Alhamisi, 09 Shawwal 1445 | 2024/04/18
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Vichwa vya Habari 16/09/2022

Vichwa vya Habari:

Viongozi wa Jamii ya Waislamu Wajumuika Pamoja Kuimba 'Mungu Muokoe Mfalme'

Mafanikio ya Ghafla ya Ukraine Yazusha Maswali Mapya kwa Makamanda

Imran Akutana na Balozi wa zamani wa Marekani Robin Raphael

Maelezo:

Viongozi wa Jamii ya Waislamu Wajumuika Pamoja Kuimba 'Mungu Muokoe Mfalme'

Waislamu katikati mwa London waliimba wimbo wa taifa katika msikiti mmoja wa Uingereza kwa mara ya kwanza tangu kifo cha Malkia Elizabeth II. Waabudu walihudhuria ibada katika Msikiti huo wa Katikati mwa London katika Bustani ya Regent ya kuheshimu maisha ya malkia na kuashiria kutawazwa kwa Mfalme Charles III. Ahmad Al Dubayan, wa Kituo cha Utamaduni cha Kiislamu na Msikiti Mkuu wa London, alisema lengo lilikuwa "kuonyesha huruma na hisia za jamii za Kiislamu nchini Uingereza". Alisema kwamba malkia huyo “alipendwa na kila mtu” na kwamba Waislamu aliowajua walikuwa “wenye shukrani sana na walitambua mambo yote aliyofanya.” Alisifu kujitolea kwa malkia kwa tamaduni nyingi na "kujitolea kwake kwa huduma ya kila mtu ambayo ilifanya Uingereza kuwa chemichemi ya uhuru". Wimbo wa taifa uliimbwa ibada ilipomalizika, ambayo waandaaji walisema ni mara ya kwanza tangu kifo cha malkia huyo kwa wimbo wa Mungu Muokoe Mfalme kuimbwa katika msikiti wa Uingereza. Mwenyekiti wa Bodi ya Kimataifa ya Prince's Trust, Shabir Randeree, alikuwepo na alielezea kama "wakati wa kusisimua sana". "Ilisimasha nywele nyuma ya shingo yangu kwa sababu mbili," alisema. “Kwanza, nilifurahi sana kusimama msikitini nikiimba Mungu Muokoe Mfalme. Na ya pili, bila shaka niliguswa sana katika kujaribu kumkumbuka Malkia. "Ilikuwa wakati muhimu na wakati wa kugusa sana." "Jumuiya ya Waislamu imeunganisha kila mtu, na mumeona huzuni nyingi, sio tu kutoka kwa jamii ya Waislamu lakini kutoka kwa jamii zote za Uingereza, na, nasubutu kusema, katika Jumuiya ya Madola na kote ulimwenguni vilevile. "Nadhani ni muhimu sana kwa jamii ya Waislamu kuwa hapa nje na kusema wanachohisi, na pia kuwa na familia ya kifalme na wengine na nchi nzima kutambua kwamba wanaomboleza sana kifo cha malkia." Alisema: "Nadhani Mfalme Charles ataendelea na kazi ya malkia katika suala la mahusiano ya kidini. Ni eneo ambalo amekuwa na shauku kubwa. "Kuwa na maingiliano kwa jamii zote ndio kitovu cha imani yake." [Chanzo: The National]

Familia ya sasa ya Kifalme ya Uingereza imeongoza maovu kadha wa kadha yaliyofanywa na serikali ya Malkia katika ulimwengu wa Kiislamu, hivi karibuni zaidi ni vita vya Afghanistan na Iraq. Ilhali licha ya hayo, Waislamu nchini Uingereza wanaonekana kuchanganyikiwa na kitambulisho chao. Utiifu kwanza kabisa ni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake (saw) na sio kwa Malkia au Mfalme!

Mafanikio ya Ghafla ya Ukraine Yazusha Maswali Mapya kwa Makamanda

Jeshi la Ukraine linapima ni umbali gani vikosi vyake vinaweza kushinikiza shambulizi, kwa hatari ya uwezo wao wa kushikilia safu mpya. Viongozi wa Urusi wanajaribu kujipanga upya baada ya machafuko makubwa na ya kukatisha tamaa. Baada ya mashambulizi ya kustaajabisha ya Ukraine katika eneo la kaskazini-mashariki kuvifanya vikosi vya Urusi kurudi nyuma kwa machafuko na kurekebisha uwanja wa vita kwa mamia ya maili, viongozi wa Ukraine mnamo Jumatatu walikuwa wakipima fursa muhimu ambazo zingeweza kuamua mkondo wa karibu wa vita. Kunyoosha vikosi vya Ukraine - jeshi ambalo bado ni ndogo sana na halina vifaa vya kutosha kuliko adui wake wa Urusi - mbali sana kunaweza kuwaacha wanajeshi katika hatari ya kushambuliwa. Kusonga polepole sana, au mahali pasipofaa, kunaweza kuiacha fursa hiyo kufujwa. Na kungoja kwa muda mrefu kunaweza kuruhusu safu za mbele kuganda wakati msimu wa baridi unapoanza. Kwa kuwafukuza wanajeshi wa Urusi kutoka sehemu kubwa ya eneo la kimkakati katika mkoa wa kaskazini-mashariki wa Kharkiv, vikosi vya Ukraine sasa viko tayari kusonga mbele kwenye Donbas, eneo la mashariki lenye viwanda ambalo rais wa Urusi, Vladimir V. Putin, ameweka msingi wa malengo yake ya vita. Muda mfupi kabla ya mafuriko ya askari kuvuka mpaka mwezi Februari, Bw. Putin alitangaza Donbas kuwa huru kutoka kwa Ukraine, na alishikilia uhuru wa eneo hilo kama sababu kuu ya uvamizi huo. Urusi sasa ina udhibiti wa karibu asilimia 90 ya Donbas, ambapo jeshi lake lilibadilisha mwelekeo wake baada ya kushindwa kwa kushangaza karibu na mji mkuu, Kyiv, katika majira ya mchipuko. Endapo Ukraine itaichukua tena sehemu ya eneo hilo, itakuwa pigo la aibu kwa Kremlin. Mnamo Jumatatu, jeshi la Ukraine lilidai kuwa lilisonga mbele katika siku iliyopita katika miji na vijiji 20 vya Ukraine katika eneo la Kharkiv ambavyo vilikuwa chini ya udhibiti wa Urusi, na kuongeza mamia ya maili za mraba ambayo imechukua tena kaskazini mashariki. Pia ilisema kuwa imefanikiwa kutwaa tena takriban maili 200 za mraba katika eneo la kusini la Kherson katika siku za hivi karibuni, huku vikosi vyake vikijaribu kukata maelfu ya vikosi vya Urusi vilivyoko magharibi mwa Mto Dnipro. Madai hayo ya jeshi hayakuweza kuthibitishwa huru, lakini wachambuzi wa Magharibi, pamoja na Pentagon, walisema kwamba Waukraine walikuwa wanapata mafanikio haraka kama vile kurudi nyuma kwa vikosi vya Urusi. Maafisa wa Urusi wanakabiliwa na maswali magumu yao wenyewe, haswa kutokana na kuongezeka kwa upinzani kwa "operesheni yao maalum ya kijeshi" kutoka kwa sauti zinazounga mkono vita za nyumbani. Viongozi wa kijeshi wa Urusi, wachambuzi wanasema, itabidi waangalie kwa uwazi uhalisia wa hali ya sasa ya vikosi vyao - iliyopungua na iliyokatishwa tamaa katika baadhi ya maeneo - ili kubaini ni kiasi gani cha malengo ya Moscow wanaweza kuyatimiza katika miezi ijayo, iwapo yapo yoyote. [Chanzo: New York Times]

Mafanikio mapya ya Ukraine yanaonyesha jinsi Marekani imetumia vyema wanajeshi wa Ukraine walio na silaha za Marekani kuwapa Warusi mapambano makali. Huu ni ukumbusho wa Marekani kuwapa silaha Mujahhidina wa Afghanistan kukabiliana na hali kama hiyo kwa wanajeshi wa Urusi nchini Afghanistan. Na inaonekana kwamba Warusi hawajajifunza kutokana na kufeli kwa misheni zao za kigeni.

Imran Akutana na Balozi wa zamani wa Marekani Robin Raphael

Balozi wa zamani wa Marekani na mchambuzi wa CIA Bi Robin Raphael Jumapili alitoa wito kwa Mwenyekiti wa PTI na waziri mkuu wa zamani Imran Khan huko Banigala. Ilifahamika kwamba wote wawili walijadili masuala ya maslahi ya pande zote, hasa katika mazingira ya uhusiano wa Pakistan na Marekani. Kiongozi wa Upinzani katika Seneti Dkt Shehzad Waseem pia alikuwepo katika mkutano huo. Hakukuwa na taarifa kuhusu mkutano huo kutoka kwa kiongozi yeyote wa PTI, msemaji au idara kuu ya vyombo vya habari. Makamu wa rais mkuu wa PTI na waziri wa zamani wa habari Chaudhry Fawad Hussain pia alikutana na Balozi wa Marekani nchini Pakistan Donald Blome katika Ubalozi wa Marekani mnamo Septemba 8. Huko nyuma mwaka wa 1993, Robin Raphel aliteuliwa na Rais wa wakati huo Bill Clinton kama Waziri Msaidizi wa Kigeni wa Mambo ya Asia Kusini na Kati. Maingiliano ya uongozi wa PTI na maafisa wa Marekani unaonekana kama jaribio la kukuuza uhusiano mzuri na Washington. Wiki chache nyuma, iliripotiwa sana kwenye vyombo vya habari kwamba PTI iliajiri kampuni ya ushawishi na Uhusiano wa Umma ya Marekani kwa gharama ya $25,000 kwa mwezi ili kusimamia mahusiano yake ya umma na vyombo vya habari nchini Marekani. Hati zilizowasilishwa na Wizara ya Haki ya Marekani chini ya Sheria ya Usajili wa Mawakala wa Kigeni (FARA) zinaonyesha kampuni ya ushawishi ya Fenton/Arlook itatoa huduma za mahusiano ya umma, ikijumuisha lakini sio kufungika tu na kusambaza habari kwa wanahabari, kuweka makala na matangazo, kupanga mahojiano na wawakilishi au wafuasi wa PTI, kushauri juu ya juhudi za mitandao ya kijamii na huduma zingine kama hizo za uhusiano wa umma. Mkataba kati ya kampuni hiyo na PTI-USA Inc umetiwa saini kwa muda wa miezi sita. Mkataba huo unataja kwamba mteja hajumuishi PTI, chama cha kisiasa kilichosajiliwa nchini Pakistan. Nyaraka za FARA chini ya vifungu vyake pia zinaangazia, "PTI USA katika hali fulani inaelekezwa na chama cha siasa cha kigeni nchini Pakistan." Kadhalika, imeripotiwa pia na kujadiliwa katika duru za kisiasa na vyombo vya habari rasmi na visivyo rasmi kwamba kampuni ya ushauri ya Kimarekani, inayoendeshwa na mkuu wa zamani wa kituo cha CIA jijini Islamabad, imejidhihirisha kuwa iliajiriwa kwa niaba ya PTI kushawishi na kutoa ushauri juu ya mahusiano ya Pakistan na Marekani. Robert Laurent Grenier wa Grenier Consulting LLC aliajiriwa mwaka jana wakati PTI ilikuwa bado mamlakani. Makubaliano na kampuni hiyo yalitiwa saini na Iftikhar ur Rehman Durrani mnamo Julai 2021 chini ya "usimamizi wa maafisa wakuu wa chama cha [PTI] na chini ya uelekezi wa maafisa wa serikali ya Pakistan". [Chanzo: The News International]

Hata mtu wa kawaida anaanza kutilia shaka ikhlasi ya Khan dhidi ya mazingira ya mikutano na maafisa wa zamani wa Amerika, huku akishikilia Amerika inahusika kwa kuondolewa kwa Khan afisini. Maneno ya Khan ya serikali iliyoagizwa kutoka nje yanazidi kuonekana kuelezea juhudi zake za kuifurahisha Marekani na kumfungulia njia ya kutwaa mamlaka.

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu