Jumanne, 27 Shawwal 1447 | 2026/04/14
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

“Amali” kama Pazia la Ukaliaji wa Kimabavu

Yale yanayoitwa makubaliano kati ya dola vamizi “Israel” na Hamas, yaliyopangwa na Washington, yanawasilishwa katika vyombo vya habari vya Magharibi na kwa masikitiko pia katika sehemu za ulimwengu wa Kiislamu kama hatua kuelekea amani. Kiulisia, si kitu chengine ila ni marudio ya mtindo wa zamani: mradi wa kikoloni “Israel” unaimarishwa na kulindwa zaidi, huku jinai zake zikifinikwa na vazi la “amani.”

Maafa Mawili Yanaukumba Ummah wa Kiislamu – Watawala Wafisadi na Mfumo Fisadi – Yote Lazima Yabadilishwe kwa Wakati Mmoja

Mnamo 26 Julai 2025, jiji la Kuala Lumpur lilishuhudia maandamano ya ajabu ya umma — maandamano makubwa ya kudai kujiuzulu kwa Waziri Mkuu wa Malaysia, Datuk Seri Anwar Ibrahim. Mkutano huu ulionyesha hasira kubwa na kuchanganyikiwa kwa watu kuelekea uongozi ambao haujashindwa tu kutekeleza ahadi zake za mageuzi, lakini pia umezidisha ugumu wa watu kupitia nyongeza za kodi, ongezeko la ushuru wa umeme, na kupanda kwa bei za bidhaa muhimu.

Kumwalika Adui wa Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, na Waumini Ni Sawa na Kualika Ghadhabu ya Mwenyezi Mungu na Msiba: Mche Mwenyezi Mungu, Ewe Waziri Mkuu wa Malaysia!

Hizb ut Tahrir / Malaysia inalaani vikali mwaliko uliotolewa na Waziri Mkuu wa Malaysia, Dato’ Seri Anwar Ibrahim, kwa Rais wa Marekani, Donald Trump — ambaye mikono yake imejaa damu ya Waislamu wa Gaza — kuja nchini Malaysia kuhudhuria Mkutano wa 47 wa ASEAN jijini Kuala Lumpur. Mwaliko huu si tu ishara ya aibu ya kidiplomasia isiyo na msimamo wa kimaadili; ni aibu kubwa kwa hadhi ya Ummah huu, usaliti unaojeruhi dhamiri ya kila Muislamu ambaye bado ana heshima karibu na moyo wake, hasa zaidi watu wa Palestina.

Watawala wa Pakistan, Watu wa Trump, Wawateka nyara Mashababu wa Hizb ut Tahrir ili Kuhakikisha Kujisalimisha kwa Palestina

“Jenerali kipenzi cha Trump,” Asim Munir, amejibu kwa udhalimu kampeni yenye nguvu ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Pakistan, ambayo kwayo inataka uhamasishwaji wa haraka wa Vikosi vya Jeshi la Pakistan ili kuikomboa Palestina. Majambazi wa Asim Munir wamewateka nyara matetezi watano, kutoka Lahore, Karachi na Peshawar, na mahali walipo hapajulikani. Udhalimu wa Asim Munir unatarajiwa. Asim Munir hawezi kutenda, sembuse kufikiria, nje ya maagizo ya Trump katika suala lolote, iwe kuhusu Gaza, Kashmir, Afghanistan au rasilimali kubwa za madini za Pakistan.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu