurahisha Trump

Leo, tarehe 5 Agosti 2025, miaka sita imepita tangu kuunganishwa kwa lazima kwa Kashmir Inayokaliwa kimabavu na Raja Dahir wa zama hizi, Modi. Kulingana na makubaliano yaliyofikiwa nchini Marekani, kuisalimisha Kashmir ilikuwa ni usaliti wa wazi wa uongozi wa kisiasa na kijeshi wa Pakistan wa wakati huo, serikali ya Bajwa-Imran. Miezi michache tu baadaye, Jenerali Bajwa aliendeleza usaliti huu kwa kutia saini makubaliano ya kusitisha mapigano, na Dola ya Kibaniani kuhusiana na Kashmir. Hata hivyo, usaliti huu dhidi ya Waislamu wanaodhulumiwa na wanyonge wa Kashmir uliendelea hata zaidi ya hapo.

Soma zaidi...

Mahusiano ya Kigeni ni Jukumu la Dola Pekee, kwa kuwa Dola Pekee ndiyo iliyo na Haki ya Kuchunga Mambo ya Ummah Kivitendo

Baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kuwa wajumbe kutoka Muungano wa Vyama na Mavuguvugu ya Sudan Mashariki, wakiongozwa na Sheiba Dirar na kuandamana na kundi la watu mashuhuri, walikutana na Rais wa Eritrea Isaias Afwerki mnamo Jumamosi, 2 Agosti 2025, afisini kwake huko Adi Halo, ambapo wajumbe hao walijadiliana naye hali ya sasa ya Sudan kwa jumla, kwa kuzingatia changamoto zinazoikabili Sudan Mashariki. Ujumbe huo pia ulisisitiza umuhimu wa uratibu na nchi jirani ili kusaidia utulivu wa nchi na kukabiliana na migogoro ya kisiasa na usalama.

Soma zaidi...

Mbele ya Serikali za Khiyana, Msikiti wa Al-Aqsa Unabadilishwa Kuwa Mahali Patakatifu kwa Mayahudi!!

Mbele ya macho ya watawala wa Waislamu, Mayahudi wamekuwa wakivamia eneo la Msikiti wa Al-Aqsa, uvamizi baada ya uvamizi, ambao wa hivi karibuni ulikuwa wa jana, Jumapili, ukiongozwa na adui wa Mwenyezi Mungu, Ben-Gvir na idadi kadhaa ya Mayahudi wenye itikadi kali, katika uvamizi mkubwa zaidi kuwahi kutokea katika msikiti huo.

Soma zaidi...

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Chazindua Kampeni ya Kimataifa “Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”

Mgogoro wa kikatili nchini Sudan kati ya Wanajeshi wa Sudan (SAF) wanaoongozwa na mtawala mkuu wa Sudan, Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) kinachoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (Hemedti), ambaye hapo awali alikuwa naibu wa al-Burhan katika Baraza Kuu, sasa umeingia mwaka wake wa tatu, na kusababisha vifo vya maelfu ya raia. Baadhi ya makadirio yanaweka idadi ya waliofariki katika vita hivi vya kipumbavu kufikia 150,000, huku kukiwa na ukatili wa kutisha uliofanywa na pande zote mbili, ikiwa ni pamoja na mauaji ya kinyama, mateso, ubakaji mkubwa na uhalifu mwingine wa kingono dhidi ya wanawake na wasichana. Mauaji ya kikabila pia yameripotiwa, huku jamii nzima zikiteketezwa kwa moto na kuangamizwa, na mauaji ya halaiki katika miji mbalimbali, vijiji na kambi za watu waliokimbia makaazi yao.

Soma zaidi...

Sio Taarifa ya Bogotá wala Tangazo la New York litaweza kuliokoa umbile la Kiyahudi!

Wakati sera ya mauaji ya halaiki na njaa huko Gaza ikiendelea huku ukatili wake wote ukionekana na kusikilizwa na dunia nzima, Uturuki vile vile, inaendelea na hatua zake rasmi za kukabiliana na ongezeko la misimamo ya rai jumla nchini Uturuki. Hata hivyo, haikutia saini taarifa iliyotayarishwa na The Hague Group huko Bogotá, mji mkuu wa Colombia, Julai 15–16. Lakini katika kujibu majibu hayo, Wizara ya Mambo ya Nje ilidai kuwa taarifa hiyo huenda ikatiwa saini hadi Septemba 20, na Waziri wa Mambo ya Nje Hakan Fidan alitangaza kuwa wana dukuduku katika muktadha wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Sheria ya Bahari.

Soma zaidi...

Ayman Safadi: “Yeyote ambaye ana badali ya Suluhisho la dola mbili, basi na aiwasilishe!” Hizb ut Tahrir imewasilisha na inaendelea kuwasilisha suluhisho halali na la kivitendo

Serikali ya Jordan ndio iliyowawekea watu wa Jordan na Umma wa Kiislamu suluhisho linaloendana na kuhifadhi usalama wa umbile katili la Kiyahudi. Hukuwa na maregeleo ya masuluhisho ya kadhia ya Palestina isipokuwa Marekani, rafiki wa serikali hii, mshirika wa umbile la Kiyahudi, mdhamini wake, mlinzi wake, na mshirika wake katika vita vya maangamizi na njaa dhidi ya watu wa Gaza.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yaandaa Kisimamo Mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan cha Kuinusuru Gaza

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan imeandaa kisimamo mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan leo, Ijumaa, 7 Safar 1447 H sawia na tarehe 1 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa. Wanachama wa Hizb waliinua mabango yenye alama ishara: “Angusheni viti vya utawala vinavyozuia kusonga kwa majeshi kuinusuru Gaza.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu