Kupigwa Marufuku kwa Hizb ut Tahrir? – Kufilisika kwa Demokrasia
- Imepeperushwa katika Denmark
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kufuatia kampeni ya uzushi ya kibinafsi dhidi ya mmoja wa wanachama wetu iliyofanywa na vyombo vya habari na wanasiasa—kutokana tu na matamshi na maadili yake ya Kiislamu—pande zote tatu za serikali ya Denmark sasa zimejadidisha wito wao wa kisiasa wa kupiga marufuku Hizb ut Tahrir nchini Denmark. Hii ni mbali na wanasiasa wa mara ya kwanza wa Denmark kucheza “karata ya upigaji marufuku” kutokana na kutapatapa kifikra. Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma, kwa nyakati tatu tofauti, amegundua kwamba hakuna msingi wa kikatiba wa upigaji marufuku wa aina hiyo.



