Jumatano, 25 Shawwal 1446 | 2025/04/23
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Uvamizi wa Umbile la Kiyahudi na Mashambulizi Yake ya Kiadui kwenye Ardhi ya Ash-Sham Jinai zinazoendelea ambazo ni Utawala wa Uislamu na Dola Yake ya Khilafah Pekee ndio Unaoweza Kusitisha na Kuvunja Nguvu yao

Tangu kuanguka kwa dhalimu Assad mnamo tarehe nane mwezi huu, makundi ya umbile la Kiyahudi yamekuwa yakishambulia ardhi ya Ash-Sham, na ndege zake zimekuwa zikivamia anga yake kwa mashambulizi ya angani yenye nia mbaya ambayo yalilenga miji kadhaa, na maeneo ya kijeshi. Mashambulizi haya yamefika katika mji wa Deir ez-Zor mashariki mwa Syria. Mashambulizi hayo ya chuki na kihalifu yamejikita kwenye maghala ya silaha, vikosi vya ulinzi wa anga katika maeneo ya kati na kusini, vituo vya utafiti wa kisayansi wa kijeshi, na viwanja vya ndege vya kijeshi, ikiwa ni pamoja na uwanja wa ndege wa kijeshi wa Al-Mazzeh viungani mwa Damascus.

Soma zaidi...

Matukio ya Uhalifu Yanayofichuliwa Katika Magereza ya Dhalimu wa Ash-Sham Yanapasa Kuwasha Moto Nyoyoni mwa Wana wa Ummah Kuwateketeza Watawala

Katika siku chache zilizopita baada ya kutoroka kwa dhalimu Bashar na kuanguka kwa utawala wake muovu, matukio ya uchungu na makali yalifichuliwa ambayo yalivunja nyoyo za Waislamu. Kwani waliona kwa macho yao ukubwa wa jinai na ukatili ambao utawala wake uliamiliana nao kwa ndugu na dada zao katika vituo vya uzuizi na magereza: kuanzia na kuwekwa kwao kizuizini kwa miongo kadhaa katika magereza ambayo yalikosa mahitaji msingi zaidi ya kibinadamu, kisha njaa, ukandamizaji na mateso ya kikatili ambayo magereza hayo na kuta zinayazungumzia, na seli, nguzo na zana za mateso zinazosimulia hadithi zao, na miili ya wahasiriwa waliopatikana wamekufa na kukatwakatwa inamfichua.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Taharir / Wilayah Lebanon Wamzuru Mbunge Osama Saad

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon katika mji wa Sidon, ukiwakilishwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Mawasiliano, Mhandisi Bilal Zaidan na Mjumbe wa Kamati ya Amali katika mji wa Sidon, Hajj Hassan Nahhas, walimtembelea Mwakilishi Osama Saad leo, Jumatano, Disemba 11, 2024. Ujumbe huo uliwasilisha msimamo wa Hizb kuhusu matukio mbalimbali hasa yanayojiri katika eneo hali ya Syria, Lebanon na kanda kwa jumla.

Soma zaidi...

Hotuba ya Kisiasa mjini Port Sudan Haki ya Kisheria ya Waislamu katika Dhahabu, Petroli, na Rasilimali Nyenginezo

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilitoa hotuba ya kisiasa mbele ya Klabu ya Al-Shabiba katika Soko Kuu la Port Sudan, mnamo siku ya Jumatatu tarehe 7 Jumada al-Akhirah 1446 H, sawia na 9/12/2024 M, yenye kichwa: “Haki ya Kisheia ya Waislamu katika dhahabu, petroli na rasilimali nyenginezo”, ambapo Ustadh Ahmed Abkar, wakili, mjumbe wa baraza la Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan alizungumza, ambapo ilifafanua mali ya umma kuwa ni vitu vilivyoainishwa na sheria kwa ajili ya jamii, vinavyoshirikiwa kati yao, na kukatazwa kumilikiwa na mtu binafsi peke yake.

Soma zaidi...

Marekani Yaogopa Kuangamia kwa Tawala za Vibaraka katika Nchi za Waislamu na Kuibuka kwa Khilafah

Marekani haiachi kuonyesha hofu yake ya kuangamia kwa tawala vibaraka katika nchi za Waislamu mara kwa mara. Hofu hii inaonekana kwenye ndimi za viongozi wake; Mshauri wake wa Usalama wa Kitaifa Jake Sullivan anathibitisha kwamba itafanya kazi kuimarisha Jordan, umbile la Kiyahudi (Kizayuni), na Iraq ili mzozo wa Syria usihamia kwao. Siku chache zilizopita, Waziri wake wa Mambo ya Nje Antony Blinken alisisitiza katika hotuba yake kabla ya Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa NATO juu ya ulazima wa kuzuia kuregea kwa Dola ya Khilafah.

Soma zaidi...

Mumempindua Dhalimu wa ash-Sham, Basi Msikubali Chochote baada ya Dhalimu huyo Zaidi ya Utawala wa Uislamu na Dola yake, Khilafah

Baada ya miaka kumi na nne ya mihanga mikubwa ya watu wa Syria katika mapinduzi yao yaliyobarikiwa, Damascus ilikuwa kwenye miadi ya ushindi alfajiri ya leo, Jumapili 8 Disemba 2024, kwa Idhini ya Mwenyezi Mungu (swt). Mwenyezi Mungu (swt) alitubariki kwa kupinduliwa kwa dhalimu Assad, baada ya zama za dhulma, uhalifu na udhalimu wa familia ya Assad katika utawala wake wa chuki, wa kimadhehebu kwa muda wa miaka 54. Katika zama zao, walipiga vita Dini, Shariah na waja wa Mwenyezi Mungu (swt). Waliwatia watu kila aina ya mateso. Hakuna ushahidi bora zaidi wa hili kuliko idadi ya kutisha ya wafungwa ambao waliachiliwa huru kutoka kwa magereza yake ya dhulma, maovu.

Soma zaidi...

Hongera Ash-Sham na Watu wake kwa Kumpindua Mtawala dhalimu na Utawala wake, Sasa ni Mbele Kuelekea Khilafah Rashida

Asubuhi ya leo, Jumapili tarehe 8/12/2024 M, na katika siku ya 12 ya operesheni ya “Kuzuia Uvamizi”, wapiganaji waliweza kuingia katika mji mkuu wa Syria, Damascus, na kupindua utawala wa Bashar al-Assad, ambaye Reuters iliripoti - ikiwanukuu maafisa wa Syria – kwamba aliuacha mji mkuu na kuelekea kusikojulikana. Hivyo, wapiganaji wa upinzani waliweza kuikomboa Idlib, Aleppo, Hama, Homs na Damascus, na kuwaachilia maelfu ya wafungwa waliokuwa wakizuiliwa na utawala wa kihalifu katika vyumba vya chini vya jela zake ovu kwa miaka na miongo kadhaa.

Soma zaidi...

Watawala wa Bara Arabu Wanashindana katika Ufisadi na Utiifu kwa Maadui wa Ummah!

Siku chache zilizopita, watawala wa Imarati walijigamba juu ya uhamasishaji wao mkubwa wa kuwafikia wauaji wa Rabbi wa Kiyahudi, Zvi Kogan, kwenye ardhi zao, na kupongeza umakini wa vyombo vya usalama na kasi ya taratibu zao zilizochangia kufichua tukio hilo, baada ya huduma hizi zote kufanya kwa muda wote, kulingana na yale yaliyoelezwa katika taarifa ya Wizara ya Mambo ya Ndani. Wakati huo huo, Imarati na Wizara yake ya Ulinzi haikujitolea kuwanusuru zaidi ya mashahidi elfu 44 na elfu 104 waliojeruhiwa huko Gaza, ingawa muuaji wao anajulikana na haihitaji uchunguzi au umakini wa vyombo vya usalama kumfikia.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu