Alhamisi, 28 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/18
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

“Amali” kama Pazia la Ukaliaji wa Kimabavu

Yale yanayoitwa makubaliano kati ya dola vamizi “Israel” na Hamas, yaliyopangwa na Washington, yanawasilishwa katika vyombo vya habari vya Magharibi na kwa masikitiko pia katika sehemu za ulimwengu wa Kiislamu kama hatua kuelekea amani. Kiulisia, si kitu chengine ila ni marudio ya mtindo wa zamani: mradi wa kikoloni “Israel” unaimarishwa na kulindwa zaidi, huku jinai zake zikifinikwa na vazi la “amani.”

Soma zaidi...

Ni lini Tutakomesha Uingiliaji wa Kafiri Magharibi na Mashirika yake ya Kikoloni katika Maisha Yetu, na Kuelekeza Nyuso Zetu Kwa Al-Waahid, Al-Haakim?

Chini ya ufadhili wa shirika la Ufaransa la Promediation, vyama vya kisiasa vya Sudan vilifanya warsha jijini Port Sudan, kama ilivyoripotiwa kwenye tovuti ya Sudan Tribune mnamo tarehe 5 Oktoba 2025: “Warsha inalenga kufafanua vigezo vya mazungumzo ya mustakbali yatakayoongozwa na Sudan, ikiwemo washiriki wake, eneo, na dori ya upatanishi wa kimataifa, kulingana na msemaji wa kambi hiyo Mohammed Zakaria. Viongozi wa muungano huo walisisitiza haja ya muungano wa ndani ulioshikamana. Minni Arko Minnawi, mkuu wa kamati ya kisiasa ya umoja huo, alisema hatua ya pamoja kati ya viongozi wa kiraia na kijeshi ni muhimu kwa ajili ya utulivu.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Chukueni Hatua na Msiache Masuala Yenu Yawe Mikononi mwa Maadui Zenu

Mazungumzo ya awamu ya kwanza ya mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump kusimamisha vita dhidi ya Gaza yalianza mjini Sharm El-Sheikh nchini Misri, kwa kuhudhuriwa na wajumbe wa Marekani Steve Witkoff na Jared Kushner, Waziri Mkuu wa Qatar, na wakuu wa kijasusi wa Uturuki na Misri.

Soma zaidi...

Machozi ya Furaha kwa Maadui wa Mwenyezi Mungu, Kushindwa na Kukata Tamaa kwa Waislamu nchini Cyprus

Aprili iliyopita, Baraza la Mawaziri la Cyprus Kaskazini lilitoa “amri ya kiserikali” ambayo inaruhusu wanafunzi kuvaa hijabu za Kiislamu katika shule za sekondari. Hata hivyo, Muungano wa Walimu wa Sekondari wa Cyprus na Uturuki (KTOEOS), ulianza migomo, ukakataa kufundisha watoto waliofika shuleni wakiwa wamevalia mavazi ya kidini, na hatimaye wakaiomba Mahakama Upeo. Wiki iliyopita (mwisho wa Septemba), Mahakama ya Upeo ya Cyprus Kaskazini ilibatilisha “amri ya kiserikali”, ikiamua kuwa ilikuwa kinyume na katiba. Viongozi wa Muungano huo wa Walimu, ambao waliomba kubatilishwa kwa amri hiyo, walisherehekea kuregea kwa marufuku ya hijabu kama “ushindi kwa usekula” kwa kububujika “machozi ya furaha”. Wakati huo huo serikali imetangaza kuanza mara moja “kufanyia kazi sheria mpya”.

Soma zaidi...

Kauli za Uhalalishaji Mahusiano ni Tangazo la Wazi la Kuoanishwa na Adui na Kujitenga na Ummah

Siku za hivi karibuni zimeshuhudia msururu wa kauli zilizotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Badr Abdelatty wakati wa ushiriki wake katika makongamano ya kimataifa. Maarufu zaidi kati ya kauli hizi ni msisitizo wake juu ya “umuhimu wa 'Israel' kuishi kwa amani na kuoanishwa ndani ya eneo hili,” na “utayari kamili wa kuhalalisha mahusiano na ‘Israel’" pamoja na Saudi Arabia na nchi zengine, na kauli yake kwamba “suluhisho pekee kwa mustakbali ni kuanzishwa kwa dola ya Palestina isiyo na kijeshi inayoishi kwa amani na ‘Israel’.” Kauli hizi waziwazi zinaakisi mwelekeo unaofuatwa na tawala zilizoko katika nchi za Kiislamu: njia iliyojaa uhalalishaji mahusiano na umbile nyakuzi, na hata juhudi za kulilinda na kulioanisha ndani ya eneo hili, kuhudumia mradi wa kikoloni wa Magharibi.

Soma zaidi...

Suluhisho la Dola Mbili ni Kejeli ya Karne isiyo na Aibu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh inashutumu vikali kile Prof. Yunus alisema kwenye Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa, “Ni kwa msingi wa mipaka ya kabla ya 1967 tu, na Israel na Palestina wakiishi bega kwa bega kwa amani, haki inaweza kutendeka”. Wakati watu wa Palestina wanaangamizwa mbele ya macho yetu na Mayahudi kunyakua 78% ya Palestina kinyume cha sheria, ni vipi haki inaweza kutendeka kwa kuruhusu ‘Israel’ kuishi bega kwa bega na Palestina! Kwa nini tunaita makundi machache ndani ya umbile haramu la Kiyahudi kuwa ni dola (Palestina), lakini haina hata jeshi lake?

Soma zaidi...

Misri Imenaswa Kati ya Kiu na Mafuriko! Gharama ya Miongo Kadhaa ya Uzembe na Mapuuza

Mgogoro wa mafuriko ambayo yalisomba baadhi ya vijiji vya Misri, na kuzamisha nyumba za makumi ya familia, ni sehemu moja tu ya mgogoro mkubwa na hatari zaidi. Mgogoro huu ni uzembe wa serikali juu wa haki za maji za Misri na kupuuza kwake kwa muda mrefu masuala ya wananchi na usimamizi wa rasilimali za nchi kwa ajili ya kulinda usalama wake na maslahi ya wananchi wake. Mgogoro huu haukutokea ghafla. Badala yake, ni matokeo ya mrundikano mtawalia wa sera zilizofeli ambazo zimekausha serikali zana zake za ulinzi wa maji na kufungua mlango kwa Ethiopia kudhibiti njia ya uhai wa Misri na Sudan kupitia Bwawa Kuu la An-Nahdha la Ethiopia.

Soma zaidi...

Baada ya Mashambulizi ya Umbile la Kiyahudi kwa Sumud Flotilla Wito wa Dharura kwa Maafisa na Askari katika Majeshi ya Waislamu Jeshi Husagwa sagwa na Jeshi Pekee

Enyi Wanajeshi: Mumeshuhudia shambulizi la umbile la Kiyahudi dhidi ya Sumud Flotilla iliyosafiri bahari ili kuvunja kuzingirwa kwa kaka na dada zenu mjini Gaza, na mkasikia vilio vyao vya kuomba msaada, na mkaona kwa macho yenu uovu wa watawala, ufisadi wao, ukosefu wao wa hisia, na kufeli kwao kuinusuru Gaza na wanaharakati wa flotilla. Imekudhihirikieni pia kwamba watawala hao walimfanyia khiyana Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kuwaangusha Waumini walipoangusha hadharani kile walichokiita “chaguo la vita” kwa kunyenyekea matamanio ya viongozi wa ukafiri.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu