Ijumaa, 09 Muharram 1447 | 2025/07/04
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Damu za Waislamu zinamwagika huku watawala wao wakishuhudia na hakuna suluhu!

Umbile la Kiyahudi linaendeleza uvamizi wake dhidi ya watu wa Palestina na linaendelea na jinai zake mbele ya masikio na macho ya walimwengu, bila kuzuiwa na azimio au hukumu yoyote ya Umoja wa Mataifa kutoka Mahakama ya Kimataifa. Idadi ya mashahidi waliohesabiwa imezidi 40,000, na pengine idadi sawia bado wamenaswa chini ya vifusi. Idadi ya waliojeruhiwa inakaribia 100,000, huku wale waliosalia wakiwa hai wanateseka sana kutokana na njaa.

Soma zaidi...

Marekani Yarefusha Vita ili Kufikia Ajenda yake, Kuteketeza Watu, Miti, na Mawe - Hakuna Njia ya Kutoweka Isipokuwa Kupitia Khilafah!

Mnamo Jumapili, Agosti 11, 2024, mikutano ya Jeddah ilikamilika kati ya wajumbe kutoka serikali ya Sudan na Mjumbe Maalum wa Marekani nchini Sudan, Tom Periello, bila kufikia maelewano yoyote kuhusu ajenda ya mazungumzo na waangalizi. Baada ya kuregea kwa wajumbe wa mazungumzo, serikali ilitoa taarifa ikibainisha kushindwa kwa ujumbe wa Marekani kuwasukuma wanamgambo wa waasi kujitolea kutekeleza Azimio la Jeddah.

Soma zaidi...

Mwanachama Mwengine wa Hizb ut Tahrir Atiwa hatiani kwa Kutoa Wito wa Ukombozi wa Palestina: Historia Itakumbuka Neno la Kweli na Wahalifu wa Kweli

Siku 303 baada ya mauaji ya halaiki ya Wazayuni yanayoungwa mkono na Denmark dhidi ya raia wa Gaza, hukumu nyengine imetolewa katika Mahakama ya Wilaya ya Copenhagen dhidi ya mwanachama wa Hizb ut Tahrir kwa kutoa wito wa ukombozi wa kijeshi wa Palestina.

Soma zaidi...

Kama Umma Mmoja: Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa Kuangamizwa kwa Dhalimu Hasina na Tunawaombea Kuporomoka Madhalimu Wote Wanaoukandamiza Ummah

Baada ya majuma kadhaa ya ukandamizaji wa kikatili dhidi ya watu wa Bangladesh na dhalimu Hasina, genge la serikali yake, na wachungaji wake wa kigeni, alilazimishwa kidhalilifu kuikimbia nchi. Waislamu shupavu wa Bangladesh, wakiongozwa na wanafunzi jasiri, walivumilia ukatili usio na kifani na hatimaye kulazimisha kuondolewa kwake kupitia wimbi lisilozuilika la maandamano ambayo yalimshinda dikteta huyo.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yaandaa Maandamano mjini Al-Qadarif Kutaka Kukomeshwa kwa Vita na Umwagaji damu ya Waislamu

Mnamo siku ya Ijumaa, Agosti 2, 2024, Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan iliandaa maandamano katika mji wa Al-Qadarif baada swala ya Juma’a karibu na Jami’ Al-Atiq (Msikiti Mkongwe) katika Soko la Al-Qadarif. Maandamano hayo yalitaka kukomeshwa kwa vita na umwagaji damu ya Waislamu.

Soma zaidi...

Njaa: Silaha Halisi ya Ubepari Mbali na Usanii wa Kipuuzi wa Misaada ya Kibinadamu ya Marekani

Samantha Power, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID), alitoa taarifa akionyesha kuzorota kwa hali ya kibinadamu katika kambi ya IDP ya Zamzam nchini Sudan. Alibainisha kuwa matumaini yametoweka, nafasi yake kuchukuliwa na hofu, kwani wataalamu kutoka mfumo wa Uainishaji wa Awamu ya Usalama wa Chakula ulithibitisha kuwa njaa imeendelea kambini humo kwa zaidi ya mwezi mmoja.

Soma zaidi...

Umbile la Mayahudi wa Kizayuni Linakiuka Matukufu Yetu Lipendavyo, Huku Watawala wa Waislamu Wakiyafungia Majeshi Yetu kwenye Kambi Zao

Mnamo asubuhi ya tarehe 31 Julai 2024, umbile la Kiyahudi lilimuua shahidi kiongozi wa Hamas Ismail Haniyeh katika shambulizi la kombora jijini Tehran, mji mkuu wa Iran. Siku moja kabla, umbile hilo la Kiyahudi lilimuua shahidi kamanda wa Hezbollah kwa kushambulia jengo la makaazi jijini Beirut, Lebanon. Hapo awali, umbile la Kiyahudi lilishambulia vituo mbalimbali katika bandari ya Hodeida nchini Yemen kwa ndege za kivita. Hii ni huku Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina ikiwa imegeuzwa kuwa magofu katika kipindi cha miezi kumi iliyopita.

Soma zaidi...

Umbile la Halifu la Mayahudi Kukiuka Nafasi za Ummah na Kuua Watu wake katika Miji Mikuu ni Uhalifu wa Tawala za Kioga mbele ya Umbile la Kiyahudi

Katika shambulizi la kiuhaini na lisilo na aibu, umbile halifu la Kiyahudi lilimuua mkuu wa afisi ya kisiasa ya Hamas jijiniTehran, ambapo Ndugu Ismail Haniyeh aliuawa shahidi alfajiri ya leo na adui wa Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, na Umma. Tunamuomba Mwenyezi Mungu rehema na msamaha wake na amjaalie miongoni mwa mashahidi. Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na hakika kwake Yeye tutaregea.

Soma zaidi...

Serikali ya Jordan Kuanzisha Afisi ya NATO ni Uhalifu dhidi ya Palestina na Gaza na Usaliti kwa Umma wa Kiislamu

Huku Wamagharibi wakikata tamaa ya uwezo wa tawala vibaraka katika nchi za Kiislamu kuendelea kudhibiti na kutawala mambo, na uhakika wake kwamba Ummah unakaribia kuzifagilia mbali tawala hizi na kuziondoa, na hivyo kuondoa uwepo wao katika nchi zetu; kwa kuzingatia haya yote, hatua hii ilitoka kwa NATO, ili wao wenyewe waweze kusimamia utekelezaji wa mipango yao na kulinda maslahi yao katika ardhi zetu, na kulinda umbile la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu