Alhamisi, 18 Ramadan 1445 | 2024/03/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Jibu la Swali

Wimbi la Kupanda kwa Bei nchini Jordan

(Imetafsiriwa)

Swali:

Wimbi la bei ya juu linaikumba Jordan, na kuathiri bidhaa za kimsingi za chakula kama vile kuku, mafuta na nyama nyekundu, pamoja na bidhaa zingine. Je, mgogoro huu wa maisha ni wa muda mfupi au una sababu za kushinikiza mfumo wa kiuchumi nchini Jordan kutokana na uhusiano wake wa kikanda na kimataifa? Na uvumi kwamba ugonjwa wa Korona na vita vya Urusi na Ukraine ndio sababu ya bei ya juu ni kweli?

Jibu:

Mapitio ya hali ya uchumi nchini Jordan yanaonyesha yafuatayo:

Kwanza: Sababu ya kawaida ya kupanda kwa bei nchini Jordan inaweza kufupishwa katika ukosefu wa huduma ya serikali kwa raia wake. Wakati Bahari ya Chumvi inakauka kwa sababu ya unyonyaji wa Kiyahudi wa maji ya Mto Jordan na Bahari ya Chumvi, ambayo mwambao wake unakaa vifaa vya Kiyahudi vya viwanda, afya na madini, Jordan, kwa upande mwingine, inajenga vifaa vidogo na visivyo na maana. Jordan inajiepusha na utafutaji madhubuti wa mafuta na gesi katika eneo la Bahari ya Chumvi, ambayo baadhi ya vyanzo vimekadiriwa kuwa vyanzo vyake vya nishati vinawakilisha utajiri mkubwa na wa kiwango cha kwanza. Wakati ambapo hazina ya serikali inapata hasara kubwa katika kuagiza gesi kutoka kwa umbile la Kiyahudi kuendesha vituo vya umeme, pamoja na matumizi mengine ya gesi, Jordan kwa upande mwingine haitilii maanani kuagiza gesi kutoka nchi tajiri za Ghuba na kwa mtazamo muhimu zaidi, haianzishi vinu vya nyuklia kuzalisha umeme na kutumia kiasi kikubwa cha uranium chini ya ardhi ya eneo la Jordan. Licha ya "sauti" kuhusu tafiti katika uwanja huu, bado utawala wa Jordan, ikiwa ni mwaminifu na wa kweli, unaweza kuwa msambazaji mkuu wa umeme katika eneo zima kutokana na nishati kubwa ya nyuklia iliyohifadhiwa katika ardhi yake.

Pili: Wakati watu wa Jordan walipoanza kutegemea kwa kiasi fulani nishati ya jua kulipa sehemu ya bili zao za umeme katika nyumba na viwanda vyao, serikali iliwafumbua macho na kutishia kutoza ushuru kwa jua na anga ili kuacha mwenendo huu na kupunguza manufaa ya wananchi kutokana na nishati hii ya bure. [Wataalamu wa masuala ya nishati na uchumi walilaani mwelekeo wa serikali wa kutoza ada ya dinari mbili kwa kila kilo ya uwezo wa kuzalisha umeme wa sola ambazo wananchi hutumia nyumbani, ikizingatiwa kuwa paneli hizo haziigharimu serikali chochote, na zimewekwa kwa gharama za raia. (Tovuti ya Jo24, 3/3/2022)].

Tatu: Moja ya sababu za wimbi la sasa la bei ya juu nchini Jordan ni kuunganisha uchumi wa Jordan na nchi za kibepari. Dolari ya Marekani ni akiba ya Benki Kuu ya Jordan inayosaidia dinari. Dinari ya Jordan inazunguka na dolari, juu na chini, na hii ina maana kwamba kutokuwa na uwezo wa serikali kupitisha hifadhi ya dhahabu kulifanya uchumi wa Jordan kuwa mojawapo ya wasaidizi wa kimataifa wa uchumi wa Marekani. Moja ya dhihirisho la utegemezi huu ni kwamba Amerika, baada ya janga la virusi vya Korona, ilianza kuongeza kiwango cha riba (riba) ya mikopo baada ya kugusa sifuri, ambayo ilisababisha Benki Kuu ya Jordan kuongeza kiwango cha riba pia: [Uamuzi wa Benki Kuu ya Jordan wa kuongeza viwango vya riba kwa zana zake zote za sera ya fedha uliongezeka kwa pointi 50, kufikia Jumapili iliyopita, kulingana na uamuzi wa Hifadhi ya Majimbo ya Marekani, umeibua wasiwasi wa wadeni binafsi wa benki na sekta za kiuchumi kutokana na hatua ya benki hiyo kuongeza viwango vya riba kwa huduma za mikopo, ikiwa ni pamoja na mikopo ya kibinafsi. (Al-Araby Al-Jadeed, 13/5/2022)], na hivyo Benki Kuu ya Jordan ilifuata uamuzi wa Benki ya Shirikisho ya Marekani na kuacha kundi la Wajordan wakishangaa kwamba riba imeongezeka kwenye mikopo yao ya awali katika benki za biashara, na. kwamba awamu zao za riba ambazo zilipaswa kulipwa zimeongezeka!

Nne: Aidha, serikali imewalemea watu wa Jordan kwa mikopo. Deni la serikali nchini Jordan limeongezeka. [Kulingana na takwimu za hivi punde za Benki Kuu ya Jordan mwishoni mwa Novemba mwaka jana kwa dinari bilioni 2.32 kufikia dinari bilioni 35.35, na kutengeneza asilimia 110.3 ya Pato la Taifa, ikilinganishwa na dinari bilioni 33.03 mwishoni mwa 2020, na asilimia 106.5 ya Pato la Taifa kwa kipindi hicho. (Al-Araby Al-Jadeed 16/4/2022)], ikimaanisha kuwa deni lote ni takriban dolari bilioni 50... ambazo ni deni la ndani kutoka benki za Jordan na madeni ya nje. Kulingana na maelezo yaliyotolewa na chanzo hicho cha awali, Jordan inalipa zaidi ya dolari bilioni 2.7 kila mwaka katika kodi zinazokusanywa na serikali ili kuhudumia madeni haya (riba), na hii ni idadi kubwa na inawakilisha 37% ya thamani ya kodi ya kila mwaka zilizokusanywa na serikali kutoka kwa raia wa Jordan. Kwa mujibu wa Gazeti la Independent Arabi, 12/1/2022: (Wajordan wanalalamikia ongezeko la mara kwa mara la kiasi cha ushuru na ada walizotozwa katika miaka ya hivi karibuni, kwa kuwa imechukua sehemu kubwa ya mapato yao. Wananchi wa Jordan wanaielezea nchi yao kama kodi inayotozwa zaidi katika kanda, kiwango cha kodi kwa bidhaa na huduma fulani, kama vile magari na mafuta, zaidi ya asilimia 70, huku robo ya mapato ya wananchi wa Jordan yakienda kwenye kulipa kodi). Kwa hivyo, ni wazi kuwa serikali ya Jordan inafanya kazi katika kuunyang'anya uchumi wa Jordan pesa zinazohitajika kwa ukuaji wa uchumi na kuzilipa kama riba kwa mikopo yake ya nje na ya ndani, na hivyo kuongeza mzigo kwa taasisi za kiuchumi na kuongeza uchovu wa Jordan. Mwananchi anayelipa ushuru kwa kila ununuzi, kiwe kidogo au kikubwa, ikimaanisha kuwa matunda ya ushuru unaokusanywa katika dola hupotea, haswa kwa wakopeshaji wa nje, bila kuwanufaisha wananchi. Raia wa Jordan haoni huduma za ustawi ambazo serikali inapaswa kutoa baada ya kukusanya ushuru. Si hayo tu, bali serikali inazidisha taarifa potofu, kwa madai kuwa wakimbizi wa Syria ni miongoni mwa sababu za kudhoofika kwa uchumi, kutokua kwake, na yote hayo ni kuwahadaa wananchi. Ikiwa taifa la Jordan lingetaka kuchukua fursa ya wakimbizi wa Syria kusaidia uchumi, wangekuwa sababu muhimu katika ukuaji wa uchumi, kama nchi zingine kama Ujerumani, kwa mfano, wakati inataka kuwachukua na kufaidika lakini serikali ya Jordan iliwafunga wengi wao katika kambi zilizofungwa kama wafungwa.

Tano: Moja ya sababu zinazohusika ni kwamba misingi muhimu ya maisha ya watu wa Jordan imewekwa na utawala huo mikononi mwa Mayahudi, kwa vile unaagiza maji kutoka kwao.

1- [Afisa mmoja wa Jordan alisema kuwa Israel "huipatia" Jordan mita za ujazo milioni 30 za maji kila mwaka kwa mujibu wa mkataba wa amani uliotiwa saini kati ya nchi hizo mbili mwaka wa 1994. (BBC, 9/7/2021)]. Kiwango cha Mto Jordan kinapungua hadi ukame kutokana na makubaliano ya utawala wa Jordan kwamba Mayahudi wanyakue Mto Jordan kutoka kwenye chemchemi zake za juu, huku maji ya Jordan yakiwa chini ya ridhaa ya umbile la Kiyahudi, ambalo hutoa, huzuia, huongezeka na hupungua. [Afisa mmoja wa Israel alinukuliwa akisema kwamba makubaliano ya Jordan na Israel yatazidisha maradufu kiwango cha maji ambacho Israel itatoa kwa Jordan mwaka huu, kuanzia Mei 2021 hadi Mei 2022. Israel tayari imeipatia Jordan mita za ujazo milioni 50 hadi sasa, kwa mujibu wa afisa huyo wa Israel. (BBC, 9/7/2021)]. Kuhusu bei za maji ambazo Jordan "inaagiza" kutoka kwa umbile la Kiyahudi, kwa kawaida huwekwa siri kutokana na ubaya wao na ufisadi unaoonekana ndani yao. Hata hivyo, baadhi ya habari zinavuja kuwa bei hizi zinafikia senti 40 za Marekani kwa kila mita ya ujazo, pamoja na bei kubwa ya kusukuma maji na kusafisha, ambayo inafikia senti 22 kwa kila mita ya ujazo (Al-Jazeera Net, 6/6/2011). Kulingana na bei hizi, maji yamekuwa moja ya vikwazo vikubwa kwa uchumi baada ya serikali kujisalimisha yenyewe na watu wake kwa umbile la Kiyahudi kuchukua maji safi ya Mto Jordan na kuipa Jordan maji ya usafi wa kutia shaka.

2- Kadhalika, utawala wa Jordan kwa makusudi uliihusisha Jordan na gesi kutoka kwa umbile la Kiyahudi baada ya kuichukua kutoka nchi za Ghuba, kana kwamba Jordan ilikuwa inawasubiri Mayahudi wavumbue gesi asilia mashariki mwa Bahari ya Mediterania, hivyo ikakata mafungamano yake na Mataifa ya Ghuba na kuyafuma na Mayahudi, ["makubaliano ya Jordan/Israel" juu ya kuagiza gesi kutoka nje yanaeleza kuipatia Jordan gesi ya takriban mita za ujazo bilioni 45 katika kipindi cha miaka 15, kuanzia Januari 2020. Makubaliano haya yanajiri huku kukiwa na mvutano wa kisiasa kati ya Israel na Jordan na upinzani maarufu na wabunge kwa makubaliano haya (The Independent Arabia, 1/1/2020)]. Hata hivyo ilifanyika licha ya mvutano na upinzani!

Sita: Kwa mambo hayo hapo juu, sababu za kweli za kuzorota kwa uchumi wa Jordan zinaonekana wazi, ambapo kiwango cha ukosefu wa ajira kimefikia 42% (The Independent Arabia, 1/3/2019), na kwamba kauli kuhusu mageuzi ya kiuchumi ni tupu kivitendo, hasa kwa vile ufisadi wa serikali unaongeza ubadhirifu na upotevu wa fedha! Hali hii ya kuzorota kwa uchumi inayoendelea nchini Jordan ni sawa na sera ya kiuchumi ambayo nchi za makafiri, Amerika na Uingereza, zinaamuru Jordan ifuate, na kile ambacho Mfuko wa Fedha wa Kimataifa unadai kutoka kwa Jordan. Sera hii ni endelevu, nchi hizi zikihofia kuwa watu wataasi utawala, watawatupia baadhi ya misaada, miongoni mwa misaada hiyo ni baadhi ya michango inayotolewa na IMF ili kuwapunguzia mzigo wa madeni, yaani kulipa riba kwa mikopo ya riba ambayo serikali ilikopa nchini Jordan. Aina nyingine ya usaidizi huo ni kwamba Uingereza imekusanya zaidi ya nchi 60 na taasisi 450 za kifedha katika mkutano wa kimataifa uliofanyika jijini London kusaidia uchumi. Serikali ya Jordan, pamoja na mawaziri wake wengi, walishiriki katika hilo. (The Independent Arabia, 1/3/2019). Lakini misaada yote hii inaelekezwa katika kuzuia mapinduzi ya Ummah kurejesha haki zake.

Saba: Kwa hivyo, sababu za wimbi la sasa la bei ya juu ambazo zinawasumbua watu wa Jordan ziko wazi. Hizi ndizo sababu kuu na za kweli nyuma ya wimbi hili la bei ya juu. Kuhusu sababu zingine za wimbi la juu la bei ulimwenguni ambazo zimetajwa kwenye vyombo vya habari kote ulimwenguni kutokana na janga la Virusi vya Korona, na pia sababu zinazohusiana na vita vya Urusi nchini Ukraine, ingawa zina athari za kiuchumi... haya yanaweza kuondolewa au kupunguzwa ikiwa sababu za kukosekana kwa usawa wa kiuchumi zilizoelezwa hapo juu zitashughulikiwa ipasavyo kwa mujibu wa hukmu za Shariah. Vyenginevyo, nchi hii itazidi kuwa mbaya na bei zitakuwa juu zaidi, na Mwenyezi Mungu (swt) ni Mkweli.

[وَمَنْ أَعْرَضَ عَنْ ذِكْرِي فَإِنَّ لَهُ مَعِيشَةً ضَنْكاً]

“Na atakaye jiepusha na mawaidha yangu, basi kwa yakini atapata maisha yenye dhiki.” [Ta-Ha: 124].

Hili litaendelea mpaka Umma utakaposuluhisha jambo lake, ushikilie moyo wake kwenye itikadi yake, ushikamane na kamba ya Mwenyezi Mungu, uukabidhi uongozi wake kwa Watoto wake wenye ikhlasi na ufahamu, na uondoe sera ya nchi kubwa kwa kuwaangusha mawakala wao, na kusimamisha Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume ili ardhi ijae uadilifu na ustawi, na kisha maisha yake yageuke kuwa utukufu baada ya unyonge, ustawi baada ya umasikini, na tamkini baada ya unyenyekevu na utegemezi.

 [إِنَّ فِي ذَلِكَ لَذِكْرَى لِمَنْ كَانَ لَهُ قَلْبٌ أَوْ أَلْقَى السَّمْعَ وَهُوَ شَهِيدٌ]

“Hakika katika hayo upo ukumbusho kwa mwenye moyo au akatega sikio naye yupo anashuhudia.” [Qaf: 37].

 7 Dhul Qi’dah 1443 H

6/6/2022 M

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu