Jumamosi, 21 Muharram 1446 | 2024/07/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Enyi Majeshi ya Waislamu!
Nani Atainusuru Rafah, Jenin, na Palestina Yote Ikiwa Hamtazinusuru?!

(Imetafsiriwa)

Al-Hamdulillah Rabb Al-Alamin, ambaye amewajibisha kupigana juu yetu na akaifanya ndio njia ya kuwatiisha makafiri, waasi, na ni chanzo cha heshima kwa Waislamu, waumini, kama alivyosema Yeye, Subhanahu:

[‌قَاتِلُوهُمْ يُعَذِّبْهُمُ اللهُ بِأَيْدِيكُمْ وَيُخْزِهِمْ وَيَنْصُرْكُمْ عَلَيْهِمْ وَيَشْفِ صُدُورَ قَوْمٍ مُؤْمِنِينَ]

“Piganeni nao, Mwenyezi Mungu awaadhibu kwa mikono yenu, na awahizi na akunusuruni muwashinde, na avipoze vifua vya kaumu ya Waumini.” [At-Tawba:14].

Rehma na amani zimshukie Mtume wa Mwenyezi Mungu, Bwana wa Mitume na Imamu wa Mujahidina, na jamaa zake na maswahaba zake, na wanaomfuata.

Enyi Waislamu, enyi Umma wa Uislamu:

Vita dhidi ya Gaza vinakaribia mwezi wake wa nane, na hatuoni yeyote katika Umma wa Kiislamu akichukua hatua! Ni vita vya dhulma na vya dhambi, vilivyojaa mauaji na uharibifu, njaa na kuzingirwa. Na nyinyi, enyi Umma wa Jihad, enyi Umma bora uliotolewa kwa ajili ya wanadamu, mnalaani hilo katika nyoyo zenu na mnatuombea kwa ndimi zenu, lakini ni lini mtawapindua watawala wenu wa khiyana na kuyakusanya majeshi yenu kuinusuru ardhi iliyobarikiwa na watu wake?!

Ee Uislamu: Kilio hiki kilitosha kushajiisha jeshi la Waislamu, na kuwafanya makamanda na askari wake wanyanyuke, wachukue hatua, na kuliangamiza jeshi la Wamongolia kwenye Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, na kusitisha uvamizi wa wale waliobakia katika Waislamu na miji yao.

Na sisi, enyi Umma wa Uislamu, kutoka katika Ardhi hii Tukufu, tunayalilia majeshi yako katika Misri, Jordan, Uturuki, Pakistani na nchi zote za Kiislamu, tunakulilia kwa kelele elfu moja za “Ewe Uislamu” na tunakuambia. : Rafah, Gaza, Jenin, na Msikiti wa Al-Aqsa zinaomba msaada wako na msaada wa majeshi yako. Je, utajibu? Je, utajibu simu? Enyi majeshi ya Ummah, je, sisi hatuna haki ya kuwaunga mkono? Je, hujasoma maneno Yake:

Na sisi, enyi Umma wa Uislamu, kutoka katika Ardhi hii Iliyobarikiwa, tunayalilia majeshi yenu nchini Misri, Jordan, Uturuki, Pakistan na nchi zote za Kiislamu, tunakulilieni kwa vilio elfu moja vya “Ee Uislamu” na tunakuambieni:

Rafah, Gaza, Jenin, na Msikiti wa Al-Aqsa zinaomba msaada wenu na msaada wa majeshi yenu. Je, mutaitika? Je, mutajibu wito?

Enyi majeshi ya Ummah, je, sisi hatuna haki ya nusra yenu? Je, hamjasoma maneno Yake:

[وَإِنِ ‌اسْتَنْصَرُوكُمْ فِي الدِّينِ فَعَلَيْكُمُ النَّصْرُ]

“Lakini wakiomba msaada kwenu katika Dini, basi ni juu yenu kuwasaidia.” [Al-Anfal:72].

Basi kwa nini hamsongi kwa kumuitikia Mwenyezi Mungu, kwa kuwanusuru ndugu zenu wanaodhulumiwa, na kuukomboa Msikiti wa Al-Aqsa, Masra (mahali pa safari ya usiku) ya Mtume wenu?

Ewe Jeshi Tukufu la Misri Tukufu Al-Kinanah:

Ewe hazina ya Umma na Kinanah ya Uislamu, maafisa waliojitolea wa jeshi la Misri:

Ikiwa damu, miili iliyokatwakatwa, uharibifu wa nyumba, na mauaji ya wanaume na wanawake bado hayajakuchocheeni, kilio chetu cha leo na kikuchocheeni kuchukua hatua. Nyinyi ni sehemu yetu na sisi ni sehemu yenu, na hatutakata tamaa na wema uliomo nyoyoni mwenu.

Ee Jeshi la Misri: Ni nani atakayeinusuru Rafah, Jenin, na Palestina yote kama sio nyinyi? Mna uwezo, ikiwa mna ikhlasi kwa Mwenyezi Mungu, kuwaadhibu wale aliowakasirikia, kuwaangamiza, na kuikomboa Palestina yote kwa siku moja au sehemu ya siku. Mnawezaje kutofanya hivyo, wakati nyinyi ni jeshi lenye nguvu na askari wenu ni miongoni mwa bora zaidi duniani! Mpindue Sisi mhalifu, anayekula njama dhidi ya Uislamu na Waislamu na kukuzuieni kutekeleza wajibu wenu. Mpindueni na muungane kusimamisha Dini, kukomboa Msikiti wa Al-Aqsa, na kuwanusuru wanaodhulumiwa. Mwenyezi Mungu (swt) asema:

[فَلْيُقَاتِلْ فِي سَبِيلِ اللهِ الَّذِينَ ‌يَشْرُونَ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا بِالْآخِرَةِ وَمَنْ يُقَاتِلْ فِي سَبِيلِ اللهِ فَيُقْتَلْ أَوْ يَغْلِبْ فَسَوْفَ نُؤْتِيهِ أَجْراً عَظِيماً]

“Basi nawapigane katika Njia ya Mwenyezi Mungu wale ambao wanao uza uhai wa dunia kwa Akhera. Na anaye pigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu kisha akauliwa au akashinda basi tutakuja mpa ujira mkubwa.” [An-Nisa:74].

Ama nyinyi, enyi jeshi la Jordan, enyi watukufu katika ardhi ya mkusanyiko na nguvu: Mnawezaje kustahimili yanayotokea Rafah, Gaza na Al-Aqsa?

Je, nyoyo zenu haziungui kwa hamu ya kuwanusuru watoto na wanawake, na hamu ya kuswali katika Msikiti wa Al-Aqsa?

Au mnawaogopa wale ambao Mwenyezi Mungu amewaandikia fedheha na mateso, licha ya kushuhudia uthabiti wa mashujaa unaowakabili kwa silaha nyepesi? Je, uthabiti na ushujaa wa mujahidina haukutieni msukumo wa kujiunga nao katika jihad kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, ili Mwenyezi Mungu akutukuzeni kwa ushindi wake na akupeni fadhla ya kuikomboa Ardhi Iliyobarikiwa kwa mikono yenu?

Vunjeni viti vya utawala vilivyokufungeni na muwapindue watawala wanaokuzuilieni kutimiza yale ambayo Mwenyezi Mungu amewajibisha juu yenu. Songeni mbele kwa jina la Mwenyezi Mungu na kwa baraka zake ili kusimamisha Dini na kuwanusuru wanaodhulumiwa.

[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنْ تَنْصُرُوا اللهَ ‌يَنْصُرْكُمْ وَيُثَبِّتْ أَقْدَامَكُمْ]

“Enyi mlio amini! Mkimnusuru Mwenyezi Mungu naye atakunusuruni na ataithibitisha miguu yenu.” [Muhammad:7]

Ama Uturuki na Pakistan:

Kutoka hapa, kutoka Ardhi Iliyobarikiwa, kutoka Palestina iliyojeruhiwa, tunatuma ujumbe kwa watu wa Uturuki na jeshi lao lenye nguvu, na kwa watu wa Pakistan na jeshi lao lisiloshindika:

Jukumu lenu ni kubwa sana, na nafasi yenu katika nyoyo za Waislamu ni kubwa. Nyinyi ni watu wa vita na wapiganaji, mna idadi na vifaa. Hamkukosa askari wala silaha. Mnachohitaji ni uongozi wa kisiasa wenye ikhlasi na makini ambao kwao mnaweza kusimamisha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume. Kisha, kwa jina la Mwenyezi Mungu na kwa kufuata nyayo za Maswahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, mtasonga mbele kukomboa Masra ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) na kueneza Uislamu kote duniani.

Enyi Waislamu kila mahali:

Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) amesema: «الْمُسْلِمُ أَخُو الْمُسْلِمِ لَا يَظْلِمُهُ وَلَا يَخْذُلُهُ وَلَا يَحْقِرُهُ» “Muislamu ni ndugu yake Muislamu. Hamdhulumu wala hamtelekezi, wala hamchukii.” (Sahih Muslim). Hivyo msiache hali yenu ikawa kama ile ya wale wanaonyamaza kimya mbele ya watawala wao wa kiimla na kuitelekeza Gaza na Rafah mpaka hatma yao inaamuliwa na maadui wa Uislamu wapendavyo. Msifanye hali yenu iwe kama yale wanaojuta kwa kusema: “Nililiwa wakati Gaza na Rafah zilipoliwa.” Ni kipi basi kinachozuia kuanguka kwa miji inayosalia ya Waislamu mikononi mwa maadui wa Umma?! 

Ama kwenu nyinyi, Enyi watu wa Gaza: Huenda Mwenyezi Mungu akakubarikini katika dunia hii kwa ushindi kwa mikono ya ndugu zenu Waislamu wenye nguvu, wema, na katika Akhera, Jannah ipitayo mito chini yake, iliyoandaliwa kwa ajili ya watu wema.

[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ ‌لِمَا يُحْيِيكُمْ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللهَ يَحُولُ بَيْنَ الْمَرْءِ وَقَلْبِهِ وَأَنَّهُ إِلَيْهِ تُحْشَرُونَ]

“Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuitieni jambo la kukupeni uzima wa milele. Na jueni kuwa Mwenyezi Mungu huingia kati ya mtu na moyo wake, na kwamba hakika kwake Yeye tu mtakusanywa.” [Al-Anfal:24].

Ewe Mwenyezi Mungu, tufikishie kheri hii kutoka kwetu, na uzilainishe kwayo nyoyo za Waislamu. Tupe nusra kutoka Kwako, na utujaalie tuwe washindi. Al-Hamdulillah Rabb Al-Alameen.

H. 16 Dhu al-Qi'dah 1445
M. : Ijumaa, 24 Mei 2024

Hizb-ut-Tahrir
Ardhi ya Baraka-Palestina

Yaliyomo ndani ya kifungu hichi: « Mpaka Lini, Enyi Ummah wa Muhammad?!

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu