Jumatano, 16 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/08
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Kuinusuru Gaza, ni Wito wa Umoja kwa Watawala: “Miaka miwili imepita! Hatungojei Maneno, bali Vitendo!”

Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili (mauaji ya halaiki) ambayo yamekuwa yakiendelea kwa miaka miwili kamili, yanayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza, ambayo hadi sasa yamesababisha kuuwawa shahidi, kujeruhiwa, na kupoteza zaidi ya wanaume na wanawake wa Kiislamu 240,000, Hizb utTahrir/Wilayah Uturuki, iliandaa matembezi makubwa ya halaiki katika mji mkuu wa Ankara na katika mji wa Istanbul na mji wa Şanlıurfa, yenye kichwa: Wito wa Umoja kutoka Viwanjani kwa ajili ya Gaza katika Mwaka Wake wa Pili: “Wito wa Umoja kwa Watawala: Miaka Miwili Imepita! Hatungojei Maneno, Bali Vitendo!”

Soma zaidi...

Trump, Msaidizi Mkuu wa Umbile la Kiyahudi katika Uhalifu wake wa Kinyama mjini Gaza na Palestina Yote, Anatoa Suluhisho la Maangamivu kwa Gaza, Hata Kulilazimisha, Juu ya Kundi la Watawala katika Nchi za Waislamu!!

Trump alisema katika chapisho kwenye jukwaa lake la Kijamii la Ukweli: “Ninafuraha kuripoti kwamba tuna mazungumzo yenye msukumo na yenye natija na Jumuiya ya Mashariki ya Kati kuhusu Gaza,” na kuongeza kuwa, “mazungumzo makali yamekuwa yakiendelea kwa siku nne, na yataendelea kwa muda mrefu iwezekanavyo ili kupata Makubaliano Yanayokamilishwa kwa Mafanikio.” (Truth Social; TRT Kiarabu, 27/9/2025)

Soma zaidi...

Al-Waqiyah TV: Khilafah Pekee Ndio Itakayoiletea Sudan Izza!

Sudan kwa sasa iko katikati ya vita vya kipumbavu ambavyo vimesababisha vifo vya makumi ya maelfu ya raia na kuzua mgogoro mkubwa zaidi duniani wa njaa na kuhama makaazi. Wananchi wa Sudan wamekumbwa na mizozo mbalimbali pamoja na umaskini mkubwa, udikteta, migawanyiko ya kikabila na kitabaka na matatizo mengine mengi ya kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa miongo kadhaa chini ya uongozi, tawala na mifumo mtawalia.

Soma zaidi...

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayat Sudan kukwamisha mpango wa kutenganisha Darfur, Hizb ilifanya Visimamo katika miji kadhaa ya Sudan

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayat Sudan kukwamisha mpango wa Marekani wa kuichana nchi hii kwa kuitenganisha Darfur na Sudan, hizb ilifanya kisimamo katika Msikiti wa Al-Aqit mjini Gadharef mnamo siku ya Alhamisi, Septemba 11, 2025 baada ya swala ya Ijumaa Septemba 12, 2025, miji kadhaa mikubwa ya Sudan ilifanyika visimamo, pamoja na misikiti mikuu ya Sudan yote. Shawak, Singa, Rabak, Madani, Abbasiya, Taqli, Khartoum (Kalakila na Dukhainat), na misikiti miwili mjini Omdurman.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Sudan Wilayah – Mji wa Kosti, Jimbo la White Nile Wakutana na Dkt. Muhammad al-Haitham, Katibu Mkuu wa chama cha National Unionist Party katika Jimbo la White Nile

Mnamo Ijumaa, 12 Septemba 2025, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilaya ya Sudan ulimtembelea Dkt. Muhammad al-Haitham, Katibu Mkuu wa chama cha National Unionist Party, katika Uwanja wa Azraq Taiba huko Kosti.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Kisimamo cha Port Sudan cha Kutibua Mpango wa Kujitenga kwa Darfur!

Kujibu kwa takbira, tahlil, na uungaji mkono, pamoja na vyombo vya habari na uhamasishaji wa kisiasa, kisimamo kilifanywa na Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan kutibua mpango wa kujitenga kwa Darfur kilifanyika mbele ya Msikiti Mkuu mjini Port Sudan. Waumini walikusanyika baada ya swala ya Ijumaa, 20 Rabi' al-Awwal 1447 H - 12 Septemba 2025 M, kwenye Msikiti Mkuu mjini Port Sudan kwa ajili ya kisimamo hicho ikiwa ni sehemu ya kampeni ya hizb kutibua mpango wa kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu