Afisi ya Habari
Wilayah Sudan
| H. 17 Rajab 1447 | Na: HTS 1447 / 76 |
| M. Jumanne, 06 Januari 2026 |
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Kuhutubia Umma katika Mji wa Al-Ubayyid kama Sehemu ya Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah
(Imetafsiriwa)
Wanachama wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan katika mji wa Al-Ubayyid walitoa hotuba ya hadhara mnamo siku ya Ijumaa, 13 Rajab 1447 H, sawia na 2 Januari 2026 M, kufuatia swala ya Ijumaa katika Msikiti wa Soko la Karima Kaskazini. Ustadh Ahmed Wada’a Abdul Karim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, alizungumza, akielezea kwamba hakuna heshima au usalama isipokuwa chini ya Khilafah. Kisha akahutubia ujumbe kwa wale walio katika nyadhifa za mamlaka na ushawishi, wasomi, wanasiasa, na wanahabari, akiwahimiza kusimama na kufanya kazi ili kusimamisha Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume.
Waliohudhuria waliitikia vyema amali na hotuba hiyo, wakiisifu Hizb, na hata baadhi ya video zilizorekodiwa na kupigwa picha.
Hotuba hiyo ilipokelewa vyema sana, Alhamdulillah Rabi Al-alamin.
Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Sudan
| Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari Wilayah Sudan |
Address & Website Tel: 0912240143- 0912377707 http://www.hizb-sudan.org/ |
E-Mail: Spokman_sd@dbzmail.com |



