Jumatatu, 16 Muharram 1446 | 2024/07/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Jordan

H.  20 Rabi' II 1444 Na: 1444 / 09
M.  Jumatatu, 14 Novemba 2022

 Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Mkataba wa Maelewano (MoU) wa Umeme kwa Maji ni Mwezeshaji Waziwazi wa umbile la Kiyahudi

Kwa Gharama ya Watu wa Jordan na Ummah na Dhidi ya Chaguo lake la Kuikomboa Palestina
(Imetafsiriwa)

Mnamo tarehe 8/11/2022, juu ya kadhia za ziada za Mkutano wa Kilele wa Tabianchi huko Sharm El-Sheikh, Jordan, Imarati na umbile la Kiyahudi zilitia saini mkataba wa maelewano (MoU) ili kuendeleza upembuzi yakinifu na "kushiriki katika kutengeneza ala muhimu katika zilizopangwa kwa wakati kwa ajili ya mkutano wa COP28” utakaofanyika Imarati mnamo Novemba 2023, kuanzisha miradi miwili tofauti, inayotegemeana na kuhusiana; kwa lengo la kuasisi kiwanda cha kusafisha maji katika Bahari ya Mediterania kwa badali ya kuanzishwa kwa kiwanda cha kuazalisha umeme safi nchini Jordan. Kutiwa saini kwa mkataba huo kumetokana na tangazo la nia lililotiwa saini na pande hizo tatu katika kadhia za ziada za Maonesho ya Dubai mwaka jana, mbele ya uwepo na upatanishi wa Mjumbe wa Rais wa Marekani John Kerry.

Miongoni mwa masharti ya mkataba wa makubaliano (MoU) na tangazo la awali la kusudio ni yafuatayo:

1- Jordan itajenga uwanja maalum kwa nishati ya jua na usafirishaji wa megawati 600 za umeme kwa umbile la Kiyahudi, pamoja na kuhifadhi nishati ya jua kwa kiwango kikubwa cha gigawati 3 kwenye eneo la Jordan kwa matumizi ya umbile la Kiyahudi.

2- Umbile la Kiyahudi litachunguza uwezekano wa kusafirisha mita za ujazo milioni 200 za maji hadi Jordan, ambayo yatatoka kwenye kiwanda maalum cha kuondoa chumvi. Yatauzwa kwa Jordan kwa bei ya sasa, sio bei ya upendeleo.

3- Imarati inafadhili na kujenga shamba la nishati ya jua katika ardhi ya Jordan, na umbile la Kiyahudi litalipa dolari milioni 180 kila mwaka kwa badali yake, kugawanywa kati ya Jordan na Imarati.

Kuhusu kutiwa saini kwa mkataba huu na adui mnyakuzi, umbile la Kiyahudi, tunasema yafuatayo:

1- Tovuti ya Axios iliyataja makubaliano haya kama “mradi mkubwa zaidi wa ushirikiano wa kikanda kuwahi kutokea kati ya 'Israel' na majirani zake”, ambao uliwezekana kutokana na Mkataba wa Wadi Araba na mikataba ya Abraham ya khiyana na uhalalishaji mahusiano. Hakuna nafasi ya kukanusha kwamba tawala hizi zinaweka maslahi ya umbile hili nyakuzi na kulipa uwezo kama mkakati wa kisiasa unaohujumu maslahi ya watu wake, kuwasaliti hadi kwenye shina, na kuidunisha dini yao.

2- Licha ya uhalalisha wa kirongo na wa kupotosha wa kunadi mikataba hii kwa watu, kwa upembuzi wao yakinifu wa kiuchumi au mahitaji ya dharura ya Jordan kwao, kama vile madai ya umaskini na uhaba wa rasilimali za maji, makubaliano haya ni ya kisiasa kikamilifu, lengo lake ni kulioanisha umbile hili nyakuzi ndani ya eneo hilo, na watu wa Jordan kwa ujumla wanakataa makubaliano haya na wameonyesha hasira yao na kukataa kwao, na wanalichukulia umbile la Kiyahudi kuwa adui wa kwanza kwao, na Amerika na Ulaya nyuma yake. Hawaoni suluhu yoyote ya kuamiliana nalo isipokuwa kwa njia ya jihad, kama ilivyo onyeshwa na kura za maoni rasmi za nchini mwezi mmoja uliopita.

3- Imarati, ambayo ni mshirika imara zaidi wa Ghuba wa Jordan, ingeweza kujenga kiwanda cha kusafisha maji katika Ghuba ya Akaba ambayo ingeweza kuipatia Jordan mara mbili ya kile ambacho umbile la Kiyahudi inakusudia kuiuzia Jordan. Kituo cha kuondoa chumvi kwenye ardhi iliyonyakuliwa ya Palestina kinawafanya watu wa Jordan wawe chini ya udhibiti na usaliti wa umbile la Kiyahudi, ambalo haliheshimu jamaa, makubaliano au ahadi na watu, lakini ni mradi wa dola za kikoloni kulipa tamkini umbile la Kiyahudi. Mwenyezi Mungu (swt) asema:

(Au wana sehemu ya ufalme, kisha hawawapi watu sehemu moja) “Au wana sehemu ya ufalme? Basi [kama ingekuwa hivyo] wasingewapa watu hata chembe ya tende” [An-Nisaa: 53]. 4- Kujenga shamba la miale ya jua kwenye ardhi ya Jordani linalotumia maeneo makubwa ya ardhi tambarare, ambayo jumuiya ya Kiyahudi haina. Ni ukaliaji kivitendo wa ardhi ya Jordani na ukiukaji wa enzi yake kwa ridhaa yake na kwa bei nafuu kwa niaba ya Jumuiya ya Kiyahudi, kutokana na nishati safi, na huiondoa kutoka kwa gharama ya ulinzi wa usalama kwa mradi kama huo na gharama ya mradi kama huo. , operesheni yake ya kila mwaka, ikiwa ilifanywa kwenye ardhi zilizokaliwa ambazo shirika la Kiyahudi hufunga kwa miradi ya kijani kibichi na maji. 5- Licha ya sababu za kupotosha na kusitasita kutumia miradi ya nishati mbadala, Waziri wa Nishati na Madini wa Jordan alisema kuwa uwezo wa jumla wa miradi ya kuzalisha umeme kutoka vyanzo vya nishati mbadala ulifikia takriban megawati 2526 mwishoni mwa Julai iliyopita, na kuchangia kuhusu 29% ya nishati ya umeme iliyozalishwa tangu mwanzo wa 2022, ambayo inaonyesha kwamba hakuna haja ya mradi wa nishati safi na chombo cha Kiyahudi, isipokuwa sera ya kuwasilisha.

(أَمْ لَهُمْ نَصِيبٌ مِّنَ الْمُلْكِ فَإِذاً لَّا يُؤْتُونَ النَّاسَ نَقِيراً)

 “Au wanayo sehemu ya utawala? Basi hapo wasingewapa watu hata tundu ya kokwa ya tende.” [An-Nisa: 53].

4- Kujenga shamba la miale ya jua kwenye ardhi za Jordan linalotumia maeneo makubwa ya ardhi tambarare, ambayo umbile la Kiyahudi halina. Ni ukaliaji wa kivitendo wa ardhi za Jordan na ukiukaji wa ubwana wake kwa ridhaa yake na kwa gharama nafuu kwa niaba ya umbile la Kiyahudi, kutokana na nishati safi, na huliondolea gharama ya ulinzi wa usalama kwa mradi kama huo na gharama ya mradi kama huo, operesheni yake ya kila mwaka, lau ungefanywa kwenye ardhi zilizokaliwa kimabavu ambazo umbile la Kiyahudi imezifunga kwa ajili ya miradi ya kijani kibichi na maji.

5- Licha ya sababu za kupotosha na kusitasita kutumia miradi ya nishati mbadala, Waziri wa Nishati na Madini wa Jordan alisema kuwa uwezo wa jumla wa miradi ya kuzalisha umeme kutoka vyanzo vya nishati mbadala ulifikia takriban megawati 2526 mwishoni mwa Julai iliyopita, na kuchangia takriban 29% ya nishati ya umeme iliyozalishwa tangu mwanzo wa 2022, ambayo inaonyesha kwamba hakuna haja ya mradi wa nishati safi na umbile la Kiyahudi, isipokuwa tu sera ya kujisalimisha.

6- Mkataba huo hauhusiani kamwe na kupunguza utoaji wa hewa carbon na kongamano la tabianchi, hata kama utakuja katika muktadha wake na chini ya shinikizo kutoka kwa John Kerry, Mjumbe wa Rais wa Marekani wa Tabianchi. Bali, ni uhalalishaji wa kuingia kwa umbile la Kiyahudi katika mfumo wa nchi za Kiislamu na unyonyaji wa rasilimali zao chini ya tawala zinazodumisha uhai wao katika utekelezaji maagizo ya Marekani na Uingereza.

7- Kadhia ni kuwa umbile la Kiyahudi ni mnyakuzi na mkaliaji kimabavu na ni adui wa Ummah mzima wa Kiislamu, na kipimo cha kivitendo kuelekea kwake ni kulichukulia kuwa ni adui na kutolitambua au kulipa nguvu na kusawazisha mahusiano nalo kupitia makubaliano ya kiuchumi, usalama na makubaliano mengine. Utaratibu wa kisheria ambao Ummah unawajibika kuufuata ni kulipiga vita na kuitakasa Palestina yote kutokana nalo.

8- Inasikitisha sana kwamba tawala za kiupofu za kiutegemezi hazioni kwamba udhalilishaji wa Mayahudi ndio hatima ya yule anayeegemeza utawala wake juu ya nchi za kikoloni za makafiri za Kimagharibi, na kutekeleza ajenda zao pamoja na umbile la Kiyahudi jukumu la watu hao ni kuwatema nje, na kwamba Ummah utaregea kwenye mradi wake na msimamo wake, msimamo wa izza na heshima mbele ya umbile hili lenye kiburi na chuki. Mwenyezi Mungu (swt) asema:

(لَا تَجِدُ قَوْماً يُؤْمِنُونَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ يُوَادُّونَ مَنْ حَادَّ اللَّهَ وَرَسُولَهُ)

“Huwakuti watu wanao muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho kuwa wanawapenda wanao mpinga Mwenyezi Mungu na Mtume wake.” [Al-Mujadila: 22].

Enyi watu wetu wa Jordan, enyi Waislamu!

Haitoshi kuonyesha kukataa kwenu na hasira kwa makubaliano haya ya khiyana. Suluhu hazitokani na kuweka viraka uhalisia wa kudhalilisha kupitia kufanya makubaliano hapa au pale. Pia, masuluhisho ya masuala ya Ummah, likiwemo suala la Palestina, hayatatuliwi kwa mujibu wa sheria za kimataifa na kwa mujibu wa uhalali wa dhulma na wa kishetani wa kimataifa. Bali, suluhisho msingi ni suluhisho ambalo Mwenyezi Mungu (swt) aliamuru. Ni kukombolewa kwa ardhi ya Palestina kutoka kwa makucha ya Mayahudi kwa nguvu inayomilikiwa na majeshi ya Ummah, ambayo haitahamishwa isipokuwa kwa Ummah kurudi kwenye kuunganishwa kwake chini ya Dola ya Khilafah Rashida kwa njia ya utume. Ndio mradi wake wa kimataifa wa kurudisha haki, uadilifu na rehma kwa Umma wa Kiislamu na ulimwengu kwa jumla, baada ya ukandamizaji na ukatili wa dola za kikoloni za makafiri kuenea na kuathiri wanadamu wote.

(إِنَّمَا يَنْهَاكُمُ اللَّهُ عَنِ الَّذِينَ قَاتَلُوكُمْ فِي الدِّينِ وَأَخْرَجُوكُم مِّن دِيَارِكُمْ وَظَاهَرُوا عَلَى إِخْرَاجِكُمْ أَن تَوَلَّوْهُمْ وَمَن يَتَوَلَّهُمْ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ)

“Hakika Mwenyezi Mungu anakukatazeni kufanya urafiki na wale walio kupigeni vita, na wakakutoeni makwenu, na wakasaidia katika kufukuzwa kwenu. Na wanao wafanya hao marafiki basi hao ndio madhaalimu.” [Al-Mumtahina: 9]

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Jordan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Jordan
Address & Website
Tel: 
http://www.hizb-jordan.org/
E-Mail: [email protected]

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu