Lazima Tuitupilie Mbali Miungu ya Uongo na Miovu ya Utaifa na Ukabila Kwenye Jaa la Historia!
- Imepeperushwa katika Khilafah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kutokana na utaifa, ukabila na kuanzishwa kwa dola za kitaifa na mipaka yake katika ardhi za Waislamu, kitambulisho cha Waislamu kimeharibika na kutengana, ambapo Ummah wa Kiislamu hapo awali uliunganishwa katika udugu mmoja na ndani ya Dola moja ya Kiislamu, badala yake ukagawanyika katika dola za kitaifa zaidi ya 50 na vitambulisho vya kitaifa kufuatia kuvunjwa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab, 1342, mikononi mwa Mustafa Kamal, “baba wa udhalifu”.



