Jumamosi, 21 Muharram 1446 | 2024/07/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia:

Matembezi ya Ukombozi… Kunusuru Watu wa Palestina na Al-Aqsa iliyotekwa Nyara

Kwa kuzingatia matendo ya kishujaa yaliyofanywa na Mujahidina mashujaa katika Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina) chini ya kauli mbiu ya (Kimbunga cha Al-Aqsa) dhidi ya umbile la nyakuzi Kiyahudi, ambalo linaendelea na hujuma yake dhidi ya Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa na uzingiraji na ulipuaji wake mabomu wa kuendelea wa Ukanda wa Gaza kwa miaka 17, Hizb ut-Tahrir/Wilaya ya Tunisia inatoa wito kwa wote wenye ghera katika nchi ya Zaitouna na Kairouan kushiriki katika “matembezi ya ukombozi... kunusuru watu wa Palestina na Al-Aqsa iliyotekwa.”

Hili litafanyika mnamo Ijumaa, 13 Oktoba 2023 M, baada ya swala ya Ijumaa (1:00 pm.), kuanzia Msikiti wa Al-Fath katika mji mkuu na kuelekea hadi Barabara ya Al-Thawra.

Kuwanusuru na kuwaombea nusra Waislamu katika Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina) na kutoa wito kwa majeshi ya Kiislamu kuvunja minyororo ambayo watawala Ruwaibidah wamewafunga kwayo ndani ya kambi zao ili wataharaki mara moja ili kukinusuru (Kimbunga cha Al-Aqsa) na kuukomboa Msikiti wa Aqsa kutoka kwenye makucha ya Mayahudi wavamizi.

Basi kuweni pamoja nasi leo na mshiriki nasi katika ujira, na Mwenyezi Mungu atatunusuru, hata kama ni baada ya muda.

Jumanne, 25 Rabi’ al-Awwal 1445 H - 10 Oktoba 2023 M

- Ualishi wa Video wa Matembezi -

- Alama Ishara za Amali hii -

#الجيوش_إلى_الأقصى

#OrdularAksaya

#ArmiesToAqsa

Kwa maelezo zaidi tafadhali zuru mitandao ya Hizb ut tahrir / Wilayah Tunisia:

Tovuti Rasmi ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia

Ukurasa wa Facebook wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu