Alhamisi, 11 Dhu al-Hijjah 1447 | 2026/05/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Silsila ya Maswali Yaliyowasilishwa kwa

Amiri wa Hizb ut Tahrir

Sheikh Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah katika Ukurasa Wake wa Kifikra wa Facebook
Jibu la Swali

Kutafuta Nusra kutoka kwa Watawala wa Waislamu wa Zama Hizi

Kwa: Saadi Dheeb Awad

(Imetafsiriwa)

Swali:

Assalamu alaikum wa Rahmatullah wa Barakatahu. Namuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu kwamba ujumbe wangu utakufikia ukiwa na afya njema zaidi. Swali langu, ewe Sheikh muheshimiwa, ni hili:  

Hii ni Hadith sahih iliyopokewa na Masheikh wawili (Bukhari na Muslim) kutoka kwa Mtume (saw) yenye lafudhi: وَإِنَّ اللَّهَ لَيُؤَيِّدُ هَذَا الدِّينَ بِالرَّجُلِ الْفَاجِرِ  “Hakika, Mwenyezi Mungu huenda akaipa nguvu dini hii hata kupitia mtu muovu.

Kwa kuwa watawala wetu ni waovu, kwa nini wametengwa na ombi la nusra wakati hadith inasema waziwazi kwamba wanaweza kuinusuru dini hii?

Kwa kuzingatia hali ya sasa, na huku nikikubali kwamba majeshi ndiyo chanzo cha nguvu na ulinzi zama hizi, naamini kwamba kumwambia mtawala na kupokea jibu lake ni rahisi kuliko kuyaambia majeshi yaliyo chini ya utiifu wa amri za mtawala, kuua, kuchinja, na kuwaangamiza watu. Tunachokiona ni ushahidi wa hili.

Makabila ya Aws na Khazraj yaliunga mkono vipi jambo hili? Je, ilikuwa kupitia watu binafsi na mashujaa wa kabila, au kupitia viongozi wa makabila hayo mawili?

Ninaomba ufafanuzi, pamoja na dalili husika ya kisheria ya Kiislamu ikiwezekana.

Jibu:

Wa Assalamu alaikum wa Rahmatullah wa Barakatahu,

1- Kuhusiana na hadith uliyoitaja, haihusiani na kunusuru kusimamishwa kwa dola, bali inahusu ruhusa kwa mtu ambaye ni dhimmi (raia asiyekuwa Muislamu) au aliye chini ya mkataba anayeishi ndani ya Khilafah kupigana sambamba na Waislamu katika jeshi lao dhidi ya maadui zao. Ili kukufafanulia jambo hilo, nitanukuu baadhi ya maandiko yanayofaa:

Hadith uliyoitaja imepokelewa na Bukhari na Muslim:

«... ثُمَّ أَمَرَ بِلَالاً فَنَادَى بِالنَّاسِ إِنَّهُ لَا يَدْخُلُ الْجَنَّةَ إِلَّا نَفْسٌ مُسْلِمَةٌ، وَإِنَّ اللَّهَ لَيُؤَيِّدُ هَذَا الدِّينَ بِالرَّجُلِ الْفَاجِرِ»

“...Kisha akamwamuru Bilal awalinganie watu, ‘Hataingia peponi isipokuwa Muislamu, na hakika Mwenyezi Mungu ataipa nguvu dini hii hata kwa mtu muovu’” (Lafdhi hii inatokana na Bukhari). Hii ina maana kwamba inaruhusiwa kwa mtu asiye Muislamu au mwenye dhambi anayeishi katika dola ya Kiislamu, kama vile dhimmi, kupigana katika jeshi la Kiislamu ikiwa ana ujuzi katika sanaa ya vita. Miongoni mwa dalili ya hili ni yafuatayo:

A- Imetajwa katika Shakhsiya ya Kiislamu Juzuu ya 2, Sura ya kutafuta msaada kutoka kwa wasiokuwa Waislamu katika vita:

Inaruhusiwa kutafuta msaada kutoka kwa makafiri katika wadhifa wao kama watu binafsi kwa sharti kwamba wako chini ya bendera ya Kiislamu bila kujali kama wao ni dhimmi au la, au kama wao ni raia wa Dola ya Kiislamu au la. Ama kuhusu kutafuta msaada kutoka kwao kama taifa maalum lenye umbo huru na Dola ya Kiislamu, hii hairuhusiwi kabisa. Kwa hivyo ni haramu kutafuta msaada wao katika wadhifa wao kama Dola huru. Dalili ya kuruhusu kutafuta msaada kwa makafiri kama watu binafsi ni “Qazman alitoka na maswahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) siku ya Uhud alipokuwa mshirikina, na akawaua watu watatu wa Banu Abd al-Dar, washika bendera wa washirikina, hadi Mtume (saw) akasema: “Hakika, Mwenyezi Mungu anaipa nguvu dini hii hata kwa mtu mwovu” (Imesimuliwa na al-Tabari katika historia yake).

B- Pia imetajwa katika Nayl al-Awtar na al-Shawkani, Sura kuhusu yale yaliyosemwa kuhusu kutafuta msaada kutoka kwa washirikina: [B- Vile vile, katika Nayl al-Awtar na al-Shawkani, katika sura kuhusu kutafuta msaada kutoka kwa washirikina, imeelezwa: [Miongoni mwa mambo yanayoonyesha ruhusa ya kutafuta msaada kutoka kwa washirikina ni yafuatayo: “Kwamba Qazman alitoka na maswahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) siku ya Uhud, alipokuwa mshirikina, na akawaua watu watatu kutoka Banu Abd al-Dar, wabeba bendera wa washirikina. Hadi Mtume (saw) aliposema: «إنَّ اللَّهَ لَيَأْزُرُ هَذَا الدِّينَ بِالرَّجُلِ الْفَاجِرِ» ‘Hakika, Mwenyezi Mungu huimarisha dini hii hata kwa mtu mwovu.’” Hili linathibitishwa na waandishi wa wasifu.]

Kama unavyoona, hadith hii ni dalili kwamba inaruhusiwa kwa mtu ambaye ni dhimmi au mtu aliyefungamana na mkataba kupigana pamoja na Waislamu katika jeshi lake dhidi ya maadui zao... na haina uhusiano wowote na kunusuru kuanzishwa kwa Khilafah.

2- Kuhusu swali lako kuhusu ruhusa ya kutafuta nusra kutoka kwa watawala wa Kiislamu wa zama hizi, jambo hili linajadiliwa kwa kina katika jumbe zetu za faragha kwa wale wanaofanya kazi katika uwanja wa kutafuta nusra. Hata hivyo, nitanukuu kutoka kwao kinachohusiana na swali lako kuhusu kutafuta nusra kutoka kwa watawala katika nchi za Kiislamu zama hizi:

[… Ikiwa eneo lina mamlaka ya utawala ambayo, mahusiano na maumbo yanayozunguka—iwe kabila au dola—yanasimamia mambo ya watu wake, yanasimamia maisha yao, yanawalipa watu wema miongoni mwao, yanawaadhibu wakosaji, na kadhalika...Na ikiwa yana nguvu na ustahimilivu wa kujilinda dhidi ya maumbo yanayozunguka, basi kwa kweli ni umbo ambalo kwalo ombi la nusra linatumika.

• Kuna njia mbili za kutafuta nusra:

Njia ya kwanza: Kuomba nusra kutoka kwa mkuu wa umbo hilo, iwe ni chifu wa kabila au mkuu wa dola...

Njia ya pili: Kuomba nusra kutoka kwa kundi la watu wenye mamlaka ndani ya umbo hilo...

Utumiaji wa njia hii katika kesi zote mbili hutegemea asili ya maumbo haya, iwe ni dola au makabila:

* Ikiwa umbo liko uhuru katika mambo yake, inaruhusiwa kuomba nusra kutoka kwa mojawapo ya njia zilizo hapo juu: kutoka kwa kiongozi wake au kutoka kwa idadi ya watu wenye mamlaka ndani yake.

* Ikiwa linanasibishwa na dola ya kigeni na halitaki kukata mafungamano, na tunafahamu hili, hatutakubali nusra yake isipokuwa likikata uhusiano wake na dola ya kigeni. Katika hali hii, tutatumia njia ya pili tu (ikiwa ni lazima), yaani, kutoka kwa kundi ndani ya watu wenye nguvu.

• Kwa kusoma na kutafakari kuhusu Seerah (Wasifu wa Mtume (saw)), mambo haya yanakuwa wazi: ...

Tumeelezea kwa undani kwa wale wanaofanya kazi kutafuta nusra, pamoja na dalili yake... Hata hivyo, nitataja jambo moja kutoka humo linalohusiana na swali lako:

[Kuhusu makabila yenye mafungamano na dola za kigeni, na dola zenye mahusiano ya kigeni, hatutafuti nusra yao ikiwa tunajua uhusiano wao wa kigeni. Wala hatukubali nusra yao katika jambo moja na wao kuuzuia nusra katika jambo jengine ili kuiridhisha dola ya kigeni wanayoiunga mkono. Badala yake, ikiwa ni lazima, mbinu katika hali ya pili ndiyo inayofuatwa: kutafuta nusra ya watu kutoka miongoni mwao ambao, kwa pamoja, wataunda nguvu inayoweza kuleta mabadiliko. Hivi ndivyo ilivyotokea kwa kabila la Shayban ibn Tha'labah, kama ilivyotajwa katika 'Uyun al-Athar (1/202):

[Qasim ibn Thabit ametaja, katika niliyoyaona kutoka kwake, hadith iliyosimuliwa na Abdullah ibn Abbas kutoka kwa Ali ibn Abi Talib, kuhusu kuondoka kwake yeye na Abu Bakr pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) kwa lengo hilo. Ali alisema: Abu Bakr alikuwa mstari wa mbele katika matendo mema kila wakati, kwa hivyo akauliza: “Watu hawa ni kina nani?” Wakajibu: “Wanatoka katika kabila la Shayban ibn Tha'labah.” Abu Bakr alimgeukia Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) na kusema: “Baba yangu na mama yangu watolewe kafara kwa ajili yako! Hawa ni watu mashuhuri miongoni mwa watu wao, na miongoni mwao ni Mafruq ibn Amr, Hani ibn Qubaysah, Muthanna ibn Harithah, na Nu'man ibn Sharik. Mafruq ibn Amr aliwazidi kwa uzuri na ufasaha...”

Mafruq alisema, “Labda wewe ni ndugu wa Maquraysh?” Abu Bakr akajibu, “Je, mmesikia kwamba yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu? Yuko hapa.” Mafruq akasema, “Tumesikia kwamba anasema hivyo. Kwa hivyo, mnaomba nini, enyi ndugu wa Waquraishi?” Kisha Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) akasogea mbele na kusema, “Ninalingania kushuhudia kwamba hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu pekee, asiye na mshirika, na kwamba mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na kwamba mnipe hifadhi na kuninusuru, kwani Waquraishi wamekula njama dhidi ya amri ya Mwenyezi Mungu, wamewakataa Mitume wake, na wamegeukia batili badala ya haki. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kujitosheleza, Mwenye kusifiwa.”

Kisha Mafruq akasema: Wallahi, Ewe ndugu wa Waquraishi, umelingania maadili mema na matendo mema, na hakika, watu wamekusingizia urongo na kula njama dhidi yako...

Ilikuwa kama vile alitaka kumjumuisha Al-Muthanna ibn Haritha katika mazungumzo, kwa hivyo akasema...

(Tulikuja hapa kwa sababu tu ya agano tulilofanya na Kisra kwamba hatutasababisha matatizo yoyote wala kumpa hifadhi mtu yeyote mkorofi. Na naona kwamba jambo hili unalotuita ni jambo ambalo wafalme hawalipendi. Ukitaka tukulinde na kukunusuru kutoka upande wa maji ya Arabuni, tutafanya hivyo. Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), akasema: «ما أسأتم في الرد إذ أفصحتم في الصدق وإن دين الله لن ينصره إلا من حاطه من جميع جوانبه» “Hakukosea katika jibu lako, kwani umesema ukweli, na dini ya Mwenyezi Mungu itakuwa na ushindi tu kupitia wale wanaoilinda kutoka pande zote”…)]

Mtume (saw) alipogundua kwamba kulikuwa na mkataba kati ya Banu Shayban na Wafursi, na kwamba Banu Shayban wangemnusuru dhidi ya Waarabu lakini si dhidi ya Wafursi, hakukubali sharti hili kutoka kwao, ingawa walikuwa wamekubali kumnusuru dhidi ya Maquraishi na Waarabu. Waliamuru kwamba usaidizi huu uwe tofauti na Wafursi kwa sababu ya mkataba walioufanya na Wafursi. Ingawa Mtume (saw) alihitaji usaidizi dhidi ya Maquraishi, hakukubali isipokuwa wamnusuru dhidi ya makafiri wote.]

Hivi, kwa ufupi, ndivyo wito wa nusra ulivyofanywa wakati wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw). Na hivi ndivyo tunavyofuata, kwa msaada wa Mwenyezi Mungu, na tunamwomba Yeye, Aliye Tukuka, aturuzuku mafanikio katika kurudisha maisha kamili ya Kiislamu kupitia kusimamisha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume ...

Nataraji haya yametosheleza, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Zaidi.

Ndugu Yenu,

Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah

27 Dhul Qi'dah 1447 H

Sawia na 14/05/2026 M

Link ya ukurasa wa Amiri wa Facebook

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu