Jumatatu, 25 Rabi' al-thani 1446 | 2024/10/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Jordan

H.  7 Rabi' II 1446 Na: 1446 / 03
M.  Alhamisi, 10 Oktoba 2024

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi

مِّنَ الْمُؤْمِنِينَ رِجَالٌ صَدَقُواْ مَا عَاهَدُواْ اللهَ عَلَيْهِ فَمِنْهُم مَّن قَضَى نَحْبَهُ

وَمِنْهُم مَّن يَنتَظِرُ وَمَا بَدَّلُواْ تَبْدِيلاً

“Miongoni mwa Waumini wapo watu walio timiza waliyo ahidiana na Mwenyezi Mungu. Baadhi yao wamekwisha kufa, na baadhi wanangojea, wala hawakubadilisha (ahadi) hata kidogo.” [Ahzab: 23]


 Kalima ya ujumbe wa Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Jordan Katika mazishi ya Hajj Youssef Mustafa Al-Toubasi (Abu Osama)

Imetolewa kwa niaba ya ujumbe huo na Ustadh Bilal Al-Qasrawi



Kutokana na imani kwa Qadhaa ya Mwenyezi Mungu, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Jordan inamuomboleza:

Hajj Youssef Mustafa Al-Toubasi (Abu Osama)

Aliyefariki dunia kwenda kwenye rehema za Mwenyezi Mungu leo, Alhamisi, 10/10/2024. Yeye ni mmoja wa mashababu wa kizazi cha kwanza cha Hizb ut Tahrir, ambapo alijiunga na kubeba ulinganizi huu katika safu za Hizb ut Tahrir katika miaka ya hamsini ya karne iliyopita, baada ya maisha yaliyojaa kazi ya kuanzisha tena maisha kamili ya Kiislamu na kutekeleza sheria ya Mwenyezi Mungu.

Uzee wake, maradhi, mateso, na kufungwa jela mara tatu mikononi mwa madhalimu havikumzuia kuendelea na shughuli yake na mapambano, subira na kutafuta malipo, kwani alitumia maisha yake kubeba ulinganizi wa Uislamu na kufanya kazi ya kusimamisha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, mpaka alipofariki. Tunamuomba Mwenyezi Mungu amghufirie maiti wetu, na ampe makaazi mahala pema katika Pepo Yake pamoja na Manabii, na wakweli, na mashahidi na watu wema na hao ndio marafiki wema.

Mwenyezi Mungu amrehemu maiti wetu na ampe makaazi mema katika Pepo Yake awape ujira mkubwa familia yake na jamaa zake na awape subira na faraja, na hatusemi isipokuwa yale tu yanayomridhisha Mwenyezi Mungu (swt), ni cha Mwenyezi Mungu alichotoa, na ni cha Mwenyezi Mungu alichochukua na kila kitu Kwake kina Qadar.

﴿إِنَّا للهِ وَإِنَّا إِلَيْهِ رَاجِعُونَ

Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye hakika tutarejea.” [Baqara: 156]

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir

katika Wilayah Jordan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Jordan
Address & Website
Tel: 
http://www.hizb-jordan.org/
E-Mail: info@hizb-jordan.org

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu