Jumanne, 07 Shawwal 1445 | 2024/04/16
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Enyi Waislamu…Waokoeni Watoto wa Yemen!

Mnamo 21/11/2018, ripoti ya Shirika la Uingereza la Okoa Watoto ilisema kuwa takribani watoto 85,000 chini ya umri wa miaka mitano wamekufa kutokana na ukosefu wa lishe bora ndani ya kipindi cha miaka mitatu ya vita ndani ya Yemen.  Idadi hii pekee ni sawa na jumla ya idadi ya watoto walioko chini ya miaka mitano ndani ya Birmingham, jiji la pili kubwa ndani ya Uingereza.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia Ilikuwa Mwenyeji wa Kongamano la Kimataifa la Wanawake “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu”

Mnamo Jumamosi 27 Oktoba, kwa Baraka za Allah, Alhamdulillah, Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kwa ushirikiano na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia kwa ufanisi kilifanya kongamano kubwa na la kuvutia la kimataifa la wanawake jijini Tunis lenye kauli mbiu, “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu” ili kuelezea sababu na suluhisho la Kiislamu juu ya mgogoro unaoathiri utulivu na umoja wa ndoa na maisha ya familia katika jamii kote ulimwenguni, ikiwemo biladi za Waislamu. Tukio hili muhimu lilihudhuriwa na zaidi ya wanawake 250 kutoka kote nchini Tunisia wakiwemo mawakili, walimu, walezi wa watoto, wahandisi, wanafunzi wa vyuo vikuu, viongozi wa jamii, na watetezi wa vijana. Hotuba zilitolewa na wanachama wa kike wa Hizb ut Tahrir kutoka Tunisia, Uturuki, Ardhi Iliyo Barikiwa – Palestina, Pakistan, Lebanon, Indonesia, Ghuba la Kiarabu. Uholanzi, na Uingereza. Kongamano hilo vile vile lilipeperushwa moja kwa moja mtandaoni kwa washiriki wa kimataifa na kutazamwa na maelfu ya watazamaji kutoka katika pembe tofauti tofauti duniani. 

Soma zaidi...

Yemen yakabiliwa na baa la njaa la kutisha lililowahi kutokea ndani ya miaka 100 ya ulimwengu likisababishwa na mzozo kati ya Uingereza na Marekani ambao umeutia nchi hiyo katika vita wasivyostahiki wakiongozwa na vibaraka wa kitaifa na kieneo!

Kwa mujibu wa duru za Umoja wa Mataifa, Yemen kwa sasa inakabiliwa na baa la njaa baya zaidi ulimwenguni kwa miaka 100. Uzani wa janga hilo umefananishwa na ule uliokumba Afrika katika miaka ya themanini. Ripoti ya hivi majuzi ya shirika la habari la BBC imenukuu kuwa kwa mujibu wa Lisa Grande, Msimamizi wa Misaada ya Kibinadamu wa UN nchini Yemen, zaidi ya raia milioni 13 wako katika hatari ya kufa kutokana na ukosefu wa chakula katika miezi mitatu ijayo

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia ni mwenyeji wa Kongamano la Kimataifa la Wanawake “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu” Lililoandaliwa na Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya

Mnamo Jumamosi 27 Oktoba 2018, Hizb ut Tahrir Wilayah ya Tunisia itakuwa mwenyeji wa kongamano muhimu la kimataifa la wanawake lililoandaliwa na Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kwa kichwa, “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu” ili kutatua janga linaloathiri uwiano na umoja wa ndoa na familia katika jamii ulimwenguni, ikijumuisha ardhi za Waislamu. Tukio hili adhimu litawakusanya wanawake waliopendekezwa kutoka Tunisia na nchi nyinginezo, ambao ni viongozi mashuhuri katika jamii zao au walio na ujuzi kuhusiana na mada hii.

Soma zaidi...

Kampeni ya Kimataifa: “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu” iliyo Zinduliwa na Kitengo cha Wanawake Katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

Mnamo 3 Oktoba, Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kilizindua kampeni muhimu ya kiulimwengu kwa anwani, “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu” ambayo itamalizikia katika kongamano la kimataifa la wanawake mwishoni mwa Oktoba litakalo hudhuriwa na wazungumzaji kutoka pembe zote za dunia.

Soma zaidi...

Faini ya Kwanza ya Denmark kwa Wanawake Wanaovaa Niqab Itawasukuma Waislamu Kushikamana na Maadili ya Kiislamu Hata Zaidi!

Mnamo Agosti 4, 2018, shirika la habari la BBC liliripoti juu ya mwanamke wa kwanza wa Kiislamu kulipishwa faini nchini Denmark kwa ajili ya kuvaa niqab hadharani. “Bunge la Denmark liliidhinisha mswada mnamo Mei 2018 wa kumwadhibu yeyote anayevaa niqab kwa faini” (BBC, 31 Mei 2018). Kwa sasa sheria hiyo haitaji burka na niqab kwa majina, bali inaeleza, “Yeyote anayevaa nguo inayofinika uso hadharani ataadhibiwa kwa faini”. Marufuku hiyo ilipangwa kuanza utekelezwaji wake mnamo Agosti 2018. Mnamo Ijumaa 3 Agosti 2018 mwanamke wa Kiislamu mwenye umri wa miaka 28 aliyekuwa amevaa niqab katika soko kuu la hadhara mjini Horshom, km 25 (maili 15) kaskazini mwa Copenhagen, alishambuliwa kwa nguvu na mwanamke mwengine aliyepinga vazi lake na kuchukua hatua mikononi mwake kumvua kwa lazima vazi hilo la Kiislamu. Polisi waliitwa katika eneo hilo la “vita” na baada ya kuangalia kanda ya CCTV walimweleza mwanamke huyo wa Kiislamu kuwa angelipishwa faini ya kroner 1,000 ($155; £120) baada ya kukataa kuvua niqab hiyo kwa agizo la polisi. Kwa sasa faini hiyo imeongezeka mara kumi zaidi hadi kroner 10,000 ($1,500; £1,200) kwa wahalifu wanaorudia kosa.

Soma zaidi...

Kifungo cha Watoto Wahamiaji cha Trump Chadhihirisha Umbile la Kinyama Lisilokubalika la Nidhamu ya Kitaifa ya Kidemokrasia ya Amerika

Chini ya sera ovu ya uhamiaji ya ‘kutokuwa na hata chembe ya uvumilivu’ ya Raisi wa Amerika, takriban watoto 2000, wengine wao wakiwa na umri mdogo wa miaka 4 au 5, ni miongoni mwa wale walioorodheshwa kama ‘wahamiaji haramu’, wametenganishwa kwa nguvu kutoka kwa wazazi wao katika mpaka wa Amerika na Mexico katika kipindi cha wiki sita pekee. Wametiwa ndani ya vibanda vya seng’enge katika vituo vya vizuizi, ambavyo hali zake zimesifiwa kuwa ‘mithili ya gereza’. Mojawapo ya vituo hivi vya wahamiaji katika jimbo la Texas kimepewa lakabu ya La Perrera, “kibanda cha mbwa”, ambamo watoto wanalala chini sakafuni juu ya magodoro membamba na makaratasi ndio blanketi zao. Kanda ya sauti ya watoto walioathirika kimawazo na kulia imepatikana, wakililia wazazi wao. Idara zimetangaza mipango ya kujenga mahema yatakayobeba mamia zaidi ya watoto katika jangwa la Texas ambako viwango vya joto kawaida hufikia nyuzi 40.     

Soma zaidi...

Risasi Zimechukua Maisha ya Watu … Na Serikali Zinacheza Densi Juu ya Majeraha!

Kwa mujibu wa mashirika ya habari; mtoto wa miezi 8 Laila Al-Ghandour alifariki mnamo Jumanne asubuhi eneo la Mashariki mwa Gaza baada ya kuvuta gesi. Tukio hili linaongeza idadi ya mashuhadaa wa “Msafara wa Mkubwa wa Maregeo” na kufikia idadi ya 61, wakiwemo watoto 7 na majeruhi 2,800, wengi wao wakiwa ni kutokana na risasi na wengine wakiwa ni kutokana na vipande vya mabomu na gesi ya sumu wakati wa uzimaji msafara na majeshi ya umbile la Kiyahudi iliyoanza maeneo tofauti Mashariki mwa ukanda wa Gaza katika kumbukumbu ya miaka 70 ya Nakba, na ambayo ilipinga na kukataa kuhamishwa kwa ubalozi wa Amerika jijini Al-Quds (Jerusalem).

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu