Jumamosi, 21 Muharram 1446 | 2024/07/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan

H.  11 Sha'aban 1443 Na: 1443 / 46
M.  Jumatatu, 14 Machi 2022

Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Kujizuia kwa Serikali ya Bajwa-Imran Mbele ya Kombora la India Lililotua kwenye Ardhi wa Pakistan, Kwasababisha Idhlali kwa Pakistan

 (Imetafsiriwa)

Kombora la India aina ya BrahMos limerushwa na India, na kugonga Mian Channu, baada ya kuvuka kilomita 124 kwenye anga ya Pakistan na kushambulia ardhi yake. Hata hivyo, katika jibu dhaifu na la kujizuia kwa uchokozi wa wazi wa India, watawala wa Pakistan walijifunga kwa maneno pekee, wakizungumzia haja ya Magharibi kuvunja ukimya wake, kuzingatia na kujilinda dhidi ya vita vya bahati mbaya. Kabla ya India inayoongozwa na BJP kuwa mshirika wa kimkakati wa Marekani, kila tofali lililorusha lilijibiwa kwa mawe, ikiwa ni pamoja na kupata uwezo wa makombora ya nyuklia, kuanzisha miundombinu yenye ufadhili wa kutosha, mafunzo na usambazaji kwa ajili ya Jihad ili kuikomboa Kashmir Inayokaliwa kwa mabavu, ilivuruga azimio la wanajeshi 900,000 wa India na kuhamasisha kuundwa kwa vuguvugu la Khalistan kwa ajili ya kuwakomboa Makalasinga. Lakini, sasa, iwe Modi aliiunganisha Kashmir Iliyokaliwa kwa nguvu au Waislamu waliokandamizwa kikatili ndani ya Kashmir Iliyokaliwa na India yenyewe, serikali ya Bajwa-Imran inajizuia kwa mujibu wa matakwa ya Biden, ili kutozuia kuinuka kwa India kama dola kuu ya eneo hilo.

Utawala katili wa Bajwa-Imran unatumia udhibiti wa kihalifu, baada ya kutia saini makubaliano ya kioga ya kusitisha mapigano juu ya Mstari wa Udhibiti, ili India iweze kushughulika kikamilifu na China, kama Biden anavyohitaji. Hii ni ingawa, baada ya kuondoka kwa Marekani kutoka Afghanistan, majeshi ya Pakistani yanaweza kuvuka Mstari wa Udhibiti kwa urahisi kuikomboa Kashmir Iliyokaliwa, hasa katika wakati ambapo kuna ongezeko la mvutano kati ya China na India na wakati ambapo dola kuu za dunia zinaingilia kati Ukraine. Badala yake, serikali ilipitisha sheria ya kutoa afueni kwa mpangaji mkuu wa kigaidi wa India Kulbhushan Yadav, kuruhusu nyambizi za Jeshi la Wanamaji la India kukiuka bahari za Pakistan mara mbili na kuruhusu kombora la hypersonic la India kukiuka anga ya Pakistan, bila kulitungua, na kushambulia ardhi ya Pakistan, bila ya mara moja kutuma uwezo wa mashambulizi ya pili, kuashiria udhaifu katika uwezo wa kuzuia nyuklia.

Uongozi wa kijeshi na kisiasa wa Pakistan umepunguza nguvu za jeshi la Kiislamu lenye nguvu zaidi duniani, zenye uwezo wa kinyuklia, kuwa shabaha ya kukaa na kuzibwa mdomo kwa vikosi vya jeshi la India. Kujizuia kwa utawala wa Bajwa-Imran kumemtia moyo Modi, huku akilinda maslahi ya Marekani, na kuifanya Pakistan kuwa dola msaidizi ndani ya muundo wa kieneo unaoongozwa na India. Kama vile Zelenskyy wa Ukraine alivyojifunza kwa kuchelewa, usalama hauko katika kuikumbatia na kuiridhisha Washington, ambayo itawaacha vibaraka wake wakiwa juu na wakavu wakati wowote wanapotumikia maslahi ya Marekani, bila kufikiria mara mbili. Usalama upo katika kuyaachilia huru majeshi ya Pakistan, kama walivyohamasishwa mnamo Februari 2019, bali kwenda mbele zaidi ya mashambulizi yaliyodhibitiwa ili kuliangamiza eneo la kurushia makombora la India na kuikomboa Kashmir Iliyokaliwa kwa ujasiri, na hatua kali.

Enyi Simba wa Vikosi vya Wanajeshi vya Pakistan! Sasa imetosha! Inatosha kwa uongozi wa kisiasa na kijeshi kujizuia, ili Modi apige risasi chungu Pakistan ili kuongeza nafasi yake ya uchaguzi, huku akiendeleza matarajio potovu ya Biden. Sasa ni kwa warithi halali wa Muhammad bin Qasim, Mahmud Ghaznavi na Ahmad Shah Abdali kuzika kiburi cha madhalimu wa India kwa nguvu za Imani yao. Umma wa Kiislamu umepatwa na uchungu wa idhlali, na hali mumefunga na wajibu wenu kwa Mwenyezi Mungu (swt) na Mtume Wake (saw) kumshambulia adui na kuziponya nyoyo za Waumini. Ama kwa uongozi wa sasa wa kisiasa na kijeshi, waokoeni Waislamu kutokana na vibaraka waoga wa Biden kwa kutoa Nussrah yenu kwa Hizb ut Tahrir kwa ajili ya kusimamisha tena Khilafah kwa Njia ya Utume. Ni chini ya uongozi wa kisiasa na kijeshi wa Khalifah Rashid  ndipo mtaondoa uadui wa India kupitia kuikomboa Kashmir Iliyokaliwa kimabavu, kama hatua ya kwanza ya kuregesha utawala wa Uislamu ndani ya Bara Hindi, katika wakati ambapo India inatikiswa na China, India imegawanyika vibaya kwa siasa za Modi za ubaguzi na wasaidizi wa Magharibi wa India wameingia katika mgogoro wa Ukraine. Mwenyezi Mungu (swt) amesema:

 (وَمَن يَتَوَلَّ اللَّهَ وَرَسُولَهُ وَالَّذِينَ آمَنُوا فَإِنَّ حِزْبَ اللَّهِ هُمُ الْغَالِبُونَ)

“Na atakaye fanya urafiki na Mwenyezi Mungu na Mtume wake na walio amini, basi hakika kundi la Mwenyezi Mungu ndilo lenye kushinda.” [Surah al-Maida 5:56].

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Pakistan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan
Address & Website
Tel: 
https://bit.ly/3hNz70q

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu