Jumamosi, 21 Muharram 1446 | 2024/07/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mauaji ya Kikatili dhidi ya Watu Wetu mjini Gaza Bila Uwajibikaji! Lini Tutayaona Majeshi ya Waislamu Yakiinuka?!

Wizara ya Afya mjini Gaza imetangaza kuwa mashahidi 79 na majeruhi zaidi ya 289, baadhi yao wakiwa katika hali mahututi, wamewasili katika hospitali ya Nasser Medical Complex kufuatia mashambulizi ya mabomu kwa kambi za watu waliokimbia makaazi yao huko Mawasi Khan Yunis. Mauaji haya yanajiri baada ya uvamizi huo kufanya mauaji ya kutisha katika eneo la viwandani la kitongoji cha Tel al-Hawa, katika vitongoji vya Mji wa Gaza, na katika kambi za eneo la kati, na kusababisha zaidi ya mashahidi 100, na kuongeza kwa kasi idadi ya majeruhi.

Soma zaidi...

Serikali Vibaraka Zinalipa Uhai Umbile la Mayahudi. Usaliti wa Siri sasa Umekuwa wa Dhahiri!

Chini ya kichwa, "Kuendesha daraja la ardhini kati ya bandari za Haifa na Dubai, kupita Saudi Arabia na Jordan, kuvipita vitisho vya Mahouthi," wavuti ya arabi21.com uliripoti, ukitoa mfano wa Vyombo vya habari vya Kiebrania, kwamba, "Imarati (UAE ) na dola inayokalia kimabavu zilitia saini makubaliano ya kuendesha daraja la ardhini, kati ya bandari za Dubai na Haifa, likipitia katika eneo la Saudia na Jordan, kwa lengo la kuvipita vitisho vya Mahouthi vya kufunga njia za kupitia meli.

Soma zaidi...

Taarifa kwa Vyombo vya Habari Mtume (saw) amesema, «مَنْ ‌حَمَلَ عَلَيْنَا السِّلَاحَ فَلَيْسَ مِنَّا» “Yeyote atakayebeba silaha dhidi yetu, si katika sisi.” Chini ya Kisingizio cha Usumbufu, Mamlaka ya Palestina Inashirikiana na Mvamizi katika Ucho

Mamlaka ya Palestina (PA) ilifanya uhalifu wa kinyama zaidi Jumatano hii asubuhi kwa kumuua kijana Abdulqader Zaqdah, ambaye alijeruhiwa wakati wa uvamizi wao kwenye kambi ya Tulkarm. Wengine kadhaa pia walijeruhiwa.

Soma zaidi...

Kuhuisha Sheria ya Hifadhi ya Jamii ni Uhalifu na Kunyima Riziki ya Watu na Mfereji Mpya Ulioongezwa na Mamlaka ya Palestina Kushambulia Ukakamavu na Uchumi wao

Kwa ujanja na hila, siku hizi Mamlaka ya Palestina (PA) inatafuta kufufua Sheria maarufu ya Hifadhi ya Jamii, ambayo watu walisimama imara dhidi yake miaka iliyopita, kukataa kushambuliwa kwa mali zao, matunda ya juhudi zao na riziki zao kwa kisingizio cha "kuwadhamini!"

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu