Alhamisi, 08 Muharram 1447 | 2025/07/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Je, Barabara ya kuelekea Quds inapitia Mogadishu?!

Mnamo siku ya Jumamosi, Waziri Mkuu wa Misri Dkt. Mostafa Madbouly alithibitisha uungaji mkono usioyumba wa Misri kwa taifa ndugu la Somalia na kujitolea kwake katika kuimarisha umoja wa nchi hiyo. Alibainisha kuwa “kipindi kijacho kina ahadi kubwa kwa watu wa Somalia.” Madbouly alisema, “Kufikia umoja wa Somalia na kuunga mkono ndugu zetu wa Somalia katika awamu hii ni mojawapo ya vipaumbele vya juu vya dola ya Misri,”

Soma zaidi...

Je, Wananchi na Jeshi la Kifahari la Tunisia Wanakubali Mapokezi ya Waziri wa Ulinzi wa wale Wanaoua Ndugu zao mjini Gaza?!

Mnamo Jumatano, Agosti 28, 2024, Jenerali Michael Langley, Kamanda wa Kamandi ya Amerika ya Afrika (AFRICOM), alisema wakati wa mkutano wake na Waziri wa Ulinzi wa Tunisia Khaled El-Suhaili kwamba Tunisia iko mstari wa mbele katika nchi za Kiafrika zenye ushirikiano wa kihistoria na wa kipekee. Marekani, ikielezea utayari wake wa kuendeleza na kupanua mahusiano haya. Ziara hii inajiri siku tatu baada ya kuapishwa kwa wajumbe wa serikali.

Soma zaidi...

Komesheni Kupigania Vyeo na Marupurupu katika Jeshi la Pakistan. Badala yake, Maafisa wa Jeshi Waislamu Lazima Watoe Nusrah kwa ajili ya Kusimamisha Khilafah Rashida

Katikati ya utakaso wa sasa na kuwekwa kando maafisa ambao wanampinga mkuu wa sasa wa jeshi la Pakistan, ilijiri kutajwa kwa Hizb ut Tahrir. Gazeti maarufu la Kiurdu la “Daily Jang,” liliripoti mnamo tarehe 13 Agosti 2024, katika toleo lake kwa jiji la jeshi la Rawalpindi kwamba, “(2011) Brigedia Ali Khan alifikishwa mahakama ya kijeshi kwa kuwa na uhusiano na shirika lenye itikadi kali la Hizb ut Tahrir. Pia alituhumiwa kwa kueneza uasi ndani ya Jeshi la Pakistan.”

Soma zaidi...

Mamlaka ya Palestina Iliyofungamana na Maadui wa Mwenyezi Mungu Yakamilisha Dori ya Ghadhabu katika Kuwatesa Watu wa Palestina na Kuwakamata Watetezi wa Haki

Siku chache zilizopita, vikosi vya usalama vya Mamlaka ya Ndani ya Palestina (PA) viliwakamata Sheikh Aws Abu Arqoub na Sheikh Muhammad Manasrah, wanachama wa Hizb ut Tahrir. Kwa kuwakamata wale wanaosema ukweli, PA na vikosi vyake vinasisitiza kuwa kiongozi wa Mayahudi, wakidunga visu watu wote wa Palestina.

Soma zaidi...

Mgogoro wa Nishati nchini Jordan na Suala la Ufisadi wa Kiuchumi wa Mradi wa Al-Attarat, Utiifu wa Kisiasa, na Kuongezeka kwa Deni

Ripoti ya habari ya Shirika la Habari la Jordan, Petra, ya tarehe 6 Agosti 2024, ilisema kwamba “Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi iliamua kwamba serikali wala Kampuni ya Kitaifa ya Umeme hazihitajiki kulipa sehemu yoyote ya gharama kwa Kampuni ya Umeme ya Al-Attarat.” Habari hizi za upotoshaji zinakusudiwa kuficha hasara inayotarajiwa ambayo serikali ya Jordan itaipata kutokana na ukweli wa hukumu hiyo, inayosema: “Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi inaamuru kwamba mkataba huo ni halali na hauhusishi ukosefu mkubwa wa haki.”

Soma zaidi...

Mlima Geneva Umefanya Kazi Na Kuzaa Panya Aliyekufa!!

Jana, Ijumaa, Agosti 23, 2024, mkutano wa Geneva, ulioanza Agosti 14 kujadili mgogoro wa Sudan, ulihitimishwa kwa kuunda “Muungano wa Umoja wa Kimataifa” ili kumaliza vita nchini Sudan. Kwa mujibu wa Mjumbe Maalum wa Marekani nchini Sudan, Tom Prillo, muungano huo unajumuisha, pamoja na Marekani, Umoja wa Mataifa, Muungano wa Afrika, IGAD, pamoja na Uswizi, Saudi Arabia, UAE na Misri. Hata hivyo, pamoja na urefu wa majadiliano ya Geneva, matokeo hayana thamani ya halisi katika kusimamisha vita vya kikatili vinavyoendelea nchini Sudan.

Soma zaidi...

Ardhi Iliyobarikiwa - Palestina Sio Karata ya Uchaguzi kwa Ruwabidha Mzembe

Mnamo siku ya Jumatatu, tarehe 19/8/2024, Rais wa Algeria Abdelmadjid Tebboune alitoa wito kwa Misri kufungua mipaka na Ukanda wa Gaza kwa jeshi la Algeria, ili kuwanusuru wakaazi wa Ukanda wa Gaza, na kusema: “Naapa kwamba haraka iwezekanavyo tutapeleka vitengo huko na kujenga upya kile kilichoharibiwa,” na akasema: “Jeshi la Algeria liko tayari kwenda Gaza na sisi tuko tayari, tunasubiri tu Misri itufungulie mipaka yake.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu