Jumamosi, 21 Muharram 1446 | 2024/07/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Sudan

H.  29 Shawwal 1445 Na: HTS 1445 / 40
M.  Jumatano, 08 Mei 2024

Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Hizb ut Tahrir Inatoa Salamu za Rambirambi kwa Kuondokewa na Mkurugenzi wa Radio Biladi
(Imetafsiriwa)

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Ustadh Muntasir Karrar, Mratibu wa Kamati ya Ushirikiano wa Amali huko Gadharef, akiandamana na Ustadh Ibrahim Musharraf, Mjumbe wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, na Ustadh Abdullah Ismail, Mwanachama wa Hizb ut Tahrir, alitekeleza jukumu la kutoa rambimbi kwa marehemu mwandishi wa habari, Ustadh Abboud Saif Al-Din, Mkurugenzi wa Radio Biladi. Ujumbe huo ulitembelea familia ya marehemu nyumbani kwao Port Sudan na kuwapa pole mnamo siku ya Jumapili, tarehe 26 Shawwal 1445 H, sawia na 5/5/2024 M.

Ujumbe huo pia ulikutana na baadhi ya maafisa, wanahabari wa chaneli za satelaiti, ndugu katika vyombo vya habari na wafanyikazi wenza wa marehemu.

[إِنَّا للهِ وَإِنَّا إِلَيْهِ رَاجِعُونَ]

“Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye hakika tutarejea.” [Al-Baqara: 156]

Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Sudan

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Sudan
Address & Website
Tel: 

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu