Jumamosi, 11 Jumada al-awwal 1447 | 2025/11/01
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Umbile la Kiyahudi ndilo Tatizo Kubwa zaidi katika Nchi za Kiislamu Na Waungaji Mkono wake ndio Tatizo Kubwa Zaidi Duniani Ewe Trump!

Vyombo vya habari viliripoti taarifa ya Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu Gaza, ambapo alisema, “Gaza ni tatizo kubwa kwa Israel na Mashariki ya Kati.” Hatujamsikia hata mmoja wa watawala wajinga wasio na maana (ruwaibidha) katika nchi za Kiislamu akimjibu, akimwambia kwamba umbile nyakuzi la Kiyahudi ndilo tatizo kubwa katika nchi za Kiislamu, na kwamba nyinyi ndio mnaliruzuku zana za kijeshi na msaada wa kisiasa na kiuchumi. Nyinyi ndio tatizo kubwa katika ulimwengu wote. Mfumo wenu wa kibepari ndiyo sababu ya masaibu ya dunia, na nyinyi ndio sababu ya kugawanyika kwa nchi za Kiislamu katika dola dhaifu na maumbo hafifi tiifu kwenu.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wakutana na Mkurugenzi wa Khalawi na Idara za Misikiti katika Mji wa Port Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan ukiongozwa na Ustadh Nasser Ridha Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail Mjumbe wa Kamati ya Mawasiliano, ulimtembelea Sheikh Onour Muhammad Ahmed, Mkurugenzi wa Khalawi na Idara za Misikiti katika Mji wa Port Sudan, afisini kwake, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb kutibua njama ya kuichana Sudan kwa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Marekani ya Kibeberu Inatumia Wakala Wake Shirika la Excelerate Energy kutia Udhibiti juu ya Bandari na Bahari zetu za Kimkakati ili Kuendeleza Udhibiti wake wa Kisiasa

Balozi wa zamani wa Marekani nchini Bangladesh Peter D Haas alifanya mkutano wa karibu saa moja na Waziri wa Mambo ya Nje Asad Alam Siam mnamo Alhamisi (4 Septemba). Ingawa hakuna upande uliofichua maelezo ya majadiliano hayo, vyanzo vya habari viliripoti kuwa mazungumzo hayo yalihusu uwezekano wa kuagiza LNG kutoka Marekani, pamoja na ushirikiano wa sasa na miradi ya mustakabali. Kwa sasa Haas anatumika kama Mshauri wa Kimkakati wa Excelerate Energy - shirika la kimataifa la Texas ambalo linaendesha kituo cha LNG kinachoelea huko Maheshkhali, Cox’s bazar.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Wakutana na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Wanazuoni katika Jimbo la White Nile

Jana, Jumatatu, tarehe 8/9/2025, huko Rabak, mji mkuu wa Jimbo la White Nile, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilayah ya Sudan ulikutana na Sheikh Abdullah Al-Nur Tutu, Imam na Khatib wa Msikiti Mkuu wa Asalaya na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Wanazuoni wa Sudan, Tawi la White Nile, nyumbani kwake katika kitongoji cha Asalaya. Ujumbe huo uliongozwa na wafuatao Dkt. Ahmad Mohammad, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, akifuatana na Ustadh Faisal Madani, Abdul Majeed Osman Abu Hajar, na Al-Zein Abdul Rahman, wanachama wa Hizb ut Tahrir. Mkutano huo ulikuwa sehemu ya kampeni ya Hizb ut Tahrir ya kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...

Wahanga wa Vita Wanaoteseka Zaidi ni Watoto wa Gaza wenye Ulemavu

Vita vya maafa dhidi ya Gaza, vilivyoanza mnamo Oktoba 7, 2023, vimeathiri kila nyanja ya maisha huko: watu, miti, mawe, na rasilimali, hasa wanawake na watoto. Vifo na uharibifu vimeenea kila mahali. Kulingana na Wizara ya Afya mjini Gaza, vimesababisha vifo vya zaidi ya watu 63,000, kujeruhiwa kwa wengine 160,000, na mamia ya maelfu ya watu kuyahama makaazi yao, huku kukiwa na janga kubwa la kibinadamu linalojumuisha uhaba wa chakula, dawa, na maji safi ya kunywa.

Soma zaidi...

Kutoka “Wizara ya Ulinzi” hadi “Wizara ya Vita”: Ni Wakati wa Kuchunguza upya Maana ya Ulinzi wa Kiislamu

Kwa kutolewa kwa agizo kuu na Donald Trump, jina la Wizara ya Ulinzi ya Marekani lilibadilishwa rasmi kuwa “Wizara ya Vita.” Haya hayakuwa tu mabadiliko ya jina; iliweka wazi fikra ya uvamizi ya dola za kikoloni na sera ya nje ya nchi za Magharibi inayoongozwa na ukaliaji kimabavu. Trump alisema wazi wazi: “Ulinzi ni wa kujihami sana ... lakini tunataka kuanza mashambulizi pia.”

Soma zaidi...

Ndani ya Muundo wa Kampeni ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Kuvuruga Mpango wa Kutenganisha Darfur Wanachama wa Hizb ut Tahrir katika Mji wa Al-Obeid Wahutubia Wito Mzito kwa Waislamu katika Msikiti Mkuu wa Al-Obeid na Kubeba Mabango katika Amali Ny

Katika amali mbili tofauti, Mashababu (wanachama) wa Hizb ut Tahrir katika mji wa Al-Obeid, mnamo Jumamosi tarehe 06/09/2025, na ndani ya muundo wa kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan ya kuvuruga mpango wa kuichana Sudan kwa kutenganisha Darfur, na kwa kuzingatia kwamba umoja wa Umma ni suala nyeti ambalo kwalo kipimo ni uha na kifo.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wakutana na Mkuu wa Chama cha Adalah nchini Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, ukiongozwa na Ustadh Al-Nadir Muhammad Hussein, mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, akifuatana na Mhandisi Banqa Hamid, na Ustadh Issam al-Din Abdul Qadir, wanachama wa Hizb ut Tahrir, walimtembelea Ustadh Al-Tijani Abdul Wahab, mkuu wa Chama cha Adalah nchini Sudan, nyumbani kwake katika mji wa Al-Obeid, mnamo Ijumaa tarehe 05/09/2025, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ili kutibua mpango wa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Matendo ya Watawala wa Sudan na Misri Kuhusu Bwawa la An-Nahdha Upotevu wa Usalama wa Maji kwa Watu wa Bonde la Nile

Utaratibu wa mashauriano baina ya nchi mbili unaojulikana kama 2+2, unaojumuisha mawaziri wa mambo ya nje na unyunyiziaji maji wa Misri na Sudan, walifanya mkutano katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri mnamo Jumatano, 3/9/2025, kujadili maendeleo katika faili la Bwawa la Grand Ethiopian Renaissance (GERD). Mkutano huo ulisababisha taarifa ya pamoja ambapo pande hizo mbili zilieleza makubaliano yao kamili kuhusu hatari ya hatua za upande mmoja zinazochukuliwa na Ethiopia kuhusu ujazaji na uendeshaji wa bwawa la GERD. Taarifa hiyo iliashiria hatari kadhaa zinazohusishwa na bwawa hilo, ikiwa ni pamoja na dhamana dhaifu ya usalama, mtiririko wa maji usio wa kawaida, na athari zinazoweza kutokea wakati wa ukame.

Soma zaidi...

Maslahi ya Nani Yanatumikiwa kwa Uamuzi wa Serikali wa Kufungua Tena Kivuko cha Mpakani cha Adre huku Watu wa Fashir Wakifa kwa Njaa?!

Serikali ya Sudan ilitangaza mnamo Jumanne kwamba itaongeza muda wa ufunguzi wa kivuko cha mpakani na Chad cha Adre kwa mashirika ya misaada ya kibinadamu hadi mwisho wa mwaka huu. Wizara ya Mambo ya Nje ilitoa taarifa ikisema kwamba hatua hii inathibitisha dhamira ya serikali ya kuhakikisha kwamba misaada ya kibinadamu inawafikia wale wanaohitaji nchini kote, na kuonyesha nia yake njema katika kuwezesha shughuli za kibinadamu.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu