Jumatano, 04 Shawwal 1446 | 2025/04/02
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Kitengo cha Wanawake

H.  23 Ramadan 1446 Na: H 1446 / 099
M.  Jumapili, 23 Machi 2025

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Leo Gaza na Yemen, na Kesho nchi zengine za Waislamu, Isipokuwa Majeshi yao Yatangaze Kusonga
(Imetafsiriwa)

Kamandi Kuu ya Ulinzi ya Marekani (CENTCOM) ilitangaza kwamba jioni ya Jumamosi, 15 Machi 2025, ilianzisha msururu wa mashambulizi ya anga dhidi ya maeneo lengwa ya Mahouthi nchini Yemen. Ilidai kuwa ilifanya mashambulizi sahihi dhidi ya maeneo lengwa ya kundi hilo kote Yemen, ikihalalisha mashambulizi hayo kama utetezi wa maslahi ya Marekani, kuzuia dhidi ya maadui, na kuregesha uhuru wa bahari, kulingana na taarifa yake. Kufikia Alhamisi jioni, Machi 20, makumi ya mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya Yemen yalikuwa yameripotiwa, na kusababisha vifo vya watu 53 na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa, wengi wao wakiwa wanawake na watoto. Kuna matarajio kwamba operesheni zitaendelea kwa wiki kadhaa. Haya ni mashambulizi ya kwanza dhidi ya Yemen tangu makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya umbile la Kiyahudi na Hamas mjini Gaza Januari iliyopita, kufuatia kiapo cha Trump cha "kuwamaliza kabisa."

Marekani inaendesha ghasia katika ardhi zote za Waislamu, ikitishia, kuhofisha, na kuua ipendavyo, kufuatia kujisalimisha kwa watawala waoga wa Waislamu ambao wanavaa vazi la udhalilifu na fedheha. Hao ndio wanaohusika na maafa ya Ummah huu, kuuvua utu wake, kuushusha hadhi yake, na kuudunisha hadi kufikia mahali ambapo hauogopwi tena, na kupuuzwa na makafiri ambao wameutia kwenye aina mbalimbali za mateso, uhamisho, unyanyasaji, mauaji na mauaji ya halaiki.

Enyi Waislamu: Marekani inafuata sera ya ukandamizaji ili kulazimisha mipango yake juu yenu - ima kujisalimisha na kusalimu amri au uchungu wa vita na mauaji ya halaiki. Kasi ya matukio, kuongezeka kwa mateso kwa watu wetu huko Gaza, na adhabu ya Amerika kwa mtu yeyote anayetishia maslahi yake au yale ya umbile la Kiyahudi yote ni juhudi za kuasisisha fikra ya kushindwa na unyonge ili kuzuia jaribio lolote la kubadilisha uhalisia wa sasa. Kinachotokea Gaza na Yemen ni utangulizi tu wa kile ambacho kinaweza kuja kwa ardhi zenu zote ikiwa hamtaungana kwa neno moja na kuzima uvamizi huu.

Enyi Majeshi ya Waislamu: Msiba ni mkubwa sana. Hakuna utiifu kwa watawala ambao hawana uhalali; bali ni lazima wapinduliwe madarakani, na hamasisho jumla lazima litangazwe ili kuikomboa ardhi iliyobarikiwa ya Palestina na maeneo yote ya Waislamu, ili kukomesha kiburi na jinai za Marekani, umbile la Kiyahudi, na wale wote waliotangaza vita dhidi ya Waislamu, kumwaga damu zao, kukiuka matukufu yao, kuua wanawake na watoto wao, bila kuonyesha huruma kwa udhaifu wao, na kunajisi maeneo yao matakatifu.

Kuweni askari wa Mwenyezi Mungu ambao kupitia kwao Dini inadumishwa, madhara ya maadui yanaondolewa, nguvu ya Uislamu inalindwa, na utakatifu wa imani unalindwa. Jitoleeni kwa ajili ya kuliinua neno la Mwenyezi Mungu ili Dini iwe yake Yeye peke yake. Msijitie nafsi zenu katika maangamivu kwa kuachana na jihad, kwani kushindwa kusonga wakati wa haja ni miongoni mwa madhambi makubwa yanayoleta adhabu kali.

[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا مَا لَكُمْ إِذَا قِيلَ لَكُمْ انفِرُوا فِي سَبِيلِ اللهِ اثَّاقَلْتُمْ إِلَى الْأَرْضِ أَرَضِيتُمْ بِالْحَيَاةِ الدُّنْيَا مِنْ الآخِرَةِ فَمَا مَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا فِي الْآخِرَةِ إِلا قَلِيلٌ * إِلا تَنفِرُوا يُعَذِّبْكُمْ عَذَاباً أَلِيماً وَيَسْتَبْدِلْ قَوْماً غَيْرَكُمْ وَلَا تَضُرُّوهُ شَيْئاً وَاللهُ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ]

“Enyi mlio amini! Mna nini mnapo ambiwa: Nendeni katika Njia ya Mwenyezi Mungu, mnajitia uzito katika ardhi? Je, mmeridhia maisha ya dunia kuliko ya Akhera? Lakini starehe za maisha ya dunia kulinganisha na ya Akhera ni chache. (38) Kama hamwendi atakuadhibuni adhabu chungu, na atawaleta watu wengine, wala nyinyi hamtamdhuru chochote. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.” [At-Tawba:38-39].

Kitengo cha Wanawake

katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Kitengo cha Wanawake
Address & Website
Al-Mazraa Sanduku la Posta. 14-5010 Beirut- Lebanon
Tel: 00961 1 30 75 94 Mobile: 00961 71 72 40 43
www.hizb-ut-tahrir.info
Fax: Telefax
E-Mail: ws-cmo@hizb-ut-tahrir.info

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu