Afisi ya Habari
Wilayah Pakistan
| H. 2 Jumada I 1447 | Na: 11 / 1447 |
| M. Ijumaa, 24 Oktoba 2025 |
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Watawala wa Pakistan wanaogopa mwamko wa Kiislamu unaoongezeka miongoni mwa Waislamu wa Pakistan na, kupitia utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Utendakazi, wanajaribu—bila mafanikio—kuusimamisha kwa kuigeuza Pakistan kuwa “dola ngumu zaidi.”
(Imetafsiriwa)
Mwenendo mkali na wa kikatili wa watawala dhidi ya mkutano wa TLP umesababisha mawimbi ya wasiwasi katika duara za kidini za Pakistan na kumshangaza kila Muislamu mwenye ufahamu. Hata hivyo, mbinu hii ya kiimla ya watawala wa Pakistan si kitendo cha pekee au kisicho cha kawaida; bali ni sehemu ya msururu wa hatua mfululizo ambazo watawala wamechukua katika siku za hivi karibuni, hatua zilizozidi wakati watawala wa Pakistan walipokubali kutekeleza mpango wa Trump pamoja na watawala wa nchi za Kiarabu na zengine za Kiislamu, mpango ambao lengo lake ni kulinda uwepo wa Mayahudi kutokana na upinzani wa Waislamu wa Palestina. Na Waislamu wa Pakistan walipokataa mpango wa Trump wa nukta 20, watawala hao walianza kuunda mazingira ya hofu kwa kuwakamata na kuwapoteza kwa nguvu wanaharakati vijana waliohamasishwa kwa ajili ya Palestina kote nchini – wakiwemo vijana kadhaa wa Hizb ut Tahrir – ambao, kupitia amali zao za dawah, walikuwa wamevitaka Vikosi vya Jeshi la Pakistan vichukue hatua ya kuondoa uwepo wa Mayahudi na kuikomboa al-Aqsa, kwa sauti ya Ummah.
Ili kuficha mwendelezo huu wa ukandamizaji na udhalimu, watawala wa Pakistan sasa wanatoa kisingizio kwamba TLP hapo awali imevuka mipaka na kutumia mbinu za vurugu – ilhali ukweli ni kwamba wahalifu halisi katika hali hii yote ni watawala wenyewe, ambao sera zao zinawaacha mamilioni ya Wapakistani wakihisi kutokuwa na usalama na wasiwasi kuhusu maadili yao matakatifu. Mwenendo wa watawala wa Pakistan ni tofauti kabisa na ule wa dola ya zamani ya Khilafah, ambayo ilikuwa ikitekeleza majukumu ya Uislamu hata kabla ya watu kuyadai; ndiyo maana watu waliichukulia Khilafah hiyo kuwa dola yao na wakasimama ubavuni mwake kutimiza malengo ya Uislamu, na hawakuhitaji kwenda kwenye maeneo ya umma.
Tangu kuundwa kwa Pakistan, kipote cha watawala wamejua kwamba Waislamu wa Pakistan wanahisi kusalitiwa kwa jina la Uislamu na walitumika kama chakula cha kuanzisha dola ya kisekula. Ili kudumisha unyonge huo wa kidini na kutokuwepo kwa lengo la pamoja usingizini, dola ya Pakistan imeupamba Uislamu kijuu juu dhidi ya usekula. Mabwana wakoloni wa dola ya Pakistan, kutokana na kisiasa za kieneo za wakati huo, pia waliruhusu kipote cha watawala kutekeleza baadhi ya sheria za Kiislamu. Hata hivyo, kwa miongo mitatu iliyopita kote Pakistan na ulimwengu mzima wa Kiislamu, mwamko unaoongezeka wa Kiislamu – na uzembe wa jinai kuhusu mauaji ya halaiki huko Gaza – umesababisha sura hii ya Uislamu na watawala kushindwa kuwatuliza Waislamu, na kila siku shinikizo linaongezeka kwa watawala wa Pakistan kutoka kwa Waislamu ili kuegemeza uhusiano wao wa kigeni kwenye amri za Uislamu badala ya amri za Amerika. Waislamu wa Pakistan wanataka kuona vikosi vya jeshi la Pakistan vikipigana jihad dhidi ya uwepo wa Mayahudi, kuwaondoa, na kuikomboa Bayt al-Maqdis – sio kuona vikosi hivi vikitoa dhamana ya usalama kwa uwepo wa Mayahudi chini ya uongozi wa Trump! Kujibu shinikizo hili linaloongezeka la watu, watawala wa Pakistan wanaashiria mfumo wa “dola ngumu”, wakifuata nyayo za Mustafa Kemal – mwanzilishi wa usekula – Al Saud, na Husni Mubarak, na wamesahau jinsi Mwenyezi Mungu anavyowageuza watawala wakandamizaji kuwa mifano kwa watu wa dunia.
Watawala wa Pakistan wanashiriki katika mapambano ya kudumu na Waislamu wa Pakistan na wanatafuta kubadilisha mitazamo ya Wapakistani na hisia zao za Kiislamu kwa mtutu wa bunduki na kwa matendo yao mabaya ili waendane na mtazamo wa kisekula wa serikali na kuwa wagumu kama watawala hawa wenyewe. Kwa hivyo ni watawala hawa ndio wameichafulia jina dini kuiita msimamo mkali ili kuwazuia Waislamu wa Pakistan kudai utekelezwaji kamili wa Uislamu. Ni watawala hawa ambao, kama vile duara za kisiasa, hutumia hongo kuwachukua baadhi ya watu kutoka duara za kidini na kuwatisha wengine ili wahudumie ajenda ya watawala; lengo lao ni kuwaaibisha Waislamu wa Pakistan kwa kushikamana kwao kwa kina na Uislamu na kuwashawishi kwamba udini huleta matokeo mabaya. Ni kundi tawala lililobuni mtaala wa elimu kwa makusudi kwa njia ya kuwabakisha watu wakiwa wamechanganyikiwa kuhusu Uislamu ili utabikishwaji Uislamu usiwe lengo lao thabiti. Kupitia sera huria ya vyombo vya habari, watawala wa Pakistan wanawasukuma watu kuelekea kwenye upendaji vitu vya kimada, anasa, na mtindo wa maisha wa kisekula, wakijaribu kuwatenga na mtindo wa maisha wa Kiislamu. Kupitia sera za kibepari, wamewaweka chini idadi kubwa ya watu wa Pakistan katika kinu cha umaskini ili wabaki wamenaswa katika mapambano ya kila siku ya kujikimu na uundaji wa sera unabaki chini ya udhibiti wa kipote chenye nguvu cha kisekula cha kisiasa bila kuingiliwa.
Watawala wa Pakistan wamekuwa uovu mtupu. Wanaunda uovu, wanalea uovu, na, kwa maslahi yao binafsi, wanaitumbukiza Pakistan katika moto wa uovu. Kama hatua ya kuzuia upinzani wowote dhidi ya mpango wa amani wa Trump, wameigeuza Punjab kuwa uwanja wa mauaji. Hapo awali walikuwa wameyafanya maeneo yote ya kikabila kuwa uwanja wa mauaji ili kukanyaga upinzani uliopo dhidi ya vikosi vya Marekani vinavyokalia Afghanistan; walizidisha badala ya kuponya dhulma walizotendewa Waislamu wa Balochistan na kuigeuza Balochistan kuwa uwanja wenye rutuba kwa shughuli mbaya za vikosi vya uadui. Watawala hawa ni saratani ambayo imeenea kila nyanja ya maisha ya Waislamu wa Pakistan.
Kwa hivyo, uongozi wote wa kidini na kikasisi haupaswi kuridhika na matakwa ya kivipande bali unapaswa kuungana kuwaondoa watawala hawa na kujitahidi kusimamishwa kwa mfumo wa Kiislamu wa Khilafah ili tatizo liweze kung'olewa, uovu umalizike, na Waislamu wa eneo hili waweze kuishi chini ya mfumo wa adilifu wa Uislamu kwa amani na usalama. Mtume (saw) amesema: «لَتَأْمُرُنَّ بِالْمَعْرُوفِ وَلَتَنْهَوُنَّ عَنِ الْمُنْكَرِ أَوْ لَيُسَلِّطَنَّ اللَّهُ عَلَيْكُمْ شِرَارَكُمْ ثُمَّ يَدْعُو خِيَارُكُمْ فَلَا يُسْتَجَابُ لَكُمْ» “Hakika nyinyi mtaamrisha mema na kukataza maovu, la sivyo Mwenyezi Mungu atakusalitini kwa waovu wenu zaidi, kisha wema katika nyinyi wataomba na hawatakubaliwa dua kwa ajili yenu.” (Imeripotiwa na al-Ṭabarānī katika al-Mu‘jam al-Awsaṭ)
Kwa robo karne iliyopita, mashababu wa Hizb ut Tahrir wamekuwa wakifanya kazi kwa ajili ya kusimamisha Khilafah katika ardhi ya Kiislamu ya Pakistan — songeni mbele na muwe mkono wa juhudi hizi za ikhlasi na za dhati za mashababu wa Hizb ut Tahrir.
Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Pakistan
| Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari Wilayah Pakistan |
Address & Website Tel: +(92)333-561-3813 http://www.hizb-pakistan.com/ |
Fax: +(92)21-520-6479 E-Mail: htmediapak@gmail.com |



