Jumatatu, 16 Muharram 1446 | 2024/07/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Kenya

H.  6 Rabi' II 1444 Na: 1444/03 H
M.  Jumatatu, 31 Oktoba 2022

 Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Ubepari ni Laana kwa Wanadamu wala sio Neema

(Imetafsiriwa)

Huku Kenya ikigubikwa na mrundiko wa deni la jumla ya Sh.10 trilioni, Rais William Ruto awataka wakenya wawe wakilipa ushuru vilivyo. Kulingana na rais serikali inanuia kukusanya Sh.2 trillioni kwa mwaka ujao. Rais amewataka raia wawe na tabia ya kulipa ushuru ipasavyo ili kusaidia serikali kulipa deni lake na kuikomboa kutokana na zigo hili. Kwa sasa Serikali inatumia Sh.1 trilioni kulipia mikopo.

Hizb ut-Tahrir Kenya ingependa kubaini yafuatayo:

Deni la kitaifa lililokopwa kutoka mashirika ya kifedha ya kimataifa linazidi kuongezeka kila mwaka. Kenya inahitaji kwa sasa kukopa kitita cha Sh.900 bilioni kugharamikia mahitaji yake ya kifedha hatua ambayo ni suluhisho la muda ambalo kiuhalisia wake litaletea nchi masharti magumu yatakayodhalilisha zaidi na kujipata kwenye madeni zaidi hali itakayopelekea nchi kufilisika na hatimaye kujihatarisha zaidi. Ni bayana kwamba sera kandamizi zinazochukuliwa na serikali kutoka kwa shirika la IMF na Benki ya Dunia hubebesha raia mzigo mzito wa kiuchumi.

Chanzo muhimu cha kukusanya mapato ya serikali ndani ya Ubepari ni utozaji ushuru na ukopaji. Kulipisha ushuru matumizi na mapato ndio hufanya raia wa kawaida kulemewa katika harakati zao za kiuchumi siku baada ya siku kwani haya ndiyo mahitaji muhimu kwa maisha ya kila siku. Kama zilivyo tawala za kirasilimali, Kenya inafuata kile kiitwacho mfumo wa utozaji ushuru uliojikita zaidi kwenye utozaji wa ushuru kwenye mapato ya wafanyikazi na wafanyibiashara. Ni wazi kwamba bajeti za kuendesha gharama za serikali ndani ya mfumo wa kibepari hutegemea pakubwa utozaji mkubwa wa ushuru huku nakisi kwenye bajeti ikisimamiwa na Mikopo na ruzuku.

Tunasema majiribio na juhudi za serikali ya sasa yatazalisha madeni na hivyo kuzalisha majanga na kuwafanya raia wazidi kuumia kiuchumi.

Uislamu ndio suluhisho pekee la kumkomboa mwanadamu kwenye masaibu haya ya kiuchumi yaliyosheheni katika mfumo wa kirasilimali, hii ni kuwa Uislamu huhakikisha kwamba mali yote ya umma hutumika katika kuwahudumikia umma. Kipengele hiki kimsingi kinaondoa kodi kama chanzo kikuu cha mapato hivyo kuacha matumizi na mapato yakisukumwa tu na nguvu za soko (mahitaji na usambazaji). Na kwa msingi huu, Dola ya Khilafah (Ukhalifa) kwa njia ya Utume ndiyo itakayo kuwa na uchumi wa kipekee utakaoweza kuwanasua wanadamu kwenye utumwa wa kiuchumi wa kikoloni wa dola za Magharibi.

Shabani Mwalimu

Mwakilishi kwa Vyombo Vya Habari wa Hizb ut Tahrir Kenya

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Kenya
Address & Website
Tel:  +254 707458907
E-Mail: [email protected]

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu