Jumapili, 15 Muharram 1446 | 2024/07/21
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Uhalifu wa Umbile la Kiyahudi Hautakomeshwa kupitia Upatanishi, Mazungumzo, au Taasisi za Kimataifa

Bali, kipitia Uhamasishaji wa Majeshi ya Kiislamu Kuharibu kile Walichokichukua kwa Uharibifi Kamili
(Imetafsiriwa)

Mwenyezi Mungu awarehemu mashahidi wetu, na Mwenyezi Mungu awaponye majeruhi wetu, Ina lilahi Wa Ina Ilaihi Raji’oon, La Hawla Wa La Quwata Ila Billah, Hasbuna Allah Wa Ni’ma Al-Wakeel.

Uvamizi wa umbile la Kiyahudi dhidi ya Umma wa Kiislamu bado unaendelea na unakua siku baada ya siku, ukiwa na uungaji mkono wa Marekani, uhalalishaji mahusiano wa Waarabu na uratibu wa usalama pamoja na Mamlaka ya khiyana ya Palestina (PA). Msikiti wa Al-Aqsa unavamiwa na walowezi wanaunajisi, na wanaendelea kuua na kuharibu kwa kila kiburi na jeuri chini ya masikio na macho ya ulimwengu mzima katika matangazo mbashara na ya moja kwa moja. Kumwaga damu ya Waislamu imekuwa kichwa cha matukio, na miili yao ni hifadhi ya shabaha za makombora na ndege. Hizi ni sera za maadui wa Uislamu; kuwasha moto, kupigana vita na kuleta maangamizi katika ardhi za Waislamu, mpaka kumwagika kwa damu yetu tukufu kukawa nukta katika rekodi ya mafanikio ya watawala wao, na aina ya propaganda ya uchaguzi iliyopakwa rangi kwa damu ya Waislamu. Rais Obama wa Marekani aliimarisha kampeni zake za uchaguzi kwa kumuua Sheikh Osama bin Laden, Mwenyezi Mungu (swt) amrehemu, na kwa Biden ili kuimarisha nafasi yake na nafasi ya chama chake katika uchaguzi wa katikati ya muhula, alimuua Sheikh Ayman al-Zawahiri, Mwenyezi Mungu (swt) amrehemu. Hivi ndivyo viongozi wa umbile la katili wanavyofanya sasa; wanamwaga damu zetu na wanaivunjia heshima Masra (mahali pa Isra) ya Mtume wetu (saw), ili kwa uhalifu wao wanyanyue viwango vyao, kwani damu yetu ndio kipimo kinachowainua miongoni mwa watu wao!

Uhalifu wa "wanyonge" unaendelea kwa uwepo wao wa kuendelea kwenye Ardhi Iliyobarikiwa. Kuwepo kwao ndio jinai kuu, bali ndio mama wa jinai na chanzo chake, na jinai ya kumuua al-Ja’bari na ndugu zake ilitanguliwa na jinai zisizohesabika. Uvamizi wao dhidi ya Palestina na watu wake na Al-Aqsa yake haukomi.

Ama kundi la watawala vibaraka ni kundi linalomfanyia khiyana Mwenyezi Mungu, Mtume wake, Waislamu na damu zao. Hawasukumwi na ari ya kuulinda Uislamu wala fahari ya wanadamu, wao si chochote zaidi ya zana za usaliti. Dori yao katika kila jinai inayotendwa na maadui zetu ni kuzuia athari zake na kukaza mtego wao kwa Waislamu ili kuwaweka pingu na kunywa udhalilifu. Misheni yao baada ya kila uhalifu ni kuosha damu na kudhibiti matokeo, kutokana na wasiwasi wao kwa umbile la Kiyahudi, ambalo wanalijali kwa vile wanavyolijali wenyewe. Wao ni watawala waovu, bali ni watumwa wa maadui zetu, ambao wana uwezo tu wa kutekeleza amri za mabwana zao huko Washington na London, na dori lao imejulikana na kurudiwa mara kwa mara baada ya kila uhalifu unaofanywa na umbile la Kiyahudi; dori ya mshirika katika ukimya, uangaziaji, njama na uratibu wa usalama.

Enyi Watu Wetu Katika Ardhi Iliyobarikiwa: jinai za umbile la Kiyahudi hazikomi, na watawala wa Waislamu wanahusika na uvamizi katika jinai zake, ushabiki wao wa vyombo vya habari kamwe hautailinda damu yenu na Aqsa yenu, na hili linawahusu watawala wa Iran, Misri, Qatar...nk. Wote ni gora moja katika uhalifu.

Suala la Palestina linatokana na Uislamu, na ukombozi wake ni jukumu la Umma wa Kiislamu na majeshi yake. Kwa ajili hiyo, elekezeni wito wenu kwa Ummah wenu ili Swalah al-Din aibuke ndani yake. Tunawaambia makundi na Mujahidina: Elekezeni wito wenu kwa Ummah wenu na majeshi yake na mukate mafungamano yenu na watawala wahalifu, kwani Uislamu na Umma wa Kiislamu ndio msingi wa kimaumbile kwa ajili ya Palestina na watu wake, na haijuzu kuzitegemea tawala za kihaini, kuzitegemea, au kuziamini, kwani zimethibitisha kwa kila uvamizi dhidi ya Ummah na matukufu yake kwamba wao wako kwenye kambi ya maadui zetu, na kwamba dori yao imepita mipaka ya usaliti hadi ulaji njama. Hatua za usuluhishi na za kutuliza zinazofanywa hivi sasa na tawala za Qatar na Misri, au madai ya kupunguza ukolaji moto zilizoanzishwa na Mamlaka ya Palestina na utawala wa Jordan ni hatua zilizojaa usaliti pamoja na njama. Tunawatahadharisha watu wa Palestina na Mujahidina dhidi ya watawala hawa wasiojali damu ya watu wa Palestina kwa lolote. Wao wanajali tu kutaka kuwadhibiti watu na kuwazuia wasifanye jihad katika njia ya Mwenyezi Mungu, na wanajali maslahi na usalama wa umbile la Kiyahudi; hii ndio dori yao ambayo imekuwa jambo la kawaida mbele ya kila uhalifu unaofanywa na maadui zetu.

Ni kujiua kisiasa kwenda Umoja wa Mataifa na taasisi zake au kuiomba ile inayoitwa inayoitwa ya kimataifa, kwani hawa ndio wafadhili na waungaji mkono wa umbile la Kiyahudi na jinai zake. Taasisi za kimataifa si chochote zaidi ya zana zinazotumiwa na wahalifu wakubwa "dola mkubwa" katika kutekeleza jinai zao dhidi ya Waislamu.

Hivyo basi, kila sauti isiyohutubia Umma wa Kiislamu na majeshi yake, au kumuomba adui yake kuulinda na adui wake; ni sauti ya kulaumiwa, ambayo makusudio yake ni kugeuza mazingatio kutoka upande wa haki, sahihi wenye uwezo wa ukombozi, na kupurukusha kutoka kwenye mazungumzo yenye ufanisi na ya kusisimua, ambayo ni mazungumzo yanayo amsha katika Umma wa Kiislamu imani yake. Jukumu la kuikomboa Ardhi Iliyobarikiwa liko shingoni mwa maafisa wa jeshi la Misri, Jordan, Pakistan na Uturuki; liko kwenye shingo za maafisa na askari wa Waislamu katika nchi zote za Kiislamu; wao ndio wamiliki wa sababu, na kuwaacha na kuwatenga kwenye mazungumzo na kisha kwenda Amerika na taasisi za kimataifa ni usaliti mkubwa… zaidi ya usaliti.

Enyi Waislamu: Katika historia yote, Bait Al-Maqdis imekuwa sababu inayounganisha Umma wa Kiislamu. Inakusanya nguvu zake na kushinda udhaifu wake kwayo, na kumshinda adui yake. Katika nchi yake iliwashinda Makruseda na kuwashinda Wamongolia. Ummah wa Kiislamu leo ​​unaweza kuling'oa umbile nyakuzi la Kiyahudi kutoka kwenye mizizi yake, na kuwahofisha wale walio nyuma yake; bali, unaweza kuzuia uvamizi wa kila mtu anayefikiria kuushambulia. Udhaifu uliotokea ndani yake ni wa muda mfupi kutokana na usaliti wa watawala wake ambao wana nia ya kukufanyeni muonekane madhaifu na kukufanyeni kuwapandikiza kasumba hii kwa watoto wenu. Umbile la "waovu" ni dhaifu; askari wao sio jasiri kukabiliana na mapambano ya moja kwa moja. Wakisikia mlio wa ndege za Pakistan na Uturuki, mngurumo wa vifaru vya Misri, na milio ya mizinga ya Jordan, mutawakuta wameuawa katika maeneo yao kwa hofu na uoga. Basi muonyesheni Mwenyezi Mungu (swt) kutokana na nafsi zenu yale yatakayowastahiki ushindi wake juu yenu.

Enyi Majeshi ya Waislamu: Tunaomba nusra yenu na tunawahutubia kutoka katika Ardhi Iliyobarikiwa kwa maneno ya Mwenyezi Mungu (swt):

[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا مَا لَكُمْ إِذَا قِيلَ لَكُمُ ‌انْفِرُوا فِي سَبِيلِ اللَّهِ اثَّاقَلْتُمْ إِلَى الْأَرْضِ أَرَضِيتُمْ بِالْحَيَاةِ الدُّنْيَا مِنَ الْآخِرَةِ فَمَا مَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا فِي الْآخِرَةِ إِلَّا قَلِيلٌ * إِلَّا تَنْفِرُوا يُعَذِّبْكُمْ عَذَاباً أَلِيماً وَيَسْتَبْدِلْ قَوْماً غَيْرَكُمْ وَلَا تَضُرُّوهُ شَيْئاً وَاللَّهُ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ]

Enyi mlio amini! Mna nini mnapo ambiwa: Nendeni katika Njia ya Mwenyezi Mungu, mnajitia uzito katika ardhi? Je, mmeridhia maisha ya dunia kuliko ya Akhera? Lakini starehe za maisha ya dunia kulinganisha na ya Akhera ni chacheKama hamwendi atakuadhibuni adhabu chungu, na atawaleta watu wengine, wala nyinyi hamtamdhuru chochote. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu. [At-Tawba: 38-39]

Na, wallahi, mnaweza kulifanya umbile la Kiyahudi kuwa historia, na kuwafukuza walio nyuma yake miongoni mwa dola za kikoloni. Kwani adui yenu anashauku zaidi ya maisha, na nyinyi mna shauku ya kufa kishahidi na kukombolewa kwa Masra ya Mtume wenu (mahali pa Isra). Kwa hivyo, musipotoshwe na uhalali dhaifu, upuuzaji na upangaji njama wa watawala au kuhalalisha kwao nguvu ya kijeshi ya umbile la Kiyahudi, au dhurufu za kimataifa, kwani sisi hatushindi kwa wingi wa idadi au silaha, bali kwa imani ya Waumini na azma ya wakweli, na kumtegemea Al-Qawi Al-Aziz, Ambaye peke yake ndiye anayeleta ushindi. Hivyo basi, tegemeeni Dini yenu na muwe wakweli kwa Mwenyezi Mungu, Yeye (swt) atakuwa mkweli kwenu na mnusuruni Yeye (swt) na yeye atakunusuruni.

Na wito wa Hizb ut Tahrir kwenu ni kauli ya Mwenyezi Mungu (swt):

[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنْ تَنْصُرُوا اللَّهَ ‌يَنْصُرْكُمْ وَيُثَبِّتْ أَقْدَامَكُمْ]

Enyi mlio amini! Mkimnusuru Mwenyezi Mungu naye atakunusuruni na ataithibitisha miguu yenu. [Muhammad: 7].

[إِنْ ‌يَنْصُرْكُمُ اللَّهُ فَلَا غَالِبَ لَكُمْ وَإِنْ يَخْذُلْكُمْ فَمَنْ ذَا الَّذِي ‌يَنْصُرُكُمْ مِنْ بَعْدِهِ وَعَلَى اللَّهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُؤْمِنُونَ]

Akikunusuruni Mwenyezi Mungu hapana wa kukushindeni, na akikutupeni ni nani, basi, baada yake Yeye ataye kunusuruni? Na Waumini wamtegemee Mwenyezi Mungu tu. [Aal-i-Imran: 160].

Basi, muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume (saw) na sogeeni kuviangamiza viti vya enzi vya madhalimu na tembeeni kuelekea kwenye Ardhi Iliyobarikiwa ili kuikomboa, huku mkitamka Tahlil na Takbir. Naapa kwa Yeye (swt) aliyeziinua mbingu bila ya nguzo, huu ni wito wa haki ambao ndani yake mna utukufu wa dunia, ushindi na mafanikio ya Akhera, na radhi kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Ewe Mwenyezi Mungu, wafikishie kheri hii Waislamu na majeshi yao kutoka kwetu na uzifungue nyoyo zao na kwa ajili yake. Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote.

H. 9 Muharram 1444
M. : Jumapili, 07 Agosti 2022

Hizb-ut-Tahrir
Ardhi ya Baraka-Palestina

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu