Ijumaa, 09 Muharram 1447 | 2025/07/04
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ujumbe kutoka Hizb ut Taharir / Wilayah Lebanon Wamzuru Mbunge Osama Saad

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon katika mji wa Sidon, ukiwakilishwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Mawasiliano, Mhandisi Bilal Zaidan na Mjumbe wa Kamati ya Amali katika mji wa Sidon, Hajj Hassan Nahhas, walimtembelea Mwakilishi Osama Saad leo, Jumatano, Disemba 11, 2024. Ujumbe huo uliwasilisha msimamo wa Hizb kuhusu matukio mbalimbali hasa yanayojiri katika eneo hali ya Syria, Lebanon na kanda kwa jumla.

Soma zaidi...

Hotuba ya Kisiasa mjini Port Sudan Haki ya Kisheria ya Waislamu katika Dhahabu, Petroli, na Rasilimali Nyenginezo

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilitoa hotuba ya kisiasa mbele ya Klabu ya Al-Shabiba katika Soko Kuu la Port Sudan, mnamo siku ya Jumatatu tarehe 7 Jumada al-Akhirah 1446 H, sawia na 9/12/2024 M, yenye kichwa: “Haki ya Kisheia ya Waislamu katika dhahabu, petroli na rasilimali nyenginezo”, ambapo Ustadh Ahmed Abkar, wakili, mjumbe wa baraza la Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan alizungumza, ambapo ilifafanua mali ya umma kuwa ni vitu vilivyoainishwa na sheria kwa ajili ya jamii, vinavyoshirikiwa kati yao, na kukatazwa kumilikiwa na mtu binafsi peke yake.

Soma zaidi...

Marekani Yaogopa Kuangamia kwa Tawala za Vibaraka katika Nchi za Waislamu na Kuibuka kwa Khilafah

Marekani haiachi kuonyesha hofu yake ya kuangamia kwa tawala vibaraka katika nchi za Waislamu mara kwa mara. Hofu hii inaonekana kwenye ndimi za viongozi wake; Mshauri wake wa Usalama wa Kitaifa Jake Sullivan anathibitisha kwamba itafanya kazi kuimarisha Jordan, umbile la Kiyahudi (Kizayuni), na Iraq ili mzozo wa Syria usihamia kwao. Siku chache zilizopita, Waziri wake wa Mambo ya Nje Antony Blinken alisisitiza katika hotuba yake kabla ya Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa NATO juu ya ulazima wa kuzuia kuregea kwa Dola ya Khilafah.

Soma zaidi...

Mumempindua Dhalimu wa ash-Sham, Basi Msikubali Chochote baada ya Dhalimu huyo Zaidi ya Utawala wa Uislamu na Dola yake, Khilafah

Baada ya miaka kumi na nne ya mihanga mikubwa ya watu wa Syria katika mapinduzi yao yaliyobarikiwa, Damascus ilikuwa kwenye miadi ya ushindi alfajiri ya leo, Jumapili 8 Disemba 2024, kwa Idhini ya Mwenyezi Mungu (swt). Mwenyezi Mungu (swt) alitubariki kwa kupinduliwa kwa dhalimu Assad, baada ya zama za dhulma, uhalifu na udhalimu wa familia ya Assad katika utawala wake wa chuki, wa kimadhehebu kwa muda wa miaka 54. Katika zama zao, walipiga vita Dini, Shariah na waja wa Mwenyezi Mungu (swt). Waliwatia watu kila aina ya mateso. Hakuna ushahidi bora zaidi wa hili kuliko idadi ya kutisha ya wafungwa ambao waliachiliwa huru kutoka kwa magereza yake ya dhulma, maovu.

Soma zaidi...

Hongera Ash-Sham na Watu wake kwa Kumpindua Mtawala dhalimu na Utawala wake, Sasa ni Mbele Kuelekea Khilafah Rashida

Asubuhi ya leo, Jumapili tarehe 8/12/2024 M, na katika siku ya 12 ya operesheni ya “Kuzuia Uvamizi”, wapiganaji waliweza kuingia katika mji mkuu wa Syria, Damascus, na kupindua utawala wa Bashar al-Assad, ambaye Reuters iliripoti - ikiwanukuu maafisa wa Syria – kwamba aliuacha mji mkuu na kuelekea kusikojulikana. Hivyo, wapiganaji wa upinzani waliweza kuikomboa Idlib, Aleppo, Hama, Homs na Damascus, na kuwaachilia maelfu ya wafungwa waliokuwa wakizuiliwa na utawala wa kihalifu katika vyumba vya chini vya jela zake ovu kwa miaka na miongo kadhaa.

Soma zaidi...

Watawala wa Bara Arabu Wanashindana katika Ufisadi na Utiifu kwa Maadui wa Ummah!

Siku chache zilizopita, watawala wa Imarati walijigamba juu ya uhamasishaji wao mkubwa wa kuwafikia wauaji wa Rabbi wa Kiyahudi, Zvi Kogan, kwenye ardhi zao, na kupongeza umakini wa vyombo vya usalama na kasi ya taratibu zao zilizochangia kufichua tukio hilo, baada ya huduma hizi zote kufanya kwa muda wote, kulingana na yale yaliyoelezwa katika taarifa ya Wizara ya Mambo ya Ndani. Wakati huo huo, Imarati na Wizara yake ya Ulinzi haikujitolea kuwanusuru zaidi ya mashahidi elfu 44 na elfu 104 waliojeruhiwa huko Gaza, ingawa muuaji wao anajulikana na haihitaji uchunguzi au umakini wa vyombo vya usalama kumfikia.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi Hajj Mustafa Abdullah Al-Issa Al-Jaber Al-Aboushi (Abu Anas)

Kwa imani katika qadhaa ya Mwenyezi Mungu (swt) na kutaka malipo Yake, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Jordan inamuomboleza Mbebaji Da’wah katika safu zake: Hajj Mustafa Abdullah Al-Issa Al-Jaber Al-Aboushi (Abu Anas) Aliyefariki kwenda kwenye rehema za Mwenyezi Mungu Mtukufu asubuhi ya leo, Jumanne, 3/12/2024, akiwa na umri wa miaka 80.

Soma zaidi...

Maamuzi ya Mkutano wa GCC ni Ushirikiano katika Dhambi na Udanganyifu

Mnamo Jumapili, tarehe 1 Disemba 2024, katika taarifa ya mwisho iliyotolewa na kikao cha 45 cha Baraza Kuu la Baraza la Ushirikiano wa Ghuba iliyoandaliwa na Serikali ya Kuwait, viongozi wa nchi za Baraza la Ushirikiano wa Ghuba (GCC) na wawakilishi wao walitoa wito wa kumalizwa kwa uhalifu wa mauaji na adhabu ya pamoja huko Gaza, uhamishaji wa wakaazi, uharibifu wa vifaa na miundombinu ya raia. Walitoa wito wa kuingilia kati kulinda raia, kusitisha vita, na kufadhili mazungumzo mazito ili kufikia suluhu endelevu, wakisisitiza misimamo yao madhubuti kuhusu kadhia ya Palestina, kukomesha uvamizi huo, na uungaji mkono wao kwa uhuru wa watu wa Palestina juu ya ardhi zote za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu tangu Juni 1967, na kuanzishwa kwa dola huru ya Palestina na Jerusalem Mashariki kama mji mkuu wake, na kuhakikisha haki za wakimbizi, kwa mujibu wa Mpango wa Amani wa Kiarabu na maazimio ya uhalali wa kimataifa. Kuhusiana na Lebanon, viongozi hao walithibitisha mshikamano kamili na Lebanon.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu