Jumapili, 02 Rajab 1447 | 2025/12/21
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Upenyaji wa Mayahudi wa Jeshi la Misri

Tangu serikali ya Misri itie saini Makubaliano ya Camp David mwaka 1979, jeshi la Misri limeingia katika njia ya utegemezi na upenywaji, likijitenga na kanuni yake ya awali ya kuulinda Ummah na kulinda mipaka yake dhidi ya maadui wake wa kweli, wa kwanza miongoni mwao ni Mayahudi walioinyakua Palestina. Hatua kwa hatua, taasisi hii imebadilika na kuwa chombo kilichozuiliwa, chini ya masharti ya adui, hata kushiriki katika kuilinda na kuiwezesha kupitia mikataba ya kijeshi, usalama, kiuchumi, na ushauri ambayo iliunda utaratibu kamili wa ushawishi wa Kiyahudi, ndani ya jeshi na dola.

Soma zaidi...

Tofauti Kubwa Kati ya Azimio la Istanbul na Fatwa Zilizotangulia!

Mwishoni mwa kongamano lao waliloliita “Gaza ni Jukumu la Kiislamu na la Kibinadamu” lililofanyika jijini Istanbul kwa siku sita la maulamaa, lililoandaliwa na Erdogan, walitoa tamko la mwisho. Walianza na aya za Qur’an kuhusu maandalizi na Jihad katika Njia ya Mwenyezi Mungu (swt), ili kwamba yeyote anayeisoma afikirie kwamba kitakachofuata kingekuwa ni programu ya kivitendo ya jinsi ya kujishughulisha mara moja na Jihad ambayo sio tu inaiondolea Gaza bali pia inaikomboa Palestina na al-Masjid al-Aqsa. Hata hivyo, uhalisia ulikuwa kinyume.

Soma zaidi...

Utegemezi wa Dola za Kikoloni za Kikafiri Humpora Mtu Utashi wa Kisiasa, Hupotosha Dira ya Mtu na Kupoteza Nguvu za Mtu

Kwa kuzingatia ukandamizaji unaoendelea Syria kwa matakwa ya Amerika na mfumo wa kimataifa, watu wanahisi wameporwa utashi wao, kukosa uwezo wa kufanya maamuzi yao wenyewe, na kuhofia mustakabali wao. Ili kuelewa ni nani anayeamua mambo nchini Syria na kwa nini tumepoteza uwezo wetu wa kufanya maamuzi, lazima tuhakiki mkondo wa mapinduzi ya Syria tangu mwanzo wake.

Soma zaidi...

Waziri wa Mambo ya Nje wa Denmark Ajifanya Kuijali Palestina, Huku Mikono Yake Ikiloa Damu ya Watu Wasio na Hatia wa Gaza

Tarehe 07-09-2025, Waziri wa Mambo ya Nje wa Denmark, Lars Løkke Rasmussen, alisafiri hadi Palestina inayokaliwa kwa mabavu na kukutana na marafiki zake na wenzake Wazayuni “kuonyesha kujali” na “kutia shinikizo” kwa serikali vamizi ya Kizayuni. Ziara hii ya kirafiki utawala vamizi wa Kizayuni inakuja siku chache tu baada ya Waziri wa Mambo ya Nje huyo kuchapisha video kwenye mtandao wa kijamii, ambapo alitoa maoni kwamba “Serikali ya Denmark sasa inachukua hatua za kuondoa kura ya turufu ya Israel juu ya msimamo wetu [kuhusiana na utambuzi wa baadaye wa Palestina]”.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wakutana na Mkurugenzi wa Khalawi na Idara za Misikiti katika Mji wa Port Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan ukiongozwa na Ustadh Nasser Ridha Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail Mjumbe wa Kamati ya Mawasiliano, ulimtembelea Sheikh Onour Muhammad Ahmed, Mkurugenzi wa Khalawi na Idara za Misikiti katika Mji wa Port Sudan, afisini kwake, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb kutibua njama ya kuichana Sudan kwa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Ghasia za Indonesia: Mabadiliko Ambayo (Bado) Yamefungwa?

Msiba wa Affan Kurniawan, dereva wa teksi ya pikipiki wa mtandaoni wa Indonesia aliyeuawa baada ya kugongwa na gari la polisi aina ya barracuda mnamo 28 Agosti 2025, uliishia katika msururu wa maandamano katika miji mingi kote Indonesia. Makala haya hayakusudii kujibu maswali, bali kuibua maswali kwa yeyote anayedai kuwa mwanaharakati wa Kiislamu.

Soma zaidi...

Swahaba Mtukufu Mus’ab ibn Umair, Mwenyezi Mungu (swt) Amuwie Radhi

Katika kundi la majina yenye kung'aa ya maswahaba watukufu, jina la Mus’ab bin Umair (ra) linajitokeza kama ishara ya muhanga na uthabiti. Mus’ab alikuwa mshika mwenge wa Da’wah katika hatua zake zote, kwani alikuwa ni kijana miongoni mwa vijana bora wa Makka, aliyejulikana kwa uzuri wake, harufu ya kupendeza, na maisha ya anasa, kiasi kwamba Maswahaba, Mwenyezi Mungu (swt) awawie radhi wote, wakasema juu yake, ما رأينا بمكة أحدا انعم عيشا من مصعب بن عمير “Hatujamuona mtu yeyote mjini Makka ambaye aliishi kwa neema kuliko Mus’ab bin Umair.”

Soma zaidi...

Mtihani wa Gaza

Mwenyezi Mungu (swt) hakumuumba mwanadamu bila ya kuweka mbele yake mitihani kulingana na ukubwa wa Imani yake na kujitolea kwake katika Dini, ili Mwenyezi Mungu (swt) apate kujua ni nani atakayekuwa na subira mbele ya mitihani hiyo na kuweka tegemeo lake (tawakkul) kwa Mwenyezi Mungu (swt) . Haya ni ili Mwenyezi Mungu (swt) amuepushe na fitna. Ama wale ambao watafeli ndani ya mitihani hiyo, watafeli tu kwa sababu ya hukumu yao mbaya, kughafilika kwao na Amri za Mwenyezi Mungu (swt), na Imani yao dhaifu.

Soma zaidi...

Iwe ni Suala la Mafuriko au Kashmir, Suala la Uchumi au Kukaliwa Kimabavu kwa Mito Yetu na Dola ya Kibaniani —Je, Tutaendelea Kungoja ‘Jumuiya ya Kimataifa’ Mpaka Lini Kutatua Matatizo Yetu?

Baada ya mafuriko makubwa katika majimbo ya kaskazini ya Khyber Pakhtunkhwa, hasa katika Buner na maeneo ya karibu, ambapo mamia ya watu walipoteza maisha na nyumba, mifugo, mali na magari kusombwa na maji, mafuriko mapya sasa yanapitia Punjab na baadaye yataelekea Sindh. Hapo awali, Karachi pia ilikumbwa na mvua kubwa. Tunamuombea Mwenyezi Mungu Mtukufu usalama na kheri, kwani pamoja na utabiri zaidi wa mvua, watawala wetu wameinua mikono juu tu na kuliacha suala zima kwa rehema ya jumuiya ya kimataifa. Wanaendelea kuwasilisha suala hili zima kwa namna ambayo ni kana kwamba haya ni mabadiliko ya tabianchi ambayo hayawezi kudhibitiwa kabisa na wao, na ikiwa ‘jumuiya ya kimataifa’ haitaingilia kati, wataachwa bila msaada kabisa – kana kwamba ulinzi wa maisha na mali ya watu wao sio jukumu lao bali ni la mfumo wa kimataifa!

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu