Jumamosi, 24 Shawwal 1447 | 2026/04/11
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Yaonekana Mazuri, lakini Ndani Hamna Kitu!

Rais Erdoğan, katika hotuba yake baada ya mkutano wa baraza la mawaziri, pia aligusia mwelekeo wa Uturuki wa sera ya kigeni, akisema: “Uturuki imeipa dunia funzo katika haki za binadamu kupitia juhudi zake zinazolenga amani na haki katika maeneo yaliyolowa damu na machozi—Gaza, Syria, Somalia, na Libya.” Alisisitiza kwamba taifa hilo limeunganishwa kwa fungamano lisilotikisika, pasi na tofauti kati ya Mturuki, Mkurdi, Muarabu, Alevi, au  Caucassian. (Mashirika, 15.12.2025)

Ubepari kama Chanzo Kikuu cha Maafa ya Mafuriko huko Sumatra

Kimbunga Senyar kilikuwa kichocheo tu; kiwango cha uharibifu nchini Indonesia kinaonyesha miongo kadhaa ya usimamizi mbaya wa ikolojia. Sumatra imepoteza mamilioni ya hekta za misitu, ikidhoofisha maeneo ya maji huko Aceh, Sumatra Kaskazini, na Sumatra Magharibi. Maeneo ya tambarare yalikaushwa maji kwa ajili ya mashamba makubwa, na kusababisha kupungua kwa ardhi na kugeuza vizuizi vya maji asilia kuwa mabonde ya mafuriko. Makaazi ya haraka katika maeneo tambarare ya mafuriko, pamoja na usimamizi dhaifu wa matumizi ya ardhi, yaliongeza athari. Mvua kali ilipofika, mandhari haikuwa na uwezo uliobaki wa kuhimili. Maafa yanaonyesha kwamba muundo wa maendeleo wa Indonesia—unaoendeshwa na uchimbaji na usimamizi duni wa mazingira—umefanya hali mbaya ya hewa kuwa hatari zaidi kuliko inavyopaswa kuwa. (news.mongabay)

Enyi Waislamu: Kufunga Vyumba vya Ibada ni Shambulizi kwa Uislamu na Lazima Kukabiliwe kwa Upinzani Mkali, wa Pamoja wa Kisiasa

Baada ya mwelekeo hasi wa kisiasa kwenye vyumba vya ibada, idara ya Chuo Kikuu cha Copenhagen iliamua mwishoni mwa Novemba kufunga kile kinachoitwa “vyumba vya utulivu,” ambavyo Waislamu walikuwa wakivitumia kwa zaidi ya miaka ishirini, bila matatizo yoyote, na wanafunzi na wafanyikazi kuswali swala za kila siku. Uamuzi huu kwa mara nyingine tena umezua mjadala kuhusu vyumba hivi na kuhusu kama kunapaswa kuwepo na nafasi kwa Waislamu kutekeleza swala zao katika taasisi za elimu.

Unyanyasaji wa Kimpangilio wa Kijinsia Dhidi ya Wanawake wa Sudan Hautoi Jibu lolote kwa Kukosekana kwa Dola Inayojali Heshima ya Mwanamke Mwislamu

Mnamo Alhamisi tarehe 11 Disemba, shirika, ‘The Strategic Initiative for Women in the Horn of  Africa’, liliripoti kuwa limerekodi karibu matukio 1300 ya unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake katika majimbo 14 nchini Sudan tangu vita vianze nchini humo mnamo Aprili 2023, huku Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vikilaumiwa kwa 87% ya visa hivi. Lilielezea unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake ukitumika kama silaha ya kimfumo katika mzozo huo, likisema “umeenea, unarudiwa rudiwa, unakusudiwa na mara nyingi unalenga”. Ubakaji ulichangia robo tatu ya matukio yaliyorekodiwa, huku visa 225 vikihusisha watoto, baadhi wakiwa na umri wa miaka 4. Matukio yalitokea majumbani, maeneo ya umma na pia yalijumuisha kizuizini cha muda mrefu cha wanawake ambao waliteswa, kubakwa na genge na ndoa za kulazimishwa. Mnamo Jumapili tarehe 7 Disemba, vikundi vya matibabu vya Sudan viliripoti kwamba watoto na wanawake kadhaa walinyanyaswa kingono na kubakwa walipokuwa wakikimbia kukamatwa kwa El Fasher huko Darfur na RSF Oktoba hii.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu